Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipatia fursa angalau na mimi kuwasemea wananchi wenzangu wa Jimbo la Singida kaskazini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nianze kwa kuchukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa uzima na afya. Pia nitangulize shukrani zangu nyingi sana kwa Waziri wetu Pamoja na Naibu wake kwa kazi kubwa wanayoifana kuhakikisha nchi yetu inapata maji. Na hapa lazima tutambue juhudi kubwa zinazofanywa na Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Kusema kweli hata ukifuatilia hotuba yangu yam waka jana kwenye wizara nilikuwa mkali sana na nilisikitika kwa ile hali ya wananchi wetu kunywa maji pamoja na Wanyama. Lakini mwaka huu nitakwenda kuzungumza kwa kutoa shukrani na pongezi kwa kazi kubwa ambayo imefanyika kwa kipindi hiki kifupi cha miaka hii miwili au huu mwaka mmoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Singida Kaskazini tumepata miradi mipya yam aji 15 ambayo inatafikisha asilimia 67 ya upatikanaji wa maji endapo miradi itakamilika ipasavyo, ambapo tumepata visima 15 vyenye thamani ya shilingi milioni 420 kila kimoja katika Kijiji cha Ntondo, Kwae, Sekotoure, Kinyamwenda, Msikii, Mwalala, Poku, Igauri, Mwakiti, Itamka, Mkenge, Makuro, Misinko, Msimihi na Maghandi. Maeneo haya sasa yanaenda ya kupata uponyaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na nichukue fursa hii pia kuwapongeza watendaji wa Wizara ya Maji, kwa maana ya RUWASA pale Mkoani. Meneja wa Mkoa pamoja na Meneja wa Wilaya pamoja na staff wao kwakweli wanatupa ushirikiano sana katika kuhakikisha jamii yaw ana Singida inapata maji safi na salama wakati wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwashukuru pia wadau wa Sekta Binafsi wanaoshirikiana na Serikali kuhakikisha wananchi wetu wanapata maji, wakiwemo World Save International, World Division pamoja Silver Crescense ya kutoka Uturuki ambao wametusaidia kukarabati na kuchimba visima vipya vipatavyo 44 katika vijiji mbalimbali vya Jimbo letu la Singida Kaskazini. Kwa hiyo, ninaendelea kuwashukuru na kuwaomba waendelee kutupa ushirikiano kuhakikisha kila mtu katika Jimbo letu la Singida Kaskazini anapata maji safi na salama wakati wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niende kwenye kuwasilisha changamoto chache ambazo ninaomba sana Mheshimiwa Waziri azingatie na kuhakikisha tunazipatia ufumbuzi ili tuendane na hii kasi ambayo nimeizungumza hapa tunayoitarajia, ya kupata maji safi. Moja ya changamoto kuna vijiji ambavyo tuliwahi kuchimba maji lakini kwakweli maji haya yanapatikana ya chumvi na si salama kwa binadamu. Kwa hiyo, maeneo yale yanahitaji tupeleke bomba. Mojawapo ni kijiji cha Gaiye kitongoji cha Gairu katika kijiji cha Sagara pamoja na kijiji cha Mangida tumechimba visima kadhaa lakini maji hayakupatikana. Kwa hiyo maeneo haya nimuombe sana Mheshimiwa Waziri tuende tukafanye usambazi kutoka kwenye kile chanzo cha Sagara ambacho kina maji ya kutosha; lakini tu hatujatandika mabomba niombe sana tufanye usambazaji tuwapelekee hawa wananchi maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi siku nilienda kuomba kura pale walinipa maji ya chumvi. Tafsiri yake ni kwamba yale maji kama yanafaa nami niyanywe. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri nikukaribishe siku moja na wewe uje haya maji uone kwamba kuna shida. Kwa hiyo, nikuombe ushirikiano tuwasambazie maji na wala si umbali mrefu ni kama kilometa moja tu ambayo wala si gharama kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, nimetaja miradi mikubwa sana ya maji hapa, nikiacha ile minne ambayo tayari imeshakamilika. Ule mradi wa Wamitura ambao una thamani wa Shilingi milioni 565 kuna ule mradi wa Mweghanji shilingi milioni 565, ule mradi wa Ndibeshi Shilingi 565. Miradi hii ina gharama kubwa lakini changamoto kubwa ipo kwenye usimamizi. Idara yetu ya RUWASA hawana vitendea kazi hata gari hawana. Unampa mtu mradi wa shilingi billions of money lakini namna ya kuusimamia kufika pale kwenye field hawana uwezo huo kwasababu ya vitendea kazi.

Niombe sana tuwasaidie hawa watu wapate magari, wapate vitendea kazi ili waweze kufika kwenye maeneo ya kazi kwa wakati na kuhakikisha miradi hii inakamilika kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na eneo la jumuiya za watumia maji amezungumza Mbunge dakika mbili tatu zilizopita kuhusu uwezo mdogo alionao wakifedha hata kitaalamu. Tunategeneza miradi ya kutosha ya fedha nyingi lakini kwenye eneo la uendeshaji tunakwama. Niombe wale watalamu wawili mhasibu pamoja na fundi hawa wawe ni waajiriwa wa Serikali pamoja na fundi hawa wawe ni waajiriwa wa Serikali na walipwe na Serikali ili tuweze kuwa- manage, na tuweze kuwafuatilia na kuwasimamia ipasavyo. Hii itasaidia kwenye ufanisi kwa maana ya efficiency ya hii miradi pamoja na kudumu iweze kudumu ili kuendelea kuwahudumia wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ningeomba pia Wizara wanisaidie, hasa Mheshimiwa Waziri ni kwenye kuongeza upanuzi wa miradi. Hii miradi ambayo nimeitaja hapa kumi na tano ni miradi minne tu ambayo itafanyiwa usambazaji. Niombe sana hii miradi iongezewe fedha ili tuweze kufanya upanuzi hata yale maeneo mengine ambayo hayajafikiwa tunaweza tukayafikia kwa kufanya upanuzi, kwa maana ya kuweka mtandao wa bomba kwenye maeneo ambayo hayana maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, kuna vijiji ambavyo tumeomba kwa Next budget vijiji ambavyo vinashinda kubwa sana ya maji na havina mradi wowote kijiji cha Semfuru, Ndugwira, Ikiu, Kibaoni na kule Mukulu Mheshimiwa Waziri ulifika siku ile ulivyokuja tuliwaahidi wananchi na walifurahi sana. Kwanza ujio wako pale ulipokuja walifurahi na ulivyowaahidi maji kwakweli walifurahi zaidi. Sasa wameendelea kunikumbusha Bwana Mheshimiwa Waziri alituahidi kisima hapa vipi? Kwa hiyo, sasa niwasilishe tena ombi hili kwako Mheshimiwa Waziri angalau basi nawao wapate maji yale siku ukienda sasa tuyanywe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kuwasilisha hili lakini pia kwenye maeneo kuna miradi ambayo tayari inafanya kazi mathalani mradi wa maji pale mji mdogo wa Ilongero ambao ndiyo makao makuu ya halmashauri. Ule mradi ni wa muda mrefu unachanzo cha uhakika cha maji, lakini shida ni maji yale yapo maeneo machache hata maeneo ya karibu tu hayapati maji. Kwa hiyo, niombe tufanye upanuzi kwa kuongeza miundo mbinu kama vile kujenga matanki pamoja na mabomba ili wananchi wapate maji ipasavyo. Pale vilevile kuna watumishi wa Serikali wanakwenda makazini asubuhi wanarudi wamechoka wanahitaji wapate maji salama na yakutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe sana mradi huu wa Ilongero pamoja na ule wa Mji mdogo wa Ngamu ifanyiwe upanuzi wa kutosha ili wananchi wengi wapate maji; kwa sababu pengine inaweza ikatupunguzia hata adha ya kuhangaika kuchimba visima vipya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine niombe pia, kwenye hizi jumuiya za watumia maji kuna shida moja ambayo naiona, kwamba hawa wananchi wale wakata risiti wale wanatumia zile risiti za mkono stakabadhi ni vyema wangekuwa na zile EFD Machines ambazo kwanza zitaepusha upotevu wa fedha lakini pia zitasaidia hata kufuatilia mapato yanayopatikana ambapo wakati mwingine miradi hii inaharibika tunashindwa kuikarabati. Kwa hiyo, niombe sasa ni vyema watu hawa wapatiwe EFD machine kwaajili ya kuhakikisha tunadhibiti mapato yanayopatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya mimi niwasilishe sana taarifa yangu hii lakini niendelee kuiomba Wizara kuhakikisha kwamba hii miradi ambayo wameahidi kututekelezea mwaka huu ichimbwe kwa wakati na fedha zije kwa wakati ili next time nikija hapa Mheshimiwa Waziri tuwe tunapongezana tu si kulalamika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya nishukuru sana, niwasilishe hotuba yangu. Ahsante.

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Ramadhani Ighondo Abeid.

MHE. ABEID R. IGHONDO: Naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)