Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. LUCY S. MAGERELI: Mheshimiwa Mwenyekiti nipo. Naomba nikushukuru sana kwa kunipa fursa kuchangia. Niwie radhi kuwa nimeisikia sauti yako kuwa ningekuwa next, lakini ni suala jema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa mapaji mengi, lakini kwa kujaaliwa fursa ya kuwepo hapa leo ili na mimi nitoe mchango wangu katika Wizara iliyoko mbele yetu.
Naomba kabla sijaendelea niungane na nimpongeze sana Mheshimiwa Mama Janet Mbene, kwa kweli mchango wako nimekusikia wakati wote uliposimama, uliiongelea ajenda ambayo na mimi ningetamani sana tuendelee kuiangalia kwa nguvu. Niulize tu kwa Mawaziri wahusika, Wizara ya TAMISEMI na Utumishi na Utawala Bora kwamba where is the woman?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Koffi Annan aliwahi kusema “There is no tool for development more effective than empowerment of a woman.” (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, there is no tool for development more effective than empowerment for a woman. Sasa nimezitazama hotuba, nimekwenda mbele, nimerudi nyuma, nimesikitishwa na namna ambavyo tunapewa empty promises. Mnafahamu population ya wanawake Tanzania ni kubwa, lakini kwenye elimu mmetuambia ni bure, lakini katika uhalisia hiyo elimu bure haina mkakati. Sasa tunapita around the bush kutafuta means and ways ya kui-subsidize hiyo elimu bure katika utaratibu ambao tulikuwa hatujajipanga; lakini bado katika hilo suala la elimu hata nilikopitia, swali langu lilibakia lile lile, where is a woman? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekwenda kwenye afya, nikatamani niwaulize, kwenye bajeti ambayo imekuja mbele yetu kimsingi imekuwa ya jumla na kwa jinsi hiyo inaendelea kuniacha niendelee kuuliza, where is the woman? Afya ya mwanamke, afya ya uzazi kwenye ripoti ya mpango nimeona mnasema vifo vya akina mama eti vimepungua kutoka 450 na kitu kuwa 410, kwa kuvipunguza vifo hivyo kwa idadi tu ya akina mama 30 hivi kutoka kwa akina mama 100,000 wanaojifungua, siyo jambo la kujisifia hata kidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikitika mmelitoa with pride kabisa ndani ya ripoti mnasema vifo vya akina mama wanaojifungua wakati wa uzazi vimepungua; lakini fikiria ni uchungu kiasi gani eti akina mama mia nne na kitu wanakufa kati ya akina mama 100,000 wanaoingia kujifungua, halafu tunataka kusema it is an achievement. It is not! Where is the woman? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtaalam mmoja aliwahi kusema you need a sense of history to know how to handle the future. Kama historia tuliyoibeba katika maisha yetu haijaweza kutuelekeza namna gani future yetu inaweza kwenda, ni dhahiri kabisa kwamba kwa sababu leo niliamua ku-centre hapo niwaeleze ya kwamba akina mama wamelia kwa muda mrefu, wamelia katika labor rooms wakati wakijifungua, wamelia kule jikoni ambako wanapika na kuni mbichi, moshi unawaumiza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanawake wamelia sana wanaposafiri kilometa nyingi kwenda kutafuta maji, wanawaacha watoto wao wadogo nyumbani, wanarudi wanakuta wameunguzana moto wakati wakijaribu kupika uji kwa sababu mama amechukua muda mrefu kwenda kutafuta maji; akina mama wamelia sana wanapolima mazao yao halafu yanakosa masoko; yakipata masoko yanapata masoko ya ajabu ajabu, wanakopwa, wanaibiwa na wachuuzi huko vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, akina mama wamelia sana vijana wao walipomaliza shule wakakosa ajira ya uhakika, wakarudi mitaani wakawa vibaka, wamechomwa moto kwa sababu Serikali haijaandaa mpango maalum wa kuwasaidia vijana. Imewaacha akina mama wakilia na kulia. Akina mama wamelia sana wanaume zao walipoondoka vijijini wakawaacha peke yao na watoto, wakaenda mjini kuhangaika kutafuta ajira kwa sababu kilimo hakilipi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnasema 80% ya Watanzania ni wakulima, lakini mmeshindwa kabisa kulitazama suala hilo katika mkakati ambao ni mahsusi. Mimi sitaki kwenda huko, nataka kuwauliza, where is the woman? Bei ya bidhaa inapopanda; jana niliongea na mama yangu ananiambia mwanangu sasa sukari hapa kwetu ni shilingi 2,500, nikamwambia mama vumilia. Eeh, 2020 bei itashuka, hamna matatizo. Akina mama wamelia sana.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba Waziri wa TAMISEMI na Waziri wa Utumishi na Utawala Bora wanisaidie kulia na akina mama hawa kwa sababu maisha yao hata wakienda kujifungua wanakokotwa na mikokoteni ya ng‟ombe, wanapelekwa katika zahanati ambazo hazina huduma za kutosha; wakijifungua watoto wao wanafariki kwa sababu ya upungufu wa huduma; nilimsikia Mheshimiwa Malapo asubuhi anasema zahanati haina maji. Imagine mwanamke anayekwenda labor ward halafu hakuna maji, halafu utamwambia kufariki mtoto wako ni bahati mbaya. Bahati mbaya kwao tu, akina mama tu au na kwa wengine?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekwenda kwenye janga kubwa la madawa ya kulevya, our youths are frustrated. We have a lot of miserable children around the streets na hili lote linatokea kwa sababu mipango ya Serikali haijamtazama mwanamke kama mwanamke. Nataka kuuliza tena katika bajeti zenu na katika mipango yenu, where is the woman?
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtaalam mmoja kutoka Singapore aliwahi pia kusema naomba nirejee, when women thrive, all the society benefits and succeeding generation are given a better start in life. You guys have gone through the same process. Ninyi wote mko na akina mama zenu, mlizaliwa.
Sasa naomba ukiwa Waziri wa Fedha na Mipango, ukiwa Waziri wa TAMISEMI, Afya na kadhalika usifikiri ya kwamba hakuna mama yako, shangazi yako, dada yako kijijini ukafikiri mipango hii tu inaweza kwenda bila kumtazama mwanamke katika jicho lenye uhakika, halafu ukadhani unakwenda kufanikiwa. When women thrive all the society benefits and succeeding generation are given a better start in life. What are we doing to give our succeeding generation a better start in life? Where is the woman? Where is the woman katika haya tunayoyafanya? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakosea sana kama Taifa kuwaacha nyuma wanawake. Viwanda vidogo vidogo ni suala ambalo kwa kweli mnapokwenda kwenye mkakati wa viwanda lingekuwa limewatazama wanawake, ndiyo watu wenye commitment, ndiyo watu ambao wangezalisha malighafi ambazo zingesaidia viwanda vikubwa; lakini mmeyaweka in general. Kwa hiyo, naomba Mawaziri wanaohusika kwenye hili, tukienda kwenye hitimisho mnisaidie. Naomba mjibu hili swali, kwa sababu nobody can ever stay here and say he never recognize a woman in his life or in her life.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuambieni kwamba suala la umeme wa REA, mlipoona ni kazi nyepesi sana kufikiri ya kwamba ni mradi ambao mnatakiwa kubeza baada ya zile fedha za MCC kukatwa, mkadhani ni sawa sawa; akina mama wanapika gizani, akina mama wanaungua na mkaa na moshi. Hilo ndiyo jambo ambalo mngetakiwa kuliweka mbele ili hatimaye mwanamke apate ahueni. Aki-smile, you guys all smile. Make a woman smile. There is no life without a woman in this world man. Tukubaliane hivyo. Where is the woman? (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningetamani sana neno langu liwe sheria halafu niwalazimishe kufanya ninayotaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa sababu naona muda wangu umekwisha, lakini naomba Waheshimiwa Mawaziri wanijibu, where is the woman in your plans?