Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia katika Wizara hii ya Maji kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Kwanza kabisa napenda kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuongoza Taifa letu kwa ufanisi mkubwa.

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Waziri wa Maji pamoja na timu nzima ya Wizara kwa kazi kubwa wanayoifanya katika sekta hii ya maji. Pia naipongeza Wizara kwa miradi mikubwa ya maji katika Jimbo la Babati Vijijini hasa miradi ya Darakuta - Magugu hadi Mwada; Mradi wa Mayoka - Minjingu, Vilima Vitatu, Madunga na maeneo mengine. Fedha za UVIKO zimesaidia mradi wa maji wa Bashnet na Secheda.

Mheshimiwa Spika, naomba sana Wizara itekeleze ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ya mradi wa maji wa Darakuta-Magugu-Mwada hadi Minjingu.

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji wa Dareda; mradi mkubwa wa Ziwa Manyara ambao utahudumia kata zote za Tarafa ya Bashnet.

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji wa Kata za Gidas, Duru, Riroda na Endadosh na Ayasanda.

Mheshimiwa Spika, nawapongeza tena Wizara hii kwa kazi nzuri na naunga mkono hoja.