Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia jioni ya leo. Nimezifuatilia hotuba zile mbili vizuri na michango michache ya waliotangulia, wamenilazimisha kufikiri baadhi ya mambo ambayo ningependa niyaseme jioni ya leo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilijiuliza hivi kwa nini kulikuwa na Serikali? Nikajiuliza kwa nini kulikuwa na Polisi, Magereza, Bunge na Mahakama? Ikanirudisha nyuma kwenye kumbukumbu yangu kipindi kile ulimwengu ulipokuwa hauna utawala kwenye state of nature na human nature. Nikawakumbuka akina Thomas Hobbes walivyokuwa wanaongelea; nikawakumbuka akina John Locke, Montesk, Jean-Jacques Rousseau na wengine wengi walivyokuwa wanaelezea dunia ilikuwaje kipindi kulikuwa hakuna utaratibu uliopo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanasema hivi, kabla ya kuwa na huu mfumo tunaouona leo dunia ilikuwa nasty, ilikuwa brutal, ilikuwa inakatisha tamaa. Maisha yalikuwa mafupi, vita ilikuwa kwa kila mtu, kwa yeyote. Tena Thomas Hobbes anasema kwa lugha ya Kilatini, katika kipindi kile kulikuwa na bellum omnium contra omnes, maana yake war of all against all, yaani vita ya wote dhidi ya wote. Ndiyo tukatengeneza huu mfumo. Huu mfumo ulivyotengenezwa ulikuwa ni kwa ajili ya ku-control tabia za wanadamu na hulka yake. Usipom-control, atatumia mamlaka yake vibaya. Mwisho wa siku unapata kile kitu kinaitwa survival for the fittest. Wenye nguvu na wenye mabavu wataendelea kuwepo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema hivi? nasema hivi ku-respond yaliyosemwa hapa na waliotangulia. Askari wanatumia nguvu zilizopitiliza katika kipindi cha chaguzi na wakaelezea maeneo na maeneo. Niwaambie kitu kimoja, kama wako makini, wao ndiyo wamewafanya Askari wafikie hatua hiyo, kutokana na ile ile hulka ya mwanadamu, akishajua kwamba hakuna kitu kinachom-control anafanya vitu vya ziada, anapambana katika jinsi anavyoona yeye mwenyewe inamfaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kilichotokea kwenye uchaguzi uliopita ambao mwenzangu ameusema pale wote ni mashahidi, nani ambaye alikuwa hajui kulikuwa na watu wanaitwa red brigade wakavalishwa kininja wakapewa mazoezi ya kupambana? Sasa mlitaka Askari waangalie red brigade wakiwa wamevaa kininja wamepambana ili nchi iwe ya makambale, vita of all against all. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii wanafanya kazi yao vizuri, ninyi mnakwenda mnasema yale yasiyowezekana. Nawaombeni ndugu zangu tuelewane. Tusipofika kwenye hatua hiyo, tunarudi kwenye state of nature, tunarudi kwenye human nature. Vitu hivi lazima viwe regulated! Lazima vitengenezewe utaratibu ili twende vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na utaratibu huu wa migawanyo ya majukumu, hawa ndugu zetu Askari nao lazima tuwaangalie ili wafanye kazi zao vizuri, watulinde vizuri, ili tufike siku wafanye ile kazi inayotarajwa kuifanya nchi hii iwe nchi ya wote yenye amani inayofuata sheria na utaratibu. Wana mambo ya msingi, inabidi lazima nao tuwaangalie. Waliosema Askari kwake kambini, walikuwa wana maana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani leo Askari akatoka nyumbani kwa baba John alikopanga, akaenda ofisini, halafu anarudi akamkamate baba John, hiyo haiwezekani. Turudi kwenye utaratibu wa zamani kuwaandalia Askari maeneo ya kukaa na kuwapatia facilities zitakazowasaidia wakafanye operations zao vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi dakika zilizobaki ataongea Mheshimiwa Kingu.