Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia makadirio ya Ofisi ya TAMISEMI na Utawala Bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu, nitumie nafasi hii nimshukuru sana Mungu ameniwezesha kuingia kwenye nyumba hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nikupongeze sana wewe mwenyewe kuchaguliwa kuwa kiongozi wetu. Niseme najivunia kuwa Mbunge wa Jimbo la Ushetu na najivunia pia kuwa na Madiwani wote wa Chama cha Mapinduzi. Nilikuwa napata shida kidogo na maswali, watu wengine hawajui Jimbo la Ushetu liko wapi, Jimbo la Ushetu limetokana na lile Jimbo la Kahama. (Makofi/Vigelegele)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayoifanya. Mheshimiwa Rais ametupa Baraza zuri la Mawaziri, Mawaziri ambao wanatusikiliza na naamini kwamba watafanya kazi vizuri kwa maendeleo ya wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Chama cha Mapinduzi kimetupa ilani nzuri sana. Niwaombe tu Waheshimiwa Wabunge ambao labda hawajaipitia vizuri waisome, ni msingi mzuri wa kwenda kwenye maendeleo na kasi ambayo tunaihitaji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sikupata nafasi ya kuchangia kwenye Mpango wa Pili wa Maendeleo lakini nitumie nafasi hii niseme kwa ufupi kabisa kwamba nilisoma Mpango wa Maendeleo umezingatia sana Ilani ya Chama cha Mapinduzi lakini pia umeangalia sana kwenye ule MKUKUTA. Kwa hiyo, niipongeze sana Serikali kwa kutazama kwa umakini na uhakika Mpango huu kwa madhumuni ya kuwaletea maendeleo wananchi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumze kwa ujumla juu ya Halmashauri zetu. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri Simbachawene kwa kazi ambayo anaifanya. Nina uhakika kwenye mpango huu aliouleta utakapokwenda kufanyika kuna mambo mengi ambayo tutakwenda kufaidika nayo sisi wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie kwanza suala la kuzisaidia Halmashauri zetu kuhusu watumishi. Rasilimali watu ni muhimu sana kwa sababu ndio rasilimali ambayo itakwenda kusimamia rasilimali zingine, itakwenda kusimamia rasilimali fedha na mambo mengine ya kiutekelezaji. Kwa sababu ukija kuangalia, TAMISEMI ndiyo Wizara ambayo inakwenda kusimamia mambo mengi ambayo pia yatakuwa yameonekana kwenye Wizara zingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka nishauri tu kwamba, Serikali itazame eneo hili la watumishi pamoja na namna ambavyo inachukua hatua mbalimbali za kuweza kuhakikisha kwamba watumishi wa umma wanakuwa na nidhamu lakini lazima tupeleke msukumo mkubwa kuhakikisha kwamba tunawapa weledi wa kutosha watumishi wetu, tunakuwa na idadi ya kutosha lakini pia tuangalie kama tunaweza kuwapa motisha ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi ili kuendana na kasi hii ya Rais wetu ya kuchapa kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka nizungumzie juu ya mapato, uko umuhimu wa kutazama sana katika hizi Halmashauri zetu. Nilikuwa nikiangalia kwenye majedwali ya namna ambavyo fedha zimekuwa zikienda kwenye Halmashauri zetu lakini pia nimeangalia na ongezeko la makusanyo, ningependa nimshauri Mheshimiwa Waziri tuweze kuongeza ruzuku kwenye Halmashauri zetu. Kwa sababu ukisoma kwenye mtiririko wa fedha inaonekana kwamba ruzuku zimekuwa zikishuka.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia kwa hesabu kuanzia za mwaka 2013/2014, Halmashauri zimekuwa zimetengewa shilingi bilioni 704, mwaka uliofuata 2014/2015 zilitengewa shilingi bilioni 563 na mwaka wa fedha uliofuata Mkuu ya mwaka wa fedha 2011/2012, kati ya wilaya ambazo zilikuwa zimekuwa proposed kuanzishwa ni Wilaya ya Ushetu lakini haikuanzishwa kwa sababu hatukuwa na halmashauri. Sasa tunayo halmashauri ambayo ilianzishwa mwaka 2012 na sasa tunalo jimbo na ili tuendane na maendeleo ambayo tunahitaji, tunahitaji kwa kweli tupate wilaya. Yako mambo mengi ambayo yanatupita kutokana na ile dhana tunapokuwa tunayapeleka maendeleo tunayapeleka kwenye Makao Makuu ya Wilaya tunasahau kwenda kwenye halmashauri ambazo haziko kwenye Makao Makuu ya Wilaya ambako ndipo watu wengi walipo. kwa hiyo, nafikiri hili linaweza kuwa ni changamoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mtizamo uwe kuangalia huduma zinaenda kwa wananchi walio wengi ambao wako nje ya makao Makuu ya Wilaya. Kwa hiyo, napenda niombe sana Mheshimiwa Waziri aliangalie hili kwa sababu ni muda mrefu tumechelewa kupewa Wilaya kwa sababu ya kutokuwa na Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo mengine ya huduma ambayo kwa sehemu kubwa kama nilivyozungumza Serikali zetu za Mitaa ndiyo zinasimamia pamoja na kuwa yanasimamiwa na Wizara zinahusika lakini ile manpower kubwa iko katika halmashauri zetu. Nikianza na eneo la afya tupate fedha za kujenga Hospitali ya Wilaya ya Ushetu.
Mheshimiwa Naibu, ahsante, naunga mkono hoja.