Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na kuniwezesha kuchangia hotuba hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vyombo vya habari ni muhimu katika kuwaelimisha wananchi kwa kupata habari kwenye tv na redio pamoja na magazeti, lakini pia wakati wengine vyombo hivi hivi vinapotosha. Kwa hiyo wawe na umakini kwa sababu utaona habari ni ile ile lakini huwa tofauti wakati wa matangazo au machapisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitendo kilichofanywa na Serikali sio haki kuzuia vyombo vya habari kuonesha Bunge wakati wa vikao vya Bunge hii ni uonevu kwa sababu wananchi Bunge ni lao, vyombo ni vyao na Wabunge wanachangia ni Wabunge wao wamewatumia kero zao kwa nini wananyimwa uhuru wao wa kuona Wabunge wao waliowatuma?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini wanamichezo wetu hasa wanawake wapokwenda nchi za wenzetu kucheza hawapati ushindi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la TBC ni chombo cha Serikali lakini chombo hiki hakiwatendei haki Watanzania kwa sababu hizo pesa wanazotumia ni za walipa kodi wa Tanzania, ukiangalia hiki chombo kina ubaguzi hasa wakati wa uchaguzi, tafadhali mtende haki. Serikali ni yetu sote hata ikiwa hatoki katika Chama cha Mapinduzi wakati uchaguzi umekwisha sasa kiongozi yeyote aliopo ni wetu sote acheni ubaguzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naomba kuwasilisha.