Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

Hon. Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

MHE. KABULA E. SHITOBELO: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia katika afya ya mama mjamzito na mtoto. Pamoja na jitihada za Serikali iliweza kupunguza vifo vya uzazi kwa kina mama kwa wastani kutoka 11,000 mwaka 2015 mpaka kufikia 2020 iliweza kupunguza wastani wa vifo 3000 kwa Taifa zima.

Mheshimiwa Spika, takwimu za Kanda ya Ziwa zinaonyesha kuwa mwaka 2019 wakinamama 448 walipoteza maisha; mwaka 2020 wakinamama 410 walipoteza maisha na mwaka 2021 wakinamama 374 walipoteza maisha pia. Ukiangalia takwimu hizi utaona vifo vinapungua lakini bado hali sio nzuri.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu kwa Serikali ni kuendelea kuimarisha upatikanaji wa dawa zote za magonjwa sababishi ya vifo hivi ambayo ni kifafa cha mimba; kutoka damu nyingi kabla na baada ya kujifungua na uambukizi wa vimelea kwenye mfumo wa uzazi. Ushauri wangu mwingine ni kupeleka madaktari bingwa wa kinamama hasa katika hospitali za Wilaya na Mikoa kwani watabaini matatizo mapema na kuweza kuyapatia ufumbuzi mapema.

Mheshimiwa Spika, pia napenda kuchangia kuhusu ugonjwa wa saratani. Shirika ia Saratani Duniani (International Agency for Research on Cancer - IARC) takwimu zinaonesha kwa mwaka kuna visa vipya vya saratani 40,500 hapa Tanzania. Wagonjwa wengi wanatoka Kanda ya Ziwa na wanahudumiwa na Hospitali ya Rufaa Bugando. Wagonjwa wanaofika Bugando wanaongezeka kwa kasi sana kwa siku wanaohitaji huduma ya mionzi ni 180 lakini hospitali ya Bugando ina uwezo wa kutibu watu 80 tu kwa siku hali inayosababisha ucheleweshaji wa matibabu.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali iharakishe uletaji wa mashine mpya za kisasa na kuongeza wataalamu ili kuboresha huduma hizi.