Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mungu. Pili nimpongeze Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa katika sekta hii.

Vilevile nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hii pamoja na watendaji wote wa Wizara akiwemo Engineer Mlavi kwa ushirikiano mkubwa anaotupa katika Wilaya yetu ya Nyasa.

Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mkurugenzi wa TPA pamoja na timu yake kwa kuanza kuimarisha bandari ya Mbamba Bay, huo ni ukombozi mkubwa sana kwa Taifa na hususan wananchi wa Wilaya ya Nyasa.

Mheshimiwa Spika, katika suala ya uboreshaji huduma bandari ya Dar es Salaam naunga mkono, la msingi masuala ya kimkataba yawekwe vizuri kuangalia flexibility ya revision in case kuna lazima ya kufanya hivyo na pia kuzingatia masuala ya kiusalama.

Mheshimiwa Spika, nashukuru pia kwa hatua zinazoendelea katika kujenga Daraja la Mitomoni. Daraja hilo ni ukombozi mkubwa kwa wananchi wa eneo hilo na wananchi wa Nyasa na Songea, hali kadhalika jirani zetu wa Msumbiji. Kutokuwepo kwa daraja hili ni kikwazo kikubwa kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, naomba bajeti ijayo itengwe fedha ya kufanya upembuzi barabara ya Unyoni hadi Mitomoni kwa ajili ya maandalizi ya kujenga kwa kiwango cha lami. Nakumbusha utekelezaji kwa kiwango cha lami barabara ya Ruanda - Lituhi - Ndumbi na Mbamba Bay - Lituhi.

Mheshimiwa Spika, mwisho kutokana na Wilaya ya Nyasa kupokea maji mengi toka milima ya Livingstone hivyo kuhitaji fedha nyingi za matengenezo ya dharura. Ni vema bajeti ya matengenezo iongezwe.