Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, vituo vya televisheni hasa Clouds, vinaonesha miziki ambayo haiendani kabisa na mila na utamaduni wetu. Wasanii hucheza miondoko isiyofaa. Pia mavazi ya wasanii wanawake (wanenguaji) na hata baadhi ya waimbaji yamekithiri kwa utovu wa maadili na vigezo vya mila zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Kamati ya Maudhui ya TCRA iwajibike ipasavyo. Inasikitisha sana kuona wasanii wakiwa uchi (wengine wakiwa na nguo za ndani tu) wakioneshwa na televisheni zetu, tena muda wa mchana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara na TCRA ni lazima wawajibike ipasavyo haraka iwezekanavyo.