Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kuwapongeza sana Mheshimiwa Jumaa Aweso, Mbunge na Waziri wa Maji na Naibu wake Mhandisi Maryprisca Mahundi, Mbunge kwa kazi nzuri ya kuwahudumia wananchi kupitia Wizara wanayoiongoza.

Mheshimiwa Spika, nawapongeza pia Katibu Mkuu Mhandisi Anthony Sanga na Naibu wake Mhandisi Nadhifa Kemikimba pamoja na watendaji wote wa Wizara akiwemo kijana mdogo Engineer Maduhu anayekaimu Wilaya yangu ya Nyasa.

Nawashukuru kwa miradi ya maji inayoendelea jimboni kwangu, hata hivyo nina maombi yafuatayo; kwanza ni kuhusu ukanda wa chini (mwambao wa Ziwa); Wilaya yangu ina milima na ni kubwa sana. Gari iliyopo ni chakavu sana. Tunaomba gari ili kufuatilia vizuri utekelezaji wa miradi.

Pili, kutatua kero ya changamoto ya maji, utekelezwe mradi wa Ngumbo na Liwundi, kukarabati mradi wa Kihagara, kuongeza upatikanaji wa maji katika Mji wa Mbamba Bay na vijiji vyake.

Mheshimiwa Spika, tatu, kupeleka maji kijij cha Mtupale hadi Chiwindi.

Kwa upande wa ikanda wa juu; kupeleka maji Kijiji cha Malayalam, Kimbango, Litindo Asili na Luhangalasi (Kata ya Luhangalasi); kupeleka maji Kijiji cha Luhindo; kupeleka maji Kijiji cha Uhuru na Mipotopoto na kupeleka maji Kijiji cha Mitomoni.

Mheshimiwa Spika, tunasisitiza matumizi ya maji ya Ziwa Nyasa.

Mheshimiwa Spika, nawashukuru na naomba kuwasilisha.