Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

Hon. Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI: Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha mchango wangu wa maandishi.

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Waziri wa Afya na Naibu wake kwa kazi nzuri sana ambayo wamekuwa wakiifanya kwa niaba ya Watanzania wote.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu naomba niiombe Wizara iangalie kwa jicho la umakini zaidi katika maeneo yafuatayo; kwanza kumekuwepo na wizi mkubwa wa dawa katika vituo vya afya nchini, baadhi ya watumishi wasio waaminifu wanachukua dawa kutoka kwenye vituo vya afya na kwenda kuuza kwenye maduka ya watu binafsi. Wizara iweke nguvu kubwa kwenye udhibiti wa vifaa tiba na dawa.

Pili, afya kwa wanadamu ni muhimu sana, hivyo tuwekeze nguvu pia kwenye uzalishaji wa wahudumu wa afya wenye sifa na ujuzi usiotiliwa shaka. Hivyo, tupitie upya sifa zinazohitajika kwa ajili ya kuwadahili wanafunzi watarajali kwenye vyuo vya afya.

Mheshimiwa Spika, ombi, ninaomba vifaa tiba na dawa na vitendanishi kwenye Hospitali ya Wilaya ya Ngorongoro na Kituo cha Afya Samunge kilichojengwa kwa nguvu za wananchi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.