Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza sana Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalimu (Mb) na Naibu wake Dkt. Godwin Mollel (Mb), Katibu Mkuu wa Wizara pamoja na Naibu wake na timu nzima ya watendaji wa Wizara pamoja na wadau wote wa maendeleo ya afya.

Mheshimiwa Spika, pamoja na pongezi hizo nina ushauri ufuatao; kumekuwa hali isiyo ya kawaida baadhi ya vituo kukosa ARVs na kulazimika kutoa dawa zilizoisha muda wake katika Wilaya ya Nyasa; uangaliwe utaratibu wa kununua dawa kwa kuwa baadhi zinanunuliwa nyingi na kupitisha muda wake wakati nyingine hazipatikani kabisa; kuna upungufu mkubwa wa vitanda na vifaa tiba muhimu katika Wilaya ya Nyasa; ni lini Wizara italeta vifaa vya upasuaji katika Kituo cha Afya cha Kihagara? Pia hali ya watumishi wa afya, madaktari na wauguzi ni wachache sana. Ni 228/800 na pia tunaomba magari ya wagonjwa.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.