Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha mchango wangu wa maandishi katika Wizara hii muhimu sana kwa maisha ya wananchi wangu wa Mkoa wa Katavi.

Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kuhakikisha anakwenda kumtua ndoo mama kichwani. Katika mwaka mmoja sasa Mheshimiwa Rais ameonesha njia nzuri ya jinsi ya kupambana na kutatua changamoto ya maji katika nchi yetu na sisi kama wawakilishi wa wanawake tutaendelee kumpatia ushirikiano wa dhati ili kutimiza azma yake ya kuwatua ndoo kinamama wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, naomba nimpongeze Mheshimiwa Juma Aweso, Waziri wa Maji kwa kazi kubwa anayoifanya ya kumsaidia Mheshimiwa Rais kuhakikisha huduma ya maji inapatikana katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, lakini nimpongeze Mheshimiwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji kwa kazi kubwa wanayoifanya, ukweli kazi inafanyika na inaonekana. Pia nimpogeze Naibu Waziri mwanamama shupavu Mheshimiwa Maryprisca kwa kazi kubwa anayoifanya kuwasaidia akinamama wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kumpogeza Mheshimiwa Waziri lakini bado kuna changamoto ndogo ndogo zilizopo katika Mkoa wa Katavi. Lengo la Serikali ni kufikisha maji kwa mijini asilimia 85 na vijijini kufikia asilimia 60, lakini kwa Mkoa wa Katavi bado ile azma ya Serikali bado haijafikia.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha changamoto za maji katika Mkoa wa Katavi, kumekuwa na kukatikakatika kwa maji, inafikia hatua mwezi mzima maji hayapatika katika baadhi ya maeneo, lakini wananchi wamekuwa wakiletewa bill kubwa za maji na kubambikiwa bill za maji kutokana na mita kutokuwa za uhakika. Nashauri Mheshimiwa Waziri zifungwe mita za uhakika na ziwe na uwazi mkubwa ili wananchi wetu wawe na uelewa kusoma bill zao.

Mheshimiwa Spika, ilikutatua changamoto ya upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Katavi lazima mradi wa ziwa tanganyika ufanyike kwa haraka ndio utakuwa mkombozi mkubwaa wa wananchi wa Mikoa Kigoma,wakatavi na Rukwa. Naunga mkono hoja.