Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kupata na fursa ya kuweza kuchangia katika Wizara hii ya Ujenzi na Uchukuzi. Wizara hii kwangu kama Mbunge wa Jimbo la Kigamboni ni Wizara ambayo inagusa maisha ya kila siku ya wananchi wa Kigamboni. Kwa sababu hiyo nitajielekeza katika hoja tatu ambazo zinagusa Jimbo langu la Kigamboni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza ni suala la Daraja la Nyerere. Daraja hili limejengwa kwa ubia kati ya Serikali na Shirika la NSSF. Daraja hili ni la kulipia; hoja ya wananchi wa Kigamboni bado iko palepale. Wananchi wa Kigamboni ni walipa kodi wa nchi hii. Wananchi wa Kigamboni michango yao na kodi zao zinachangia katika ujenzi wa madaraja mengine nchini lakini wananchi wa Kigamboni ni wananchi pekee katika nchi yetu ambao wao pekee wanachangia katika kuingia na kutoka Kigamboni. Kwa hiyo wananchi wa Kigamboni wamenituma kuja kusisitiza hoja yao ya kutaka daraja lile liondolewe ile tozo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Waziri, tulifanya mapunguzo ya tozo lakini bado wananchi wa Kigamboni wanasisitiza kwamba tozo ile iondolewe ili wapate ahueni ya maisha. Gharama za maisha kwa wananchi wa Kigamboni kwa kweli ni kubwa sana, hususan katika bidhaa zote zinazoingia Kigamboni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili ambalo nilikuwa nataka kuchangia ni suala la vivuko. Kivuko cha Kigamboni kinapitisha takribani watu 50,000 mpaka 60,000 kila siku na magari takribani 2,000 kila siku. Ni watu wengi sana. Lakini kumekuwa na changamoto nyingi sana katika kivuko kile. Kwanza, sehemu ya kusubiria abiria ni ndogo sana, hususan katika kipindi cha asubuhi na jioni. Lakini mifumo ya ulipaji fedha, kwa maana ya N-card nayo imekuwa na changamoto ya mifumo kuwa down, jambo ambalo linapelekea wananchi kupata usumbufu muda mrefu. Vile vile njia za kuingilia na kutokea katika kivuko hususani kwa upande wa Kigamboni na upande wa Magogoni nazo zimekuwa ni finyu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona katia taarifa ya bajeti hii kwamba mmetenga milioni 300 kwa ajili ya kulipa fidia, fedha hizi ni ndogo sana. Mwende mkaangalie jinsi gani ya kuweza kufanya. Lengo letu na kusudio letu mfanye kama ilivyofanyika pale kwenye Daraja la Nyerere, kuwe na njia saba za kuingilia na njia saba za kuweza kutokea na hii itasaidia sana. Muangalie vile vile jinsi gani ya kuweza kufanya kuhakikisha kwamba tunakuwa nae neo la ku–park. Si kila mtu anataka kuvuka na gari. Nilikuwa natamani kuona kwamba kuna sehemu ya parking ambayo mtu anaweza aka–park gari yake akavuka akaenda mjini kwa sababu kuna watu wengine wanaofanya kazi pale maeneo ya Kivukoni haitaji kuvuka na gari Kwenda mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo ukishatoka kwenye kivuko upande wa kushoto ni eneo la bandari, hii ni Taasisi mama na sisi dada na TEMESA. Mimi nadhani suala hili liko ndani ya Wizara yenu, naomba mkae muangalie jinsi gani ya kufanya mawasiliano ili eneo ambalo halitumiki kwa upande wa bandari baada ya kuvuka upande wa kigamboni basi liweze kutumika katika sehemu ya park and go.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nataka nitoe ushauri kwa Mheshimiwa Waziri, TEMESA ni Taasisi ambayo inasimamia masuala ya ufundi umeme na masuala ya vivuko. Mimi ushauri wangu, tuwekeze katika Nyanja ambazo tunaona zinakwenda kuwa na tija. Sasa hivi TEMESA Imejitawanya sana katika masuala ya mechanical, masuala ya electrical pamoja na masuala ya vivuko. Tukiweza kuijengea uwezo vizuri TEMESA katika masuala ya ufundi wakaweza kufanya matengenezo ya magari yote nchini, kwa maana ya magari ya Serikali, jukumu hilo peke yake linawatosha sana. Lakini vilevile wakatoa ushauri katika masuala ya umeme tukawanunulia vifaa, tukawapatia nyenzo za kuweza kufanya kazi. Majukumu haya yanatosha sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado mimi kama Mbunge nitaendelea kusimama na kusema kwamba suala la vivuko liondolewe TEMESA. Wapeni watu wenye uwezo waende wakaifanye hiyo kazi. Wananchi wa Kigamboni wanahitaji usafiri wa uhakika ili wasafiri salama. Sasa hivi kutoka Kigamboni sehemu ambayo straight haifiki hata kilomita moja watu wanasubiria Zaidi ya saa moja. Tunataka ifike mahali ambapo mwananchi akifika pale dakika tano yuko upande wa pili wa mjini. Kwa hiyo nitaendelea kusisitiza kwamba huduma za vivuko zibinafsishwe. TEMESA ibaki na majukumu ya msingi ya huduma za umeme na ufundi na hao mkiwawezesha vizuri wataweza kufanya vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la tatu ambalo nilikuwa nataka nilisemee ni suala la miundombinu ya barabara. Katika wilaya za Mkoa wa Dar es Salaam Wilaya ya Kiagamboni ndiyo wilaya pekee katika Mkoa wa Dare es Salaam ambayo iko nyuma sana katika miundombinu ya barabara. Katika miundombinu ya barabara za TANROADS tuna asilimia 37 tu; na zaidi ya asilimia 50 ya barabara zote za TANROADS katika Mkoa wa Dar es Salaam ambazo hazijawekwa lami ziko katika Wilaya yetu ya Kigamboni. Tumechelewa sana na tuko nyuma sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kigamboni ni Wilaya ambayo inakuwa kwa kasi kubwa mno. Sasa hivi uwekezaji wa viwanda ni mkubwa, kasi ya ujenzi ni kubwa, na Kigamboni ndilo eneo pekee ambalo sasa hivi vinapatikana viwanja vingi sana, na hata nikiangalia hapa ndani ya Bunge lako la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nina Wabunge nadhani theluthi moja kama si zaidi ni wakazi wa Kigamboni. Wamejenga au wana nyumba kule Kigamboni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi niombe sana Wizara ya Ujenzi iweke msukumo katika miundombinu ya barabara. Sasa hivi barabara ya kutoka Gomvu Kwenda Pembamnazi tulikuwa tumeijenga kwa kilomita moja moja ni ndogo sana. Kumekuwa na ujenzi mkubwa wa viwanda katika maeneo ya Kimbinji na tumetenga eneo la uwekezaji kule Pembamnazi, na hata Wizara ya ardhi imepima viwanja kule lakini watu wanashindwa kujenga kwa sababu hakuna miundombinu ya kuweza kufika kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, Barabara ya Kibada – Mwasonga kueleke Kimbiji na Tundusongani, hili nisipolisema kwa kweli wananchi wa Kigamboni hawatanielewa. Barabara hii tuliipitisha katika bajeti ya mwaka jana, katika barabara chache ambazo Serikali iliridhia na tukaipitisha kwenye bajeti. Lakini nitoe malalamiko yangu makubwa sana, kwamba mchakato wa barabara hii umekwenda taratibu sana. Ni jana tu Mheshimiwa Waziri ndipo amekuja kunithibitishia, jana, kwamba tenda imefunguliwa juzi, Mkandarsi amepatikana. Na mimi nimemwambia Mheshimiwa Waziri jana, kwamba mchakato utakapokamilika aje yeye mwenyewe Kigamboni kutia saini ule mkataba na kuwaambia wananchi wa Kigamboni ujenzi unaanza lini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka umeniambia kwamba mkandarasi amepatikana, na tunategemea ndani ya mwezi mmoja ujenzi wa barabara mkandarasi wa barabara ya Kibada Kwenda Mwasonga atakuwa amepatikana. Nikutake Mheshimiwa Waziri uje wewe mwenyewe Kigamboni katika sherehe ya utiaji saini ya ile barabara ili na wewe useme na wananchi wa Kigamboni. Nimechoka kuwasemea kwa niaba yako, mchakato umekuwa ni mrefu sana, barabara hii tulipitisha kwenye bajeti ya mwaka jana, na sasa hivi imebakia mwezi mmoja kabla ya mwaka wa fedha kuisha. Kwa hiyo nikuombe sana, kabla ya mwaka huu wa fedha kwisha uje Kigamboni utie saini hii barabara. Umenithibitishia wewe mwenyewe kwamba mkandarasi ameshapatikana kwa hiyo ndani ya mwezi mmoja kamilisha hizo taratibu za mikataba ili uweze kuja kuwatangazia wananchi wa Kigamboni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimuombe vilevile Mheshimiwa Waziri kuhakikisha kwamba hizi barabara nyingine especially ya Gomvu, Kimbiji mpaka Kwenda Pembamnazi nayo tunaiongezea wigo kuhakikisha kwamba nayo inafika Pembamnazi kwa sababu hili ni eneo la kimkakati na ni eneo la uwekezaji. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri wakati unapokuja kuhitimisha mimi nitaomba nipate commitment yako katika maeneo haya yote ambayo nimeweza kuyataja ili wananchi wa Kigamboni waweze kusikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana sana.