Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge Kuhusu Mapendekezo ya Kurejea Katiba ya Tume ya Usafiri wa Anga ya Afrika ya Mwaka 2009

Hon. Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge Kuhusu Mapendekezo ya Kurejea Katiba ya Tume ya Usafiri wa Anga ya Afrika ya Mwaka 2009

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipatia nafasi ili niweze kuchangia katika Katiba ya Usafiri wa Anga Afrika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kusema naunga mkono azimio hili kutokana na umuhimu wake. Pamoja na kuunga mkono nina mambo machache ya kuishauri Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kukubaliana kwa azimio hili ni kwamba tumekubali kuingia katika ushirikiano na ushindani wa kibiashara. Hata hivyo, kama tumekubali kuingia katika suala zima la ushindani wa kibiashara ni lazima tuangalie shirika letu. Je, lina uwezo wa kukabiliana na huo ushindani ambao tunakwenda kuingia?

Mheshimiwa Naibu Spika, ukirudi kwenye hali halisi ya shirika letu la usafirishaji limekuwa likikabiliana na changamoto nyngi sana. Vile vile, tumeona katika taarifa mbalimbali ikiwemo taarifa ya CAG namna ambavyo shirika hili limekuwa likikabiliana na matatizo makubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa kuwa tunakwenda kuingia kwenye ushindani wa kibiashara ni lazima Serikali ikubali kufanya mabadiliko kwenye suala zima la ushindani wa kibiashara ili twende tukafaulu kwenye suala zima la ushindani wa kibiashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeona kabisa kwenye taarifa ya CAG namna ambavyo shirika limepata hasara kwa miaka mitano mfululizo. Sasa kama tunakwenda kuingia kwenye ushindani wa kibiashara na tunaona kuna maeneo ambayo shirika letu linakwama, ni lazima tuwe na mambo ya kushauri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia taarifa ya CAG hiyo hiyo ya mwaka 2022, inasema wazi kabisa kwenye suala la ukaguzi wa mashirika ya umma namna ambavyo shirika lina madeni makubwa kuliko mtaji lilionao. Sasa, kama tunakwenda kuingia kwenye ushindani wa kibiashara ni lazima Serikali ikubali kuyatazama haya ili tusiende kuaibika huko mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa ya CAG inasema wazi kabisa kwamba mtaji ambao shirika lilikuwa nao ni bilioni 295.2, wakati huo madeni ambayo shirika linadaiwa ni bilioni 535. Tafsiri yake shirika lina mtaji hasiā€¦. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Stella, changia hoja ambayo iko mbele yako. Changia mjadala wa kuridhia kuingia katika huu Mkataba wa Civil Aviation.

MHE. STELLA S. FIYAO: (Hapa alizungumza bila kutumia kipaza sauti).

NAIBU SPIKA: Wewe hebu kaa kimya. Mimi naongea na wewe unasema, kama nani? Kuna shirika gani katika dunia sasa hivi linatengeneza faida kwenye ndege? Nitajie moja tu. Changia hoja iliyokuwepo mbele, kama umemaliza kaa chini. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Naibu Spika ni lazima tutoe angalizo kama Bunge. Ni vema Serikali ikajidhatiti katika kuwekeza kwenye shirika hili ili tupate matokeo yaliyo sahihi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza, naomba kuishauri Serikali iwekeze kwenye shirika hili ili liweze kujiendesha kibiashara. Jambo la pili, Serikali iwekeze kwenye shirika hili ili tuweze kuinuka kidedea katika suala zima la ushindani wa kibiashara. Hatuwezi kuingia kwenye ushindani wa kibiasharra kama Serikali haijakubali kuwekeza kwa asilimia mia moja kwenye shirika hili, tuta-fail na tutaaibika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo nataka kushauri, kumekuwa na changamoto nyingi za ukamataji wa ndege. Ni vema Serikali ipitie kesi za madai za kitaifa ili kuepusha changamoto ya ukamataji wa ndege na kuziingiza ndege zetu kwenye hatari ya kukamatwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kusema hayo naunga mkono Azimio, lakini naomba Serikali iyazingatie niliyoshauri. Nashukuru sana. (Makofi)