Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

Hon. Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, napenda kumshukuru Mungu kwa kazi nzuri inayoendelea kufanyika kwa ajili ya kuiboresha afya ya Watanzania.

Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Rais Samia kwa kujitoa kwake kwa Watanzania kufanya kazi nzuri na nampongeza sana.

Mheshimiwa Spika, pongezi nyingi kwa Waziri wa Afya na Naibu Waziri pamoja na watendaji wa Wizara ya Afya wote.

Mheshimiwa Spika, pamoja na pongezi na kazi nzuri inayoendelea kufanyika, naomba nijikite katika Jimbo la Temeke.

Mheshimiwa Spika, Hospitali ya Temeke iliyoko ndani ya Jimbo la Temeke imepandishwa hadhi na kuwa ya rufaa ya kimkoa lakini Serikali ilichukua hatua ya kutujengea Kituo cha Afya kilichopo Yombo Vituka kiitwachwo Malawi. Tunashukuru sana na majengo mazuri na ni ya kisasa ni ya ghorofa lakini lifti iliyoko pale ni nzima ila mkandarasi ameifunga isifanye kazi kwani hajalipwa pesa ya kuiweka pale na sasa ni zaidi ya mwaka na wahudumu wanapata taabu.