Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Wizara hii ya Uchukuzi.

Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa kutoa fedha nyingi sana za kujenga barabara na madaraja katika mkoa wetu. Kwa kweli naipongeza Serikali kwa ujenzi mkubwa wa madaraja likiwemo la Tanzanite, Kurasini, TAZARA Mfugale na Inter Change ya Kijazi, kwa kweli madaraja hayo yamebadilisha sura ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Aidha, napongeza kwa ujenzi wa barabara za mwendokasi Mbagala na Gongo la Mboto; naishukuru sana na kuipongeza Serikali.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu; naomba mradi wa DMDP uje katika Mkoa Dar es Salaam kutusaidia katika barabara za mitaa na naomba ujenzi wa barabara uende sambamba na taa za barabarani kwa kuwa barabara zetu zimekuwa na giza sana.

Kuhusu bandari ya Dar es Salaam, kwa kweli utendaji wa bandari ni wa kusuasua kwa muda mrefu na hasa eneo la operation, Wakurugenzi wa Bandari wamekuwa wakipata tuhuma mbalimbali kutokana na mifumo yetu kutosomana. Sasa naiomba Serikali tuangalie upande mwingine wa shilingi kufikiria kumuweka mwekezaji wa kuendesha bandari upande wa operation. Mwekezaji aendeshe bandari na kuboresha miundombinu, na sisi atupe faida yetu, cha msingi ni kuangalia mkataba uwe win win na maslahi ya wafanyakazi wetu yazingatiwe kulingana na mkataba wao wa kazi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na nakupongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na watendaji wote wa Serikali bila kusahau Wakurugenzi wa Taasisi zetu zote zilizo chini ya Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, ushauri wangu naomba uzingatiwe.