Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Nkasi haipati matangazo toka TBC redio hasa wananchi wanaokaa mwambao wa Ziwa Tanganyika, naomba Wizara yako iweke mnara wa kuongeza nguvu Redio Tanzania, Namanyele - Nkasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu matangazo ya Bunge live; mimi nashauri liwe linaoneshwa siku ya Jumamosi saa tatu usiku kwa sababu mchana watu wote wako kazini wanatafuta riziki na sababu ya pili wanafunzi na walimu wao wako kazini na masomoni mchana hawana muda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya tatu hata ukichunguza mji kama Dar es Salaam kila mtu yuko na shughuli zake siku nzima hawana muda wa kuangalia tv mchana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya nne ni kwamba madereva wote wa magari ya abiria, malori, daladala na abiria zao wako safarini. Wapi nafasi wanayo? Tuache ushabiki, wanaotaka kuuza sura zao wakaombe kazi kwenye vituo vya tv.