Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

Hon. Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi hii na naunga mkono hoja iliyopo mezani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nianze kwa kuishukuru Serikali yetu ya Chama Cha Mapinduzi ambayo inaongozwa na Mheshimiwa Rais wetu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Pia nitumie nafasi hii kuwaomba Watanzania wote tuendelee kumwombea Mheshimiwa Rais wetu ili Mungu amwezeshe kumpa maono, maarifa, busara na hekima ili ajue namna bora na ambayo inastahili katika kuwaongoza Watanzania. Kwa sababu kama Mwenyezi Mungu anaweza kutupa fumbo tusiweze kuijua kesho yetu tunapolala, ni imani yangu Mwenyezi Mungu naweza kumsaidia kumpa maono yaliyo matakatifu na maono mazuri Mheshimiwa Rais ya namna ya kuwaongoza Watanzania kuwafikisha pale wanapopataka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nishukuru kwa ajili ya hatua ya kwanza ya ujenzi wa hospitali yetu ya wilaya lakini Kituo cha Afya Msangano pamoja na KLituo cha Afya cha Nkulu. Naomba nijielekeze kwenye hoja yangu ya leo, kutoa changamoto zangu ambazo zinawakumba wananchi wa Jimbo la Momba, kupitia Bunge lako Tukufu naomba niseme kwamba huduma ya afya kwa wananchi wa Jimbo la Momba kiukweli hairidhishi na ni hafifu.

Mheshimiwa Spika, tuna changamoto nyingi sana ambazo zinatukumba ndani ya Jimbo la Momba. Cha kwanza ni upungufu wa dawa kwenye zahanati zetu na kwenye vituo vya afya. Ukiangalia hatuna hospitali ya wilaya lakini hata Hospitali ya Mkoa ambayo tunaitegemea labda tunaweza tukaitumia kwa ajili ya rufaa iweze kutusaidia, bado pia ina changamoto.

Mheshimiwa Spika, changamoto nyingine ni vifaa tib ana vile vile ukosefu wa watumishi, watumishi kuwa wachache, imepelekea hata mtumishi anapopata likizo yake ambayo ni stahili yake, analazimika kufunga zahanati ili aende kwenye likizo yake na wananchi wanakosa huduma na wakati mwingine inaleta ugomvi na wananchi kuona kwamba walistahili kuendelea kuhudumiwa, lakini mtumishi hayupo ili hali huyu mtumishi ilikuwa ni haki yake kwenda likizo.

Mheshimiwa Spika, pia changamoto hizi ambazo zimeendelea kutupata zimepelekea hata wakati mwingine kuwepo na mchafuko kuzidi kwa imani za kishirikina kwenye jamii zetu, kwa sababu wananchi wanapokosa dawa kwenye zahanati kwenye kituo cha afya na ukiangalia sisi wengine majimbo yetu ni ya vijijini mtu atoke Siliwiti, Mkomba kuja kufuata huduma kwenye Kituo cha Afya cha Kamsamba, pikipiki tu inabidi atumie Sh.40,000.

Mheshimiwa Spika, mwananchi kutoka Kamsamba kwenda Vwawa inabidi atumie nauli zaidi ya Sh.15,000 na wakati mwingine ni kipindi cha mvua barabara hazipitiki. Kwa hiyo kutokana na kwamba mwananchi anaona suala la afya halina mbadala anaona atumie njia yoyote ile kwa ajili ya kutafuta afya. Ninao mfano mzuri wa Katibu wetu wa Chama Cha Mapinduzi, alipata ajali pamoja na Mwenezi mwaka jana mwezi Mei, wakavunjika miguu mara mbili, lakini kutokana na kwamba kwenye Kituo cha Afya cha Kamsamba hakuna hata x-ray ambayo angeweza kupimwa kuona inabidi apate huduma ipi akalazimika kwenda kwa waganga wa jadi na mpaka sasa hivi Katibu huyu hajapona. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa swali kama huyu tu ndio kiongozi ambaye wananchi wanamwona, kwa hiyo unaweza ukaona namna gani ambavyo kutokuwepo na vifaa tiba na dawa kwenye zahanati zetu na kwenye vituo vyetu vya afya, vinawafanya wananchi waendelee kutafuta njia nyingine mbadala ya kutafuta afya zao. Ombi langu kwa Serikali, tunaomba sana zahanati zetu ambazo zipo katika Jimbo la Momba, zipate dawa za kutosha, vifaa tiba tuweze kuvipata, whether tutapata kutoka kwenye Wizara ya Afya au Wizara Afya wataongea na TAMISEMI vyovyote vile itakavyokuwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni matumaini yangu kwamba, wananchi wa Jimbo la Momba watapata afya stahiki ili tuweze kupambana, kuendelea kujenga Jimbo letu. Pamoja na kukosekana dawa pamoja na vifaa tiba kwenye zahanati zetu na vituo vya afya, bado hata kwenye Hospitali yetu ya Mkoa wa Songwe ambayo ndio tunaitegemea kama hospitali ya rufaa kwa ajili ya kutusaidia, huduma zipo lakini haziwezi kufanyika kwa ufanisi kama inavyotakiwa, hakuna vifaa tiba kwenye suala la mifupa, hakuna Madaktari Bingwa wa watoto, hakuna Daktari Bingwa wa upasuaji, hakuna Madaktari Bingwa wa magonjwa ya ndani, hakuna Wauguzi wa kutosha, lakini hata vifaa ambavyo vinabidi viwasaidie watu ambao wana changamoto ya mifupa hakuna. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye zahanati zetu unaweza ukakuta mgonjwa anakwenda hakuna hata kipimo cha kumpima BP imepelekea wananchi hawa wanapata BP mpaka wana-paralyze, wazee wako wengi kule kila wakati kushinda kwa waganga wa jadi wakifikiri wamelogwa, lambalamba wanatusumbua kila wakati kwa sababu kila mtu anasema huyu kaniloga, huyu kaniloga, lakini kama dawa zingekuwepo za kutosha, watumishi wapo wa kutosha, wakawahudumia wananchi hawa inavyotakiwa sidhani kama kuna mtu yeyote angeenda kutafuta njia mbadala huko mahali pengine ambapo hapafai. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu kwa watu wa Wizara ya Afya, kipo kitengo kwenye Wizara ya Afya ambacho kinawatambua hawa watu wa Tiba Asili. Tunawaomba wale watu walioko kule ambao wanatoa hizi tiba asili Mheshimiwa Waziri, watoe wito wa namna ya kuwasajili ili tuwajue ambao Serikali imewaona ndio wanafaa, wanatambulika na watu na NIMR ambao wao wanafanya utafiti kwamba hizi tiba asili ndizo zinafaa, huko mitaani ni ugomvi kila mtu kaniloga, kila mtu kaniloga, watu wanauwana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hivi ni nani atajua huyu kaniloga halafu nimwache, umeona, mtu anajua fulani kamloga na yeye anaona mimi siwezi kumloga anaenda kumkata mapanga usiku. Kwa hiyo kutokana na huduma mbovu za afya ambazo zipo kwenye jamii zetu zinafanya hivyo vitendo viendee kushamiri, lakini huduma za afya zikiboreshwa na zikiwa nzuri, mtu akaenda hospitali amevunjika mguu, akapata huduma, sidhani kama atawaza kwenda kumtafuta mganga wa jadi, mganga wa jadi atakuwa wa nini? Unaweza Mbunge ukaenda kufanya mkutano wa hadhara, lambalamba akapata wafuasi kuliko hata wewe kiongozi ambaye unaenda kuwaambia mambo mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lambalamba amejaza watu kwa sababu gani? Kwa sababu anatoa matunguli, wewe hapo unaumwa mguu kwa sababu huyu alikuloga, wewe hapa ulivunjika mguu hauponi kwa sababu hivi. Sasa huyu ataponaje wala hata hajapimwa, usikute hata mfupa umeoza. Sasa hivi kwenye Hospitali yetu ya Mkoa wa Songwe tunaye mwananchi ambaye amekaa zaidi ya miezi sita, alivunjika mguu ameenda kwa waganga wa jadi, amekaa huko hajapona, mfupa sasa hivi unaoza, lakini kungekuwa na x-ray kwenye vituo vyetu vya afyam akapata huduma inayostahili, kusingekuwa na hii migongano kwa ajili ya kuendelea kufanya jamii zetu ziendeā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)