Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, kumekuwa na ongezeko la mabubu na viziwi kila mwaka, mwaka wa fedha 2018/2019 kulikuwa na mabubu na viziwi 6,103; mwaka 2019/2020 walikuwa 6967; mwaka 2020/2021 idadi ya mabubu na viziwi walikuwa 7246 na mwaka 2021/2022 walikuwa 8508. Ongezeko hilo kila mwaka lina based implication watoto hao wanapokuwa mashuleni Serikali inatoa ruzuku kwa chakula kwenye shule za vitengo maalum.

Mheshimiwa Spika, tuna shule 213 na vitengo 10 vinavyofundisha mabubu na viziwi. Serikali imetumia bilioni 3.4 kwa shule ya mabubu na viziwi mwaka wa fedha 2018/2019; mwaka 2019/2020 bilioni 3.9; mwaka 2020/2021 bilioni nne na mwaka wa fedha 2021/2022 bilioni 6.3.

Mheshimiwa Spika, gharama ya walimu wanaolipwa kuwafundisha wanafunzi hao, na hata uhitaji wa wataalamu wa kuzungumza kwa alama ni mzigo mkubwa kwa Taifa ambao tunaweza kuuepuka. Hata hivyo ustawi wa rasilimali watu unapungua na well being ya mtu husika inaharibika na familia nyingi zinataabika. Kwa kuwa gharama za matibabu na hata vifaa vya mabubu na viziwi ni gharama kubwa. Serikali imeshapeleka nje watoto wengi kupandikizwa vifaa vya usikivu. Gharama ni kubwa upasuaji na machine ni dola 35000. Serikali imesema katika hotuba ya Waziri kuwa wamepandikiza usikivu kwa watoto 14 hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali kwa mara ya kwanza wakati wa awamu ya kwanza ya Waziri Ummy upasuaji umefanyika hapa nchini na bado Serikali haingalii chanzo cha yote hayo.

Mheshimiwa Spika, ushauri au mapendekezo yangu kwa Serikali; waweke audiometer katika Hospitali za Wilaya, audiometer ni kipimo cha kujua usikivu wa mtoto. Audiometer bei yake ni kati ya shilingi milioni sita had inane, na iwe ni lazima mtoto akizaliwa apimwe usikivu. Pia ABR iko muhimbili peke yake, Serikali iongeze ABR kwenye hospitali za rufaa nchini ili kubaini watoto wakiwa wadogo na kupunguza idadi ya mabubu na viziwi; matibabu hayo yaingizwe kwenye matibabu yanayohudumiwa na Bima ya Afya na pia Serikali iweke bei elekezi ya vifaa tiba kama hakuna sheria ya bei elekezi basi, Serikali ilete muswada, tutengeneze sheria.

Mheshimiwa Spika, Serikali iweke vitengo vya speech therapy kila hospitali ya rufaa na hospitali za Wilaya ili kuwasaidia watoto wa-develop speech, lakini watafute namna ya kuongeza wataalam wa speech therapy kwa sababu hawapo nchini na ni wachache mno. Watu wanapoteza usikivu kwenye migodi lakini vifaa ni ghali sana na hata wanaopata stroke wanahitaji mazoezi ya speech, vitengo vya speech na wataalamu waongezwe nchini.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.