Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuchangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Naomba nianze na mambo haya ili kuweka mambo vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa wale ambao tulibahatika kucheza mpira wa soka, kuna wachezaji wa aina mbili, kuna mchezaji ambaye ana uwezo wa kutumia mguu mmoja tu wa kulia na kuna mchezaji mwingine anatumia miguu yote kulia na kushoto. Kwa wale tunaotazama mpira tunajua siku zote mchezaji anayetumia mguu mmoja tu wa kulia maadui wakishamgundua wakambana wakamfanyia tight making kwenye mguu wa kulia hawezi akacheza mpira uwanjani, sana sana atatolewa nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitendo cha Kamati ya Kanuni kukaba mguu wa kulia wa hotuba ya Kambi ya Upinzani wameshindwa sasa kutumia mguu wa kushoto na ndiyo maana wamejiondoa na kutoendelea kusoma hotuba yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna aina mbili ya wazungumzaji, kuna mzungumzaji mwingine ukishamdhibiti kusema uwongo, ukamdhibiti kutoa lugha ya matusi atajitoa kwenye mazungumzo kwa sababu hana uwezo tena wa kuendelea kuongea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nasikitika sana Mheshimiwa Lema kunizulia mambo ambayo mimi sijawahi kuyasema, hii inatokana na kukabwa mguu wa kulia akashindwa namna ya kuendelea kutumia mguu wa kushoto. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge hili lipo kwa ajili ya Watanzania, kwa ajili ya kutenda haki na ndiyo maana hakuna kiti wala Kamati ya Kanuni iliyozuia Mheshimiwa Lema kutozungumzia jambo la Lugumi, hakuzuiwa ameambiwa arekebishe maneno fulani yeye anasema amezuiwa, hajazuiwa ni kwa sababu anashindwa kuchangia hoja…
MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye ripoti ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama suala la Lugumi limeongelewa kwenye ukurasa wa 12 na ukurasa wa 13 na Kamati hiyo Mwenyekiti huyo hakuzuiwa na ndiyo ripoti tuliyonayo mezani na hapo ndipo ninapozungumzia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niheshimu busara za kiti chako, niende moja kwa moja..
MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa nne wa Hotuba ya Mheshimiwa Waziri amezungumzia majukumu ya msingi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Kwangu mimi majukumu hayo hayawezi yakafanyika kwa ufanisi endapo hatutakuwa na jeshi lenye nidhamu, endapo hatutakuwa na jeshi lenye makazi bora ya askari, endapo hatutakuwa na askari wenye afya bora, hatutakuwa na askari wenye moral ya kazi, ufanisi ndani ya majukumu haya hautatokea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie makazi ya askari, sisi ambao tupo kwenye Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama tumekuwa tukipata fursa ya kukagua na kutembelea nyumba za askari vyombo vyote hivi vya ulinzi na usalama si Magereza, si Uhamiaji, si Zimamoto, si Jeshi la Polisi, makazi yao ni duni. Alichosema Mheshimiwa Kawambwa kwamba ukiingia kwenye makazi ya Polisi, makazi ya Askari Magereza na vyombo vingine vya ulinzi na usalama amesema unaweza ukatoka ukiwa na masikitiko. Ninayo picha hapa nilikutana nayo kwenye gazeti la uhuru tarehe 17 Novemba, 2015 inahusu ukaguzi wa nyumba za askari uliofanywa na Mheshimiwa Waziri Kitwanga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, picha hii ambayo nitaileta kwako, utayaona makazi haya ni makazi duni na picha inamwonesha Mheshimiwa Waziri Kitwanga alipokuwa anatoka kwenye nyumba hiyo alishindwa kupita akainama akapindisha mgongo haikutosha ikabidi akunje na miguu ndipo akatoka kwenye nyumba hii. Nyuma yake kuna AGP Mangu analia ametoa na kitambaa mfukoni anapangusa machozi, picha hii inasikitisha sana. Kwa nini AGP ndani ya dakika chache anaingia kwenye nyumba analia? Je, askari ambaye amekaa kwenye nyumba hiyo miezi nenda rudi, miaka nenda rudi, amelia kwa kiwango gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii picha nitaileta kwako uone jinsi ambavyo AGP analia kwa sababu ya uduni wa makazi ya askari. Mheshimiwa Kitwanga kutuambia kwamba kuna fedha za Wachina kujenga nyumba za askari lazima pia tutumie vyanzo vyetu vya ndani tujenge nyumba badala ya kusubiri Wachina. Katika bajeti yakehakuna mahali popote ambapo ametenga fedha za ndani kwa ajili ya kujenga nyumba bora za askari. Ndiyo maana nikasema askari mwenye nidhamu ambaye anatakiwa apatikane kwa urahisi ikitokea dharura ni yule ambaye yupo kwenye nyumba ambazo ni za askari kwenye kituo anachofanyia kazi. Kwa hiyo, kwa stahili hii Wizara ya Mambo ya Ndani itakuwa katika kipindi kigumu sana kama hawatatenga fedha za ndani kwa ajili ya makazi ya askari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye suala la posho ya chakula kwa vyombo vyote hivi vya ulinzi na usalama. Nilishasema hapa kwamba posho hii inayoitwa ya chakula ni posho ya lishe kwa ajili ya kuwatengeneza askari, wanatakiwa wapate lishe. Hii elfu kumi kwa siku ni lishe gani ambayo askari anaweza akabajeti akapata lishe halafu akaweza kuhimili kufanya doria, kufanya kazi zenye shuruba. (Makofi)
Nimeshangaa sana Kamati ilishasema viwango hivi vya posho ya chakula ya lishe iwe inahuishwa kila mwaka, lakini mwaka huu Mheshimiwa Kitwanga ameshindwa kuhuisha posho hizi. Ndiyo maana juzi hapa Waheshimiwa Wabunge getini kwetu hapa askari ambaye ameshindwa kupata lishe bora amevamiwa na mama mmoja akamchoma kisu yule askari kwa kukosa lishe bora, hana nguvu alishindwa kuhimili kumtoa yule mwanamama aliyekuwa amemchoma kisu. Tunalipeleka wapi jeshi hili, Wizara ya Mambo ya Ndani Mheshimiwa Kitwanga angalia lishe ndiyo inawapa moral askari hawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye OC bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani imekatwa bilioni nane kutoka ile ya mwaka wa fedha uliopita. Hapa tunasema jeshi lazima liwe na fedha za kutosha OC kwa ajili ya kufanya doria kwenye maziwa, kwenye bahari wakiwa na marine police watu wa Uhamiaji waweze kudhibiti mipaka yote kwa ajili ya doria, wakimbizi waweze kushughulikiwa, magereza waweze kufanya shughuli yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini inakuwaje Wizara ya Mambo ya Ndani, fedha za OC mnadhani na zenyewe ni fedha za maandazi, mnadhani ni fedha za soda, za biskuti. Fedha hizi ni kwa ajili ya shughuli za kutoa huduma kwa ajili ya Watanzania. Sasa mnapunguza fedha mpaka zile za kununulia taarifa za wahalifu ambazo ma-RCO wote wanakuwa nazo zikitoka kwa DCI yaani Criminal Investigation Fund, watafanyaje kazi bila fedha hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara ya Mambo ya Ndani, fedha zake za OC zinafanana na fedha za maendeleo kwenye Wizara zingine kwa sababu huduma hizi zinatakiwa zifanyike kila wakati, magari yanahitajika kwenye vyombo vyote, mafuta yanahitajika. Kwa hiyo, msifikiri kwamba OC ni fedha za kukata kata tu kila wakati, wakati kwenye vyombo vya ulinzi na usalama fedha hizi ni sawa na zile ambazo zipo kwenye miradi ya maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la vituo vya polisi. Kadiri siku zinavyokwenda mahitaji makubwa ya vituo vya polisi kwenye nchi yetu yanaongezeka. Ndio maana Jeshi la Polisi walikuwa wana utaratibu wa kujenga vituo vya polisi vya tarafa ili kila tarafa iwe na vituo vya polisi. Hata hivyo, matokeo yake ni nini? Tumekuwa tukisubiri fedha zingine hizi za maendeleo ndipo zikajenge vituo hivi vya tarafa, hatutaweza kuvijenga mpaka tuhakikishe zile fedha ambazo wanazikusanya kwenye maduhuli, Bunge hili liwaruhusu fedha hizi wanapozikusanya wapate ile asilimia ambayo moja kwa moja itakwenda kujenga vituo vya polisi. Vinginevyo tutaendelea kuwalalamikia kwamba uhalifu unatokea polisi ukiwaita hawafiki kwa wakati na hata vile vituo ambavyo vipo maeneo hayo wako kwenye nyumba za kupanga, hawana magari, wengine hawana hata pikipiki, tutaendelea kuwalaumu kama jambo hili hatutalifanya kwa umakini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie magereza kwenye suala lao lenye mahitaji maalum na ndiyo maana Mheshimiwa Kitwanga katika hili naomba angalau ufungwe siku moja tu ndani ya magereza yetu ili uweze kuona jinsi wafungwa na mahabusu na hawa mahabusu nadhani kuna wakati itabidi tubadilishe sheria kwa sababu ni mahabusu lakini ukienda kule nao wanakula mlo mmoja, ukienda kule na wao mahali pa kujisaidia ni shida. Nimekwenda kule wanakwenda kujisaidia kila mmoja anawaona, tufike mahali Mheshimiwa Kitwanga tusidhani kila mtu aliye…
MWENYEKITI: Ahsante.