Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, kwanza nawapongeza sana kwa kazi nzuri, hii inathibitisha kuwa mnafanya kazi kama timu.

Mheshimiwa Spika, nina ushauri na mawazo machache; kwanza ni kuhusu udhibiti wa Malaria; nafahamu kuhusu Kiwanda cha Kibaha ambacho ni ubia kati ya Serikali yetu na Serikali ya Cuba, nafahamu kiwanda hiki ni muhimu sana, ikiwa tutaamua kwa dhati kutumia dawa inayozalishwa ili kutokomeza mazalia ya mbu, tutapiga hatua kubwa.

Mheshimiwa Spika, ushauri, jipeni muda kujua uhalisia na mwenendo wa Kiwanda hiki, nani anakisimamia na kwa kiwango gani.

Mheshimiwa Spika, pili ni kuhusu damu salama, napongeza hatua ya Wizara kugawa mifuko ya kukusanyia damu kwa Halmashauri zote, hata hivyo nashauri suala la hamasa ya wananchi kuchangia damu iongezeke, kwa namna gani. Nashauri namna bora ni kutoa kits kama point ambazo hizo zinaweza kumpa unafuu katika kupata huduma mbalimbali, kwa mfano tunaweza kusema kuwa wanafunzi wakiomba mkopo wa elimu ya juu, ambaye amewahi kuchangia damu anakuwa na better chance ya kupata mkopo kwa asilimia fulani zaidi kuliko mwingine.

Mheshimiwa Spika, nimetoa kama mfano lakini wataalam wetu wanaweza kutusaidia best practice ambayo italeta hamasa kuchangia damu, kwa mfano baadhi ya nchi mwenye point nyingi anakuwa considered katika nafasi kama za ajira, za jeshi na kadhalika. Hii itasaidia sana kukuza hamasa ya watu au makundi katika jamii kama vile wanafunzi kuchangia damu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ajira kwa wanaojitolea hasa pale Benjamin Mkapa, nilikuwa na mgonjwa Hospitali ya Benjamin Mkapa, mzazi. Ndugu zangu wiki mbili ambazo nimekaa pale hospitali na mzazi ambaye alijifungua wiki tatu Kayla na hivyo kulazimika kukaa kwa muda hospitali, nimeshuhudia ambavyo kwanza madaktari na wauguzi wakifanya kazi kwa bidii na moyo wa kujituma. Kwa kweli nimeona pia nilivoenda kuwaona wagonjwa ndugu zangu kwa kweli watu wanafanya kazi sana.

Ushauri wangu kuhusu ajira kwa wanaojitolea, Mheshimiwa Waziri nafahamu kwamba zipo taratibu za kiutumishi lakini zipo exceptional cases, pale Benjamin Mkapa wauguzi wa kike kwa kiume wanakesha na wale watoto waliozaliwa wakiwa na matatizo kama vile kuzaliwa kabla ya siku, wanafanya kazi, wanawabembeleza kwa moyo tena kuna wakati unakuta hata mama mzazi hawezi kumhudumia mtoto wa aina hiyo kwa kiwango cha hawa wauguzi.

Mheshimiwa Spika, ninaomba watizamwe kwa jicho la kipekee. Suala hili nimeshauri hata katika mchango wangu kwa Wizara ya Utumishi.

Kuhusu Mafinga Hospital; kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Waziri Ummy wakati ule kabla hajahamishiwa TAMISEMI, lakini pia Katibu Mkuu alipita Mafinga. Nafahamu kuwa hospitali hii iko chini ya TAMISEMI, hata hivyo ninaomba kama ambavyo Serikali imefanyia ukarabati shule kongwe, ione uwezekano wa kuzifanyia ukarabati mkubwa hospitali kongwe kama ya Mafinga ambayo inahudumia zaidi ya Halmashauri tano. Tunashukuru kupitia fedha za UVIKO tunajenga jengo la dharura, hata hivyo kwa kuwa iko kando ya highway inazidiwa sana kwa huduma. Kwa mfano katika suala la watumishi, bado nasisitiza pamoja na kuwa ni suala la TAMISEMI, Mafinga itizamwe kwa macho mawili kwa sababu ya location. Kwa mfano Mafinga inahudumia wagonjwa kutoka Ihalimba - Mkoa wa Morogoro, Mbalari - Mkoa wa Mbeya, Nyigo - Mkoa wa Njombe na pia Mufindi DC na Iringa DC. Hivyo kwa namna ambayo itawapendeza na kwa fursa zitakazojitokeza kuitizama kwa macho mawili.