Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Nianze kwanza kuishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri wanayoifanya kwa kuweza kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi na wananchi wanaipokea kwa asilimia mia moja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naishukuru Wizara ya TAMISEMI kwa kazi kubwa na kwa muda mfupi walioifanya na kuonesha kwa wananchi kwa kuchukua hatua kwa wale wanaofuja fedha za Serikali. Naiomba Wizara hii ijaribu kuangalia maeneo mapya hususan Wilaya ya Itilima, ni Jimbo jipya na Wilaya mpya, takribani miaka 20 liko upinzani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli, wananchi hawa wameweza kufanya kazi kubwa ya kutekeleza Sera za Serikali ya Awamu ya Tano. Serikali ya Awamu ya Tano inasema kila kijiji kuwe na zahanati. Tunavyozungumza hivi, tunazo Zahanati 29 na zahanati nane ziko katika hatua za mwisho. Naiomba Wizara iweze kuleta fedha za kumalizia hizo zahanati ziweze kufanya kazi, ukizingatia Wilaya yetu ya Itilima ni Wilaya ambayo haina Hospitali ya Wilaya. Tunategemea sana hizo zahanati zitapunguza kasi katika maeneo ya Maswa pamoja na Wilaya ya Bariadi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kuipongeza tu Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi kubwa inayoifanya, vilevile na Waziri Mkuu kwa kazi kubwa anayoifanya pamoja na wasaidizi wake. Nataka niwaambieni ndugu zangu, Awamu ya Tano imewagusa Watanzania wote na haya tunayoyazungumza na wao wanasikia. Kwa kweli, kazi inayofanywa, kila mtu anaiona na anaitazama. Ni sehemu pekee kwa muda mfupi wameweza kutekeleza majukumu makubwa na ya msingi kwa kuleta mabadiliko makubwa katika awamu hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukizungumzia suala la madawati, Awamu ya Tano imezungumza kwa mapana sana. Tunaozunguka vijijini unakuta shule moja ina wanafunzi 939, ina madawati 36! Unategemea pale tunatengeneza Taifa la aina gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini baada ya Awamu ya Tano kugundua na kutoa maelekezo, bado wenzetu wanaendelea kulalamika, lakini hoja ni nzuri ni kuhakikisha Watanzania, watoto wetu, wanapata maisha bora na elimu iliyo bora. Vilevile itapunguza gharama kwa wazazi wetu kununua mashati pamoja na sketi kwa ajili ya watoto wetu watakapokuwa na madawati bora, natarajia na elimu itakuwa nzuri zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe ushauri, kwenye 50%, kwenye suala la shilingi milioni 50 kwa kila kijiji. Wengi wamesema, lakini ikumbukwe, lazima tujenge uwezo katika maeneo yetu ya vijiji. Shilingi milioni 50 tutakapozipeleka bila kuwa na elimu ya kutosha, zile fedha zitapotea na hazitaleta impact yoyote katika maeneo husika. Taasisi moja ipo katika maeneo ya Halmashauri inaitwa Idara ya Maendeleo ya Jamii; wale watu wangefanya kazi ya kutoa elimu kwa wananchi kabla fedha zile hazijafika waweze kujua jinsi ya kuzitumia, kuliko kumpelekea mtu lundo la shilingi milioni 50 katika kijiji kimoja, halafu zile fedha zitapotea na hazitakuwa na hadhi yoyote katika maeneo husika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukifanya hivyo, zile fedha ni nyingi zinaweza zikasaidia na zikatoa umaskini katika maeneo husika. Maeneo yako katika tabaka mbalimbali. Maeneo mengine kuna Vyama vya Ushirika, kuna ma-godown, maeneo mengine wanalima korosho, pamba na kadhalika. Ile fedha ikitolewa na Tume ya Ushirika ikiboreshwa vizuri, ni imani yangu ile fedha inaweza ikawa mtaji mkubwa katika vijiji husika na ikaleta maendeleo makubwa sana kama wenzangu walivyochangia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya machache, nashukuru sana, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja ili Watanzania waweze kufaidika na hii Awamu ya Tano. Ahsante sana.