Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Nami naomba kwanza nitoe shukurani za dhati kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa Hotuba yake nzuri ambayo ime-reflect Mpango wa Serikali wa Miaka Mitano; lakini vile vile imejikita katika Hotuba ya Mheshimiwa Rais aliyoitoa Novemba, wakati anazindua Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwanza na kumpongeza sana Waziri wa Nishati Profesa Sospeter Muhongo, kwa kupigana na kuwezesha Serikali yetu kupata mradi ule wa bomba la mafuta kutoka Ziwa Albert kule Uganda hadi katika Bandari ya Tanga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ile ni fursa nzuri kwa sisi Watanzania kuitumia kama comparative geographical advantage kwamba isiishie tu kwenye kusafirisha mafuta ghafi; lakini iendane sambamba na upanuzi wa Bandari ya Tanga ili iweze kuwa hub ya mizigo ya nchi ya Uganda na pia ushirikiano na wenzetu wa Sudani ya Kusini ambao wamejiunga katika Jumuiya Afrika Mashariki. Tukiitumia fursa hiyo vizuri ya kupanua Bandari ya Tanga kuboresha miundombinu ya reli kutoka Tanga, Moshi, Arusha hadi Musoma; pia sambamba na kuboresha Bandari ya Ziwa Victoria katika bandari ya Musoma, itaweza kuleta tija zaidi kwa Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiwa katika bajeti ya TAMISEMI kama ambavyo iko mbele yetu, naomba na mimi nichangie katika maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la kwanza, nitajikita katika eneo la ugatuzi wa madaraka, maana dhana nzima ya ugatuzi ni kuweza kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi, lakini ninavyozungumza hapa mimi ni Mbunge wa tatu wa Jimbo la Mlalo, tunayo maombi yetu Wizara ya TAMISEMI ya kutaka tupate Halmashauri ya Mlalo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Mlalo linaundwa na tarafa tatu, kata 18, vijiji 78, vitongoji 599, sekondari 29, shule za msingi 93. Tunao mwingiliano wa mabasi ya kwenda Arusha, Dar es Salaam na kadhalika. Tunayo magulio makubwa ambayo yanaweza yakaleta watu wengine kutoka Zanzibar, Comoro na Mheshimiwa Ally Salehe pale Mbunge wa Malindi; naye alitoa mchango wake kushuhudia katika hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ombi letu sisi ni kuweza kupata Halmashauri, ili tuweze kuhudumia wananchi kwa ukaribu. Tunavyo vituo vya afya vya kutosha zaidi ya vinne, na viwili tayari vinafanya shughuli ya upasuaji, kwa hiyo, ni imani yangu kwamba Wizara husika italichukua hili na italifanyia kazi kadri inavyowezekana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sikupata fursa ya kuchangia kwenye bajeti ya Waziri Mkuu, kulikuwa na suala zima la Baraza la Uwezeshaji la Taifa. Kama ambavyo Hotuba ilivyotoka Baraza hili ndilo litakalohusika na dhana nzima ya hizi shilingi milioni 50 kwa kila kijiji na kwa kila mtaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu ni kwamba, ahadi ya milioni 50 imetokana na zao la kisiasa, kwamba ni utekelezaji wa Ilani ya Chama lakini kwa kuwa tuna uzoefu na mamilioni ya JK; kwamba hayakuwafikia walengwa waliokusudiwa, nitoe rai kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu na Baraza zima hili wa Uwezeshaji kwamba pesa hizi zipitie kwenye mabenki. Mabenki ambayo yana network mpaka kwenye vijiji hata kama ni microfinance pesa hizi zitengenezewe utaratibu tusije tukajidanganya tukazipeleka kwa Makatibu wa Vijiji, ama zikaishia kwenye halmashauri halafu wao ndio wazipeleke huko; tunaweza tukakumbana na kadhia kama ambayo tumekutana nayo katika mamilioni ya JK.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo nataka kuchangia ni suala zima la mazao ya kilimo. Serikali ya Awamu ya Tano imejipambanua wazi kwamba tunataka kwenda kwenye uchumi wa kati wa viwanda, ni jambo zuri. Yako mazao ambayo hayapo katika utaratibu huo wa kuwa kwenye viwanda vikubwa; mfano mazao yanayotokana na mbogamboga. Mazao haya kwa halmashauri ya Wilaya ya Lushoto ni kama viazi, kabichi, karoti, nyanya, vitunguu na kadhalika. Mazao haya huwa wanatumia mfumo wa lumbesa kuyapeleka masokoni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo huu ulikuwa ni wa unyonyaji sana kwa wakulima. Kwa hiyo, mwisho wa siku mkulima hawezi kupata tija kwenye mazao ambayo anatumia muda mrefu kuyazalisha. Niiombe Serikali kupitia halmashauri waweke utaratibu mzuri wa kuzibana halmashauri zote ziweze kudhibiti huu ufungaji wa mazao kupitia lumbesa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu huu utawasaidia hao wananchi ambao hawawezi kwenda kwenye uchumi wa viwanda; waweze kupata mazao yao katika ubora mzuri wa kupata tija ya faida ya mazao ambayo wanayazalisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la uwezeshaji wa wananchi kupitia miundombinu ya masoko. Huko vijijini masoko bado ni tatizo kama ambavyo nimetangulia kusema kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto inapokea wageni kutoka maeneo mbalimbali kutoka Zanzibar na Comoro, lakini bado hatuna miundombinu mizuri ya masoko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwa Baraza la Uwezeshaji la Taifa kwamba watujengee masoko na kwa kupatikana masoko; inaweza ikawa ni tiba mojawapo ya kupunguza haya matatizo ya lumbesa kwa sababu naamini wakulima watakuwa wanauza mazao yao katika masoko yaliyoko karibu na maeneo yao, hawatakuwa na haja ya kuwauzia wachuuzi ambao huwa ndiyo wanapeleka katika mtindo wa lumbesa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la utawala bora; nimefarijika kuona katika Hotuba ya Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora wamezungumzia suala zima la uanzishaji wa Idara ya Mikataba na Utendaji Kazi Serikalini. Jambo hili ni jema, tunaomba lifanyiwe kazi na utaratibu uanze mara moja ili mwisho wa mwaka waweze kupima tija ya wafanyakazi wa umma pamoja na wafanyakazi katika idara mbalimbali za Serikali. Hii itazidi kuongeza uwazi na uwajibikaji miongoni mwa Taasisi na Idara za Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni suala la chaguzi zetu ambazo tumekuwa tunaendelea kuzifanya. Lazima tukumbuke kwamba chaguzi hizi zinafanywa kwa mujibu wa sheria, lakini pia zipo tume ambazo zinasimamia, ni vizuri sana tusilitumie Bunge kama sehemu ambayo kila siku tunaongelea jambo ambalo limekuwa linatolewa ufafanuzi mara kwa mara. Tunapozungumza dhana zima ya utawala bora pamoja na utumbuaji wa majipu tusijaribu kuegemea upande mmoja hata kwenye vyama vyetu ni lazima tuhakikishe kwamba dhana nzima ya utawala bora pia inapatikana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mfano ambao nisingependa sana kuutumia kwa jinsi ambavyo namuheshimu kaka yangu Mheshimiwa Zitto Kabwe, lakini naomba tu niutumie, kwamba hata yeye alipokuwa na kesi na chama „X‟ siku ambayo hukumu imesomwa basi wamemtangazia pale pale mahakamani kwamba kuanzia wakati ule sio mwanachama wa chama kile, hawajampa hata muda wa kufanya hiyo natural justice. Sasa haiwezi ikawa akijisaidia kuku ndiyo kajisaidia, lakini akijisaidia bata basi inakuwa ni matatizo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Ezekiel Wenje Mbunge wa Nyamagana kwenye Bunge lililopita, alizungumza sana kuhusu suala la Mheshimiwa Kabwe ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, sasa leo anatumbuliwa hadharani bado watu tunahoji kwa nini huyu mtu hapewi haki ya kusikilizwa. Niwaombe tunaposema upinzani, tunataka kwamba tuwe na Serikali mbadala na naamini kwamba upinzani wa kweli umeondoka na Mheshimiwa Zitto Kabwe na Mheshimiwa Dkt. Willbroad Slaa, uliobaki Bungeni sasa hivi ni upingaji sio upinzani, tumeona kete moja ya ACT Wazalendo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja.