Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

Hon. Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha mchango wangu kwa maandishi na kwa kifupi kabisa.

Mheshimiwa Spika, katika mchango wangu naomba nianze kwa kumpongeza Waziri Ummy na Naibu wake Dkt. Godwin Mollel, Katibu Mkuu na watendaji wote Wizarani kwa kazi nzuri sana wanayofanya. Lakini kipekee naomba kwa dhati kabisa, nimshukuru na kumpongeza sana Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake mahiri na jinsi anavyotubeba Watanzania kama vile mama anavyobeba familia yake. Ni kwa sababu ya uongozi wake mahiri Mawaziri wanatekeleza majukumu yao kwa umakini . Pamoja na salamu zangu za pongezi naomba kuweka mezani changamoto zifuatazo kwenye Jimbo la Arumeru Mashariki kama ifuatavyo: -

Kwanza kuna upungufu mkubwa wa vituo vya afya jimboni na hata vile vilivyopo havikidhi viwango na mfano mzuri ni Kituo cha Afya Makiba ambacho Naibu Waziri alikitembelea.

Mheshimiwa Spika, Hospitali ya Wilaya miundombinu imechakaa inahitaji ukarabati mkubwa. Mwaka jana tuliletewa shilingi 500,000,000 ambazo zilirudishwa Serikalini kabla ya kutekeleza kazi iliyokusudiwa.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.