Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia bajeti ya Wizara ya Maji na ninaomba nianze kwa kumpogeza Mheshimiwa Rais kwa jitihada zake za kumtua mama ndoo kichwani kwa kuipatia shilingi 709,361,607,000 kwa maendeleo ya miradi ya maji katika Taifa hili.

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya jitihada kubwa za kuchimba visima maeneo oevu ili kuboresha hali ya upatikanaji wa maji. Ninaiomba Serikali iongeze fedha kupitia bajeti hii ili visima vingi vichimbwe nchini ili kuzidi kutatua changamoto ya maji katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, nchi yetu ina miradi mingi ya maji ambayo haijakamilika, niombe Serikali ikamilishe miradi yote ambayo imeshaanza ili kuweza kuwatua akimama ndoo kichwani katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, niendelee kuishukuru Serikali kwa jitihada zake za kuhakikisha tatizo la maji linamalizika hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.