Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kuungana na viongozi wenzangu wote kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa majaliwa yake kwetu sote, kwani tunajivunia kwa jinsi alivyotuvusha kwenye majanga mbalimbali kwa mfano corona na ustawi katika nyanja za kisiasa, kiuchumi, kidplomasia, kisiasa, amani, mshikamano wetu kitaifa, hongera sana mama.

Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kwa niaba ya wananchi wote wa Jimbo la Mbulu Mjini kutoa pongezi nyingi sana kwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wetu mpendwa kwa jinsi anavyoiongoza nchi yetu na kusimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM yam waka 2020/2025.

Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kuwapongeza Mheshimiwa Makamu wa Rais, Mheshimiwa Waziri Mkuu, Waziri wa Wizara hii, Mheshimiwa Naibu Waziri wa Wizara na Mheshimiwa Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii kwa jinsi mnavyoitendea haki Wizara hii kwanza kutusikiliza sisi wawakilishi wa wananchi na kutatua tatizo la maji kwa nchi nzima, hongereni sana.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nitoe mchango wangu kupitia hotuba ya Wizara hii, Mheshimiwa Waziri pamoja na timu yako nzima naomba kukueleza masikitiko yangu kwa kuwa katika mpango wa bajeti mwaka 2016/2017 Halmashauri ya Mji wa Mbulu ilikuwa miongoni mwa miji itakayonufaika na mradi wa miji 28. Binafsi mimi nasikitika kwa sababu hata wakati tunaondolewa mimi kama mwakilishi wa wananchi sijashirikishwa, wakati Jimbo la Mbulu Mjini kuna kama 17 kata 10 eneo la vijiji 34 na kama saba yenye mitaa 58, hadi sasa ni kisima kimoja tu cha Bargish Antsi kilichimbwa 2016/2020. Hivyo basi kupitia kauli yako ya wali wa kushiba unaonekana kwenye sahani. Tunaomba mturudishe kwenye miradi ya P4R kutokana na eneo hilo la vijiji 34 na kutuongezea fedha zaidi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tuliwasilisha maombi yetu ya nyongeza ya fedha za miradi kutoka milioni 700 mpaka bilioni 1.5 lakini kiasi hicho hakipo kwenye mapendekezo bajeti ya mwaka 2022/2023 na document hizo ninazo kwenye tablet yangu. Ninapata wakati mgumu sana kushika shilingi yako, hivyo kwa heshima kubwa ninakuomba mdogo wangu kaa na timu yako kuona njia mbadala ya kunusuru hali hii, chonde chonde.

Mheshimiwa Spika, ninaiomba Wizara yetu hii iagize makusanyo ya mapato ya bili za maji katika maeneo yote ambayo tayari kuna DPS za maji nchini kwani hali hii itasaidia kudhibiti upotevu wa fedha za mauzo ya maji.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maji itazame utaratibu wa mapendekezo ya majina ya bodi za maji kwani kwa sasa mchakato wa wajumbe wawili wa bodi mpya kwa kila nafasi kwenye ngazi za Kata, Baraza la Madiwani na baada ya hapo Meneja wa RUWASA ngazi hiyo kuwasilisha ngazi ya Mkoa na Wizara kwa ajili ya kupata wajumbe mahiri katika kusimamia utoaji wa huduma bora za maji kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, mwisho, naomba kuwasilisha na naunga hoja kwa asilimia mia moja.