Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Amina Daud Hassan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. AMINA DAUDI HASSAN: Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza sana Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha nyingi katika Wizara ya Maji ili kuhakikisha maji yanapatikana na kumtua mama ndoo kichwani katika kutafuta maji.

Mheshimiwa Spika, pia nimpongeze Waziri wa Maji na Naibu wake kwa kuaminiwa na Rais kwa kazi nzuri wanayoifanya kwa kuendeleza malengo ya Rais wetu kuwa wanahakikisha maji yanapatikana.

Mheshimiwa Spika, mimi nijikite katika suala la uchimbaji wa mabwawa na visima nchini, naishauri Serikali iongeze fedha katika uchimbaji wa mabwawa na visima ili kutatua tatizo la maji katika maeneo ambayo hayana vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Spika, lingine kuna maeneo ambayo maji yanaharibika kwa kuwa hakuna usimamizi katika maeneo ya vyanzo vya maji. Niiombe Serikali isimamie na kulinda maeneo hayo kwa kuweka walinzi ili kulinda maji ambayo ni uhai.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.