Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Utanisamehe sauti yangu leo si nzuri sana. Lakini kwanza kabla ya yote kabisa nimpongeze sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayofanya kutatua kero za maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Kiteto wakati tunachaguliwa Mkoa wa Manyara, nilishazungumza hapa mwaka jana, upatikanaji wa maji ni asilimia 58, way below national average. Lakini nafurahi sana kwamba kwa mwaka jana na mwaka huu bajeti ya mwaka huu, nilikuwa naongea na Engineer wananiambia kwamba mpaka Disemba tutakuwa tumefikisha asilimia 68 well done. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kumpongeza Mheshimiwa Rais nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri, Katibu Mkuu na timu yao wote kwakweli kwa kazi kubwa wanayofanya kumsaidia Rais. Tunaona kila mahala wanapokwenda kusimamia miradi ya maji big up. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mkurugenzi wa RUWASA na Meneja wa RUWASA Mkoa wa Manyara kwakweli kwa kazi kubwa wanayofanya. Ndiyo maana Mheshimiwa

Makamu wa Rais wakati alipotembelea Simanjiro aliahidi fedha kwa Meneja wa RUWASA wa Mkoa kwa kazi kubwa anayofanya, hii ni kutambua kazi yake kubwa anayofanya. Meneja wa RUWASA Kiteto anafanya kazi nzuri sana. Kwa kweli timu hii mmejipanga vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nilishazungumza hapa, kwamba Kiteto ni jimbo moja kubwa sana, zaidi ya Mkoa wa Kilimanjaro. Meneja wa RUWASA Kiteto hana gari. Alishalala siku moja mpaka saa nane kwenye mapori yale. Mheshimiwa Waziri tunaomba Landcruiser moja nzuri sana ili huyu meneja apate kufanyakazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais alituletea mradi mkubwa sana wa maji pale Mjini Kibaya Kata ya Kaloreni wenye thamani ya shilingi milioni 400; ni mradi mzuri sana. Lakini nilisema mwaka jana kwamba miundombinu ya mabomba pale mjini yamechakaa. Kwa hiyo, hata tukipata haya maji ya milioni 400 bila kufumua mabomba ya mjini pale, na nilikuomba milioni 100, hata huo mradi hatutafaidi sana itakuwa na linkage. Naomba milioni 100 ili tufumue mifumo ya maji pale ili wananchi wa-enjoy maji milioni yenye thamani ya Shilingi milioni 400 ambayo yameletwa na Mama Samia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu mabwawa. Kiteto ni kame. Nilishazungumza hapa tarehe 10 mwezi wa pili mwaka huu, kwenye swali namba 84, kuhusu Mabwawa ya Dongo, Dosidosi na Kijungu. Mliniahidi kwamba mtapata fedha na mtajenga mabwawa haya.

Naomba kwakweli Mheshimiwa Waziri nikufahamishe kuwa ilikuja timu ya Dosidosi hapa wakifuatilia Bwawa lao la Dosidosi; na nimeshazungumza mara nyingi sana hapa, kwamba wilaya hizi ambazo ni kame tusipopata mabwawa kwaajili ya wakulima na wafugaji kwakweli changamoto za ukame hata mifugo imekufa sana mwakajana kwasababu ya ukame huo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri mimi najua bajeti hii umetutengea karibu bilioni mbili tena, tunakushukuru sana. Tunayaomba sana Mabwawa haya ya Dongo, Dosidosi, Kijungu ili wananchi hawa wakapate kunufaika na maji.

Mheshimiwa Spika, napenda pia niwashukuru wadau wa maendeleo wanaosaidia miradi ya maji Kiteto kama vile OIKOS. Juzi tu siku mbili zilizopita tumekwenda kuzindua mradi wa vijiji 16 miradi ya maji ninawashukuru sana OIKOS. Kwakweli Mheshimwia Waziri hili Shirika la OIKOS mlisaidie na muwape support nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maabara ya maji naambiwa zilikuwa takriban 16 nchi hii lakini wameleta maabara ya maji Mkoa wa Manyara, Shirika hili la OIKOS.

Mheshimiwa Spika, mashirika mengine yanayojishughulisha na miradi ya maji kwenye Jimbo la Kiteto ni; Shirika la PINGOS, ELEWA AFRICA, KINAPA na PICODEO.
Mashirika haya yanahitaji support sana; na ninawashukuru sana kwa kazi kubwa wanayofanya. Juzi tu Kata karibu 10 zimenufaika na mradi huu Kata za Makame, Ndedo, Engusero, Lengateri, Loolera, Matui, Ndiringishi, Magungu na Bwawani kata 10 vijiji 16 kwakweli wanafanyakazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tulishazungumza mimi na Mheshimiwa Waziri na nilimualika aje Kiteto; na kati ya maeneo ambayo nilimuahidi tutatembelea ni kwenda Dongo kuangalia Bwawa la Dongo. Naomba sana, baada ya bajeti hii ambayo mimi najua itapita kwa speed kubwa sana kwa kazi unayofanya; tupange utembelee Kiteto. Vilevile nilimualika na Naibu Waziri pia twende Kiteto. Mheshimiwa Waziri tutampeleka Dongo huku huyu tutampeleka umasaini huko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Kiteto kwakweli kwa kasi ya maji, alikuwa ananiambia meneja wangu wa RUWASA, kwamba mpaka Juni mwaka huu tutakuwa tumetoka asilimia 52 ya maji mpaka asilimia 68, ambayo ni nzuri sana. Tukiendelea na kasi hii ile dream ya mama yetu yakuleta maji asilimia 95 vijijini na 85 tutafikia bila shida yoyote.

Mheshimiwa Spika, wakati Mheshimiwa Waziri, atakapohitimisha bajeti yake nitataka baadaye atuambie, zile mashine ambazo Mama Samia alisema ataleta kila mkoa hebu mtuambie imefikia wapi? Kwa sababu sasa tunataka kujishughulisha na mambo ya mabwawa yetu. Akifanya hivyo kwakweli Mwenyezi Mungu atambariki sana.

Mheshimiwa Spika, kwakweli Wizara Maji kwa kazi wanayofanya kwakweli tuwasaidie wapate pesa hizi za bajeti ili miradi hii ikatekelezwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya naomba kuunga mkono hoja, ahsanteni sana. (Makofi)