Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuchangia. Nianze kwa kumshukuru Mwenyenzi Mungu kwa kutufanya tuweze kuwa salama na tuweze kushiriki kikao hiki cha siku ya leo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kuwapongeza Mawaziri na nawapongeza kwa jambo moja la msingi. Zamani kabla sijaingia Bungeni nilikuwa nasikia kwamba kumfikia Waziri ni kazi ngumu kweli, lakini Mawaziri wa Serikali ya Awamu ya Tano naona ni Mawaziri reachable, ni rahisi kuwafikia. Binafsi niwashukuru kwa dhati kabisa Waziri Mheshimiwa Simbachawene na Naibu wake Mheshimiwa Jafo kwa sababu yanayohusu Halmashauri yangu ya Mji wa Nzega wamekuwa wakitoa ushirikiano hata yale ambayo hajakamilika lakini angalau unakuwa una moyo kwamba kesho litakamilika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na jambo la kwanza. Halmashauri ya Mji wa Nzega ni mpya, lakini kwa muda mrefu kwa lugha ambayo nimeisikia Serikalini inalelewa na Halmashauri ya Wilaya ya Nzega. Kwa maana kwamba bajeti ceiling zake zinakuwa zikipitia Halmashauri ya Wilaya ya Nzega. Mheshimiwa Waziri anafahamu matatizo yanayoikabili Halmashauri ya Mji wa Nzega, fedha za OC mnazopeleka Halmashauri ya Mji wa Nzega zinazopitia Nzega DC hazifiki katika Halmashauri ya Mji wa Nzega. Inakuwa ni unfair kwa watendaji walioko pale, Serikali Kuu ina disburse fedha kwenda kwenye Halmashauri ya Mji wa Nzega kupita Halmashauri ya Nzega DC kwa sababu tu ceiling na vote ya Halmashauri ya Mji wa Nzega ilikuwa chini ya Halmshauri ya Wilaya ya Nzega. Mpaka leo fedha mlizotuma kwenda Halmashauri ya Mji wa Nzega 56 million shillings ambazo ni za OC zimetumika katika Halmashauri ya Wilaya na Halmashauri ya Mji haijapata zile fedha, ni tatizo kweli.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Halmashauri ya Mji wa Nzega ipewe vote yake, ijitegemee, ina wafanya kazi wake, ina vyanzo vyake vya mapato, ina kila kitu, for how long Halmashauri ya Mji huu itakuwa chini ya Halmshauri ya Wilaya ya Nzega, ni mateso. Leo hii fedha za Mfuko wa Jimbo la Nzega Mjini tunashindwa kuzipata na hili siyo suala la Wabunge ni la watendaji walioko pale hawako flexible kutumia taratibu zilizowekwa ili fedha zile ziwe disbursed kwenda kwenye Halmshauri ya Mji wa Nzega, hili ni ni tatizo. Nakuomba Mheshimiwa Simbachawene, Halmashauri ya Mji wa Nzega muiondoe kwenye kwapa la Halmashauri ya Wilaya ya Nzega. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo vyanzo vya mapato vya Halmashauri ya Mji wa Nzega vinakusanywa na Halmashauri ya Wilaya kwa hoja kwamba fedha hizi zitahamishiwa katika Halmashauri ya Mji lakini hawahamishi. Kwa hiyo, ningeomba hili jambo litatuliwe kabisa katika Mji wa Nzega. Hilo ni jambo la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, nimeona hapa katika jedwali lililoambatanishwa, Halmashauri ya Mji wa Nzega imetegewa shilingi milioni saba kwa ajili ya kilimo, Halmashauri ya Mji wa Nzega ina kata 10, kata nane zote ni za wakulima na ndiyo zinalisha ule mji lakini tume-allocate only seven million shillings. Bajeti iliyokuwa proposed na Halmashauri ya Mji ambayo tuliomba for development ni 176 million shillings lakini tunapata shilingi milioni saba. Kwa hiyo, naomba mnapo-allocate fedha hizi mnazoweka kwenye majiji makubwa kama Mwanza, Arusha na kwingine kwamba ni ya kilimo hawalimi, hizi fedha pelekeni kwenye maeneo yenye kilimo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mfano katika Mji wa Nzega tuna eneo kubwa la kilimo katika Kata ya Mwanzori, kumekuwepo na irrigation scheme toka miaka ya 1970. Kwa sababu tu hakuna allocation ya resources, sasa hivi ile irrigation scheme katika Kijiji cha Idudumo inakufa. Namuomba Mheshimiwa Waziri waliangalie suala hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukiitazama allocation ya funds kwenye kilimo kwa Wilaya zote za Mkoa wa Tabora imetengwa 198 million shillings. Mkoa wa Tabora unalima tumbaku na kwa mwaka jana tumbaku ime-contribute over three hundred million US dollars kwenye pato la Taifa, tunawapelekea shilingi milioni 180. Ukiangalia fedha zilizokuwa allocated kwenye Wizara ya Kilimo na zenyewe ni masikitiko. Najua kasungura kadogo wekeni priority sehemu ya kuzi-allocate.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais alipofika katika Mji wa Nzega wakati anaomba kura tarehe 14 Oktoba, 2015 aliahidi mambo makubwa mawili. Jambo la kwanza katika Mji wa Nzega tuna tatizo sugu la maji, tukamuomba Mheshimiwa Rais kwamba kutatua tatizo la maji katika Mji wa Nzega wakati tunasubiri mradi wa maji wa Ziwa Victoria, kwanza nimwambie Mheshimiwa Waziri wa Maji akija hapa atuambie ni lini mradi wa Ziwa Victoria utaanza kwa ajili ya Mkoa wa Tabora. Wasiposema specifically ni tarehe ngapi mkandarasi anaingia pale mimi nitakuwa mmoja kati ya Mbunge wa Chama cha Mapinduzi ambaye hataunga mkono bajeti ya Serikali kwa sababu mradi huu umejadiliwa mwaka 2013, 2014 na 2015.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais, wakati anajadili suala la maji alitupa shorten solution, katika Mji wa Nzega tunahitaji pampu na matenki matano, ukitazama allocation ya maji iliyowekwa ni shilingi milioni nane. Nikiangalia fedha zilizokuwa allocated Wizara ya Maji hazitatui kabisa tatizo la maji la muda mfupi Nzega. Leo tunatarajia maji kutoka Bwawa la Kilimi, chujio liko Bwawa la Uchama, kwa hiyo vijiji vyote vinavyotoka Kilimi mpaka Uchama ambako tunaenda kusafishia maji hawapati maji. Naiomba Serikali kwa heshima kabisa tunapo-allocate hivi vitu kidogo kidogo hatutatui tatizo. Ni lazima tulitatue tatizo kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ningeomba ahadi ya Rais ya kufunga pampu ya maji katika Bwawa la Kilimi na kujenga matenki matano katika Mji wa Nzega ili kutatua tatizo la maji wakati tunasubiri utekelezaji wa mradi wa maji wa Ziwa Victoria itekelezwe na tuone commitment ya Serikali katika jambo hili. For good news, nimwambie Waziri wa Maji yupo hapa kwamba kwa kuwa Rais alisema mkandarasi atakaa pale Nzega kwa sababu ni njia panda kupeleka maji Singida na Tabora, sisi Halmashauri ya Mji wa Nzega tumetenga eneo ambalo Serikali haitataka fidia yoyote hata shilingi kwa ajili ya kuja kumkaribisha huyo mkandarasi ili aweze kukaa pale na kufanya huu mradi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilimsikia Mbunge mwenzangu mmoja hapa anaongea simkumbuki nadhani ni Mheshimiwa Sannda, namuomba Mheshimiwa Naibu Waziri Jafo na Waziri Mheshimiwa Simbachawene, leo tunaenda kuwaambia wananchi wachangie madawati, wachangie ujenzi wa maabara, Nzega zimeliwa 2.2 billion shillings zilizotolewa na Mgodi wa Resolute ambazo zilikuwa allocated kwa ajili ya ujenzi wa maabara.
Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla aliandamana, alipigwa mabomu, aliwekwa jela ndiyo akapata hako kasungura ka shilingi bilioni 2.2 kalivyoenda Halmashauri waliopiga deal mwingine mme-promote ndiyo kawa Injinia wa Manispaa ya Kagera. Huyu mtu aliharibu Ilala, akahamishiwa Nzega and Nzega is a dumping place kwenye local government, zikaja 2.2 billion shillings akapiga yeye na wenzake maabara zilizokuwa allocated 68 million shillings hazijafika hata kwenye lenta, akahamishiwa kuwa Injinia wa Manispaa ya Kagera, yupo pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Mji wa Nzega, tena Mheshimiwa Waziri Mkuu nisikilize, aliyekuwa Mweka Hazina wa Halmashauri ya Sumbawanga ana kesi ya uhujumu uchumi akapelekwa Magu, akapata kesi ya uhujumu uchumi, leo kahamishiwa Nzega. Leo tumemkamata yeye na network yake wakiiba fedha za parking, wenzake wamewekwa ndani yeye anazunguka pale, this is unfair. Halafu tunaenda kwa wananchi kuwaambia watuchangie fedha za maabara, mimi nimewaambia wananchi wangu wa Mji wa Nzega hakuna kuchanga fedha ya maabara mpaka wezi wapelekwe mahakamani tutafunika maabara zilizobaki. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, kwa masikitiko kabisa, dhamira ya Rais kumpatia kila mtoto wa nchi hii elimu bora ni dhamira njema, tuione kwenye commitment ya Serikali katika allocational of resources, tumefanya mass expansion ya elimu. Hata ukisoma Mpango wa Miaka Mitano, Waziri Mpango anakiri kwenye document yake kwamba quality ya elimu yetu ni tatizo. Niiombe Wizara ya TAMISEMI, kwa sababu kwa sasa hivi dhamana ya ku-expand infrastructure iko mikononi mwenu, jamani tengeni fedha ya kujenga infrastructure ya elimu, tukiuacha huu mzigo kwa wananchi peke yao hawawezi, tuiombe central government. Nishukuru nimepokea madawati 250 nadhani ni chenji ya rada, nashukuru kabisa na nimeyapokea yako pale. Nitumie fursa hii kushukuru institution ambazo zimetusaidia katika Mji wa Nzega, tumepata madawati 600 kutoka TEA…
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, ahsante.