Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima. Pia nimpongeze sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri sana anayoifanya kwa kuwatumikia Watanzania.

Pia niwapongeze Mheshimiwa Jumaa Aweso, Waziri wa Maji, Mheshimiwa Engineer Maryprisca Mahundi, Naibu Waziri wa Maji, Katibu Mkuu pamoja na watumishi wote wa makao makuu ya Wizara ya Maji pamoja na RUWASA kwani wanafanya kazi nzuri sana.

Mheshimiwa Spika, kipekee niwapongeze Engineer Walter, Meneja wa RUWASA Mkoa wa Manyara na Engineer Idd Msuya - Mkurugenzi Mtendaji wa BAWASA, wanafanya kazi nzuri sana. Naomba sana watumishi hawa waendelee kutusaidia ili kukamilisha miradi inayoendelea.

Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa kutupatia fedha kwa ajili ya maji ya mji wa Katesh wa shillingi 2,300,000,000 ambapo mabomba yameanza kupokelewa ili kusambaza maji, pia mradi wa maji Gehandu na visima 24 ambavyo vinaendelea kuchimbwa kwa fedha za mwaka 2021/2022.

Mheshimiwa Spika, baada ya shukurani nilizotoa hapo juu Wilaya ya Hanang ni kubwa, ina kata 33, vijijini 96 na maeneo mengi hayana maji, naomba mtuangalie kwa jicho la kipekee kwa kukamilisha miradi inayoendelea ya Ziwa Bassotu (mradi wa vijijini 12), mradi wa Gehandu; pia miradi mpya ifanyiwe usanifu kwenye chanzo cha Mto Duru- Masakta, maji ya Bwawa Bassotughang iliyopo kijiji cha Bassotughang, kata ya Hidet ili yatumike kwa matumizi ya binadamu na mifugo.

Mheshimiwa Spika, mimi ninaimani kubwa sana na Mheshimiwa Waziri na timu yake, ila atusaidie Wilaya ya Hanang kwani Meneja wa Wilaya tuliyenaye kweli hafanyi vizuri na Mheshimiwa Waziri alipokuwa Kongwa alitamka kumfukuza kazi na analalamikiwa sana kwa kufanya kazi chini ya kiwango. Hivyo ili meneja huyu asiharibu kazi nzuri inayofanywa na Serikali apangiwe majukumu mengine atakayomudu vizuri.

Mheshimiwa Spika, baada ya mchango wangu huu naomba kuunga mkono hoja.