Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Naomba niungane na wachangiaji wote walio mshukuru Mungu kwa majaliwa yake kwetu sote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa kazi kubwa inayofanya. Mimi nichangie tu mchango mdogo sana, la kwanza ni kwenye Bima ya Afya.

Mheshimiwa Waziri Bima ya Afya kwa baadhi ya hospitali imekuwa tatizo kubwa sana. Nadhani ni wakati muafaka wa kufanya tathmini kuongeza idadi ya watu tutakaowataka maoni yao kuhusu suala la Bima ya Afya.

Mheshimiwa Spika, Bima ya Afya huduma inayotoa Benjamin Mkapa, Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na baadhi ya hospitali hapa nchini inatolewa kwa hatua ya juu sana, lakini katika hospitali nyingi nchini Bima ya Afya inalalamikiwa sana. Nadhani ifike mahali sasa tuone kwamba namna ya Bima ya Afya ni pamoja na kuangalia utoaji wa huduma kwa wanachama wake na jinsi ambavyo kila hospitali nchini inakuwa na dirisha na Afisa anayehudumia pamoja na Daktari. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukienda Benjamin Mkapa na ukaenda Hospitali ya Rufaa ya Dodoma wanao Madaktari waliopangwa kuhudumia watu wa Bima ya Afya, lakini katika hospitali nyingine wanachama wa Mfuko huu wa Bima ya Afya na Makundi yale mengine ya Bima ya Afya wanalalamika sana. Jukumu letu kubwa ni kusema yale ambayo ni mazuri na yale ambayo kidogo wapokea huduma wanalalamika. Mimi nadhani tuongeze wigo wa mikutano kwa mwaka kama mara mbili kwa wale wapokea huduma ili tujue wanasema nini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, eneo lingine ni eneo la utendaji wa MSD. Kupitia Bunge hili nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Mkuu. MSD utendaji wao tumechoka, MSD nanunuzi yenyewe yanachukua miezi Sita, mifano hai ambulance tunazosubiri sasa ni miezi sita, lakini pia picha ya wazi ipo kwenye Halmashauri ya Mji wa Mbulu. Tumeagiza jokofu ni miezi sita sasa, jokofu halijaletwa wananchi wanapata matatizo, tumehangaika vya kutosha.

Mheshimiwa Spika, hebu tuulizane kumbadilisha Mkurugenzi Mkuu inatosha Mheshimiwa Waziri? Kupitia ile ziara ya Waziri Mkuu hadi sasa, kwa nini tusiangalie kurudi kwenye suala la kuangalia upya mfumo mzima wa MSD na watendaji wake? Jambo hili linawaumiza watanzania walio wengi, kwa sababu tunaweza tukambadilisha Mkurugenzi Mkuu lakini MSD ikabaki na mfumo uleule ambao una matatizo. Nilitegemea baada ya ziara ya Waziri Mkuu, naamini Mheshimiwa Waziri Mkuu amefanya kazi kubwa sana Serikali haitachukua hatua. Lakini ni wapi tumepoteza hata ile sura ya kutumbua tumbua, tukatumbue tumbue huko huko MSD kwa sababu kuna matatizo sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, katika hali ambayo tunafanya hii kazi ya kuwawakilisha wananchi, wananchi wanalamika kule, hiyo MSD yenyewe ukizungumza upande mmoja, Mbulu Mji hatuna ambulance, x-ray, mortuary. Hivi kweli Watanzania wa Halmashauri ya Mji Mbulu inazungukwa na eneo lote la vijijini, huduma ni pale katikati, vitu vyote hivyo havipo! Pamoja na kwamba Mheshimiwa Waziri tunakupongeza sana umefanya kazi kubwa sana ulipokuwa Wizara hii ndiyo maana Mheshimiwa Rais amekuona akakurudisha Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, hivi kweli watanzania wa Mji wa Halmashauri ya Mbulu Hospitali ya Mji wa Mbulu inazungukwa na eneo lote la vijijini huduma ni pale katikati vitu vyote hivyo havipo. Pamoja na kwamba Mheshimiwa Waziri tunakupongeza sana umefanya kazi kubwa sana ulipo Wizara hii ndio maana Mheshimiwa Rais amekuona akakurudisha Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa nashauri kama itawezekana tuone utaratibu wa namna gani tunaweza tukatazama. Kama ni sisi tunashindwa kumudu huduma hizi za upatikanaji wa dawa na huduma zingine tukae chini tuangalie, ni utaratibu gani utakaowawezesha Watanzania kupata huduma ya dawa na huduma nyingine za matibabu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia ufunguzi wa zahanati. Halmashauri ya Mji wa Mbulu tayari tuna zahanati nne zilizo tayari zimeanzishwa kwa mchakato wa wananchi takribani miaka kama saba, nane, sita sasa hivi ziko tayari kibali tu cha kusajili zahanati hizi imechukua zaidi ya mwaka. Wananchi waliouza mali zao waliotumia nguvu zao wakajenga zahanati hizo wanasubiri huduma lakini huduma haziwafikii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nadhani tuharakishe utaratibu huu wa mchakato wa kusajili zahanati na vituo vya afya ili walau, huduma za mwanzo zianze kutolewa tuweze kufanikiwa namna ambavyo tunaweza tukapata hali halisi ya mafanikio katika utoaji wa huduma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wananchi hawatuelewi kabisa wanapoona wamemaliza kujenga zahanati mwaka wa kwanza unakwisha mwaka wa pili unakwisha. Ninawaomba sana watu wa Wizara ya Afya na TAMISEMI kaeni pamoja mtufungulie hizo zahanati ili wananchi wapate huduma za mwanzo. Mwananchi analalamika anapotoka kwenye Kijiji kwenda kwenye Hospitali ya Mji kwa gharama pengine ya Shilingi 20,000 kwenda Shilingi 10,000 na kurudi Shilingi 10,000 lakini huko huko dawa anagharamikia nafuu angekuwa anapata hiyo huduma anayofuata pale alipo ili gharama za usafiri zisiwepo kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, eneo lingine ni matumizi ya lugha ambayo hayaridhishi. Yapo matumizi ya lugha kwa baadhi ya watumishi wetu wa sekta ya afya hususani wale ambao tunawaita wakunga, wauguzi pamoja na madaktari. Lugha ya daktari ni sehemu ya tiba anapotumia lugha ambayo mgonjwa akifika anaongezeka ugonjwa ni shida sana. Mheshimiwa Waziri ninakuomba sana katika jambo kama hili tusione haya kuchukua hatua unapofanya ziara. Alikuja Naibu Waziri wa TAMISEMI Afya alikuta madudu kule Mbulu alipewa taarifa ambayo haina uhalisia, alipokwenda kwenye nyaraka inapishana na taarifa ambazo amepewa hadi leo hakuna hatua iliyochukuliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi nadhani kama Waziri wa TAMISEMI amefanya ziara awasiliane na Waziri wa Afya hatua zichukuliwe mapema ili huduma ibadilike, lakini pia wananchi waone kuna mabadiliko baada ya maagizo ya viongozi wanaokuja. Mwisho niseme tu kwamba ninaomba sana Wizara ya Afya itembelee Hospitali ya Mji wa Mbulu ina matatizo nyinyi kama Wizara chukueni majukumu yaliyo yenu TAMISEMI kama Wizara itachukua majukumu yaliyo yao, ili kuona ni kwa namna gani walau Hospitali ya Mji wa Mbulu inakuwa sehemu ya kimbilio kwa huduma za afya kwa wakati wote katika hali ya kumhudumia mwananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hili suala la Ambulance Mheshimiwa Waziri wa Afya Mheshimiwa Jafo alipokuwa Waziri nimeandika barua hakuna Ambulance iliyokwenda, nimeomba Ambulance hakuna Ambulance iliyokwenda, sasa hivi tena ni mwaka unakwisha. Jamani kama ni namna hii tungeelezwa lugha ya wazi tu kwamba Ambulance hizo hazipo, X-Ray hiyo haipo lakini pia tungeelezwa kama ambavyo dawa inakosekana. Mimi nilikuwa nashauri kwenye dawa tuna shida gani tusiweke alama kwenye dawa za Serikali kama tatizo ni wizi. Tuna ugumu gani wa kuweka alama ya Serikali kwenye dawa za Serikali ili upotevu wa dawa na wizi wa dawa…

SPIKA: Kengele ya pili hiyo Mheshimiwa. Kengele ya pili imeshagonga.

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Naunga mkono hoja. (Makofi)