Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

Hon. Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nampongeza Mheshimiwa Rais wangu mpendwa Mama Samia Suluhu kwa kazi nzuri alizozifanya, Mwenyezi Mungu ambariki sana.

Pili nampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi nzuri anazozifanya Mwenyezi Mungu ambariki sana. Tatu nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Maji pamoja na Naibu Waziri na cabnet yake, wanafanya kazi nzuri. Mheshimiwa Aweso unafanya kazi nzuri mwanangu, Mungu akubariki.

Mheshimiwa mwenyekiti, tunamuona Mheshimiwa Waziri anazunguka nchi nzima kukagua miradi ya maendeleo; Mungu ambariki sana pamoja na Naibu Waziri. Nawapongeza Mawaziri wa Wizara pamoja na Naibu Mawaziri, wanafanya kazi nzuri, wanazunguka nchi nzima kukagua miradi ya maendeleo, Mungu awabariki sana. Nampongeza sana Meneja wetu wa Maji wa Mkoa, Mariam, kwa kazi nzuri anazozifanya, Mungu ambariki sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nianze kuchangia. Namshukuru Mheshimiwa Rais kwa kutupatia milioni 400 kwa ajili ya Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Mkoa wa Simiyu katika Wilaya za Busega, Bariadi, Itilima, Maswa pamoja na Meatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, waziri tayari ameshasema, bilioni 400 zimeshapatikana. Mheshimiwa Rais ana dhamira ya dhati ya kumtua mama ndoo kichwani. Na Mheshimiwa Waziri amesema kwamba pesa, hizo bilioni 400 zimepatikana 400, ila bado wanatafuta mkandarasi. Niiombe Serikali yangu sikivu ya Chama Cha Mapinduzi mkandarasi apatikane haraka ili wananchi wa Mkoa wa Simiyu tuweze kupata maji ya Ziwa Victoria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanachi wa Mkoa wa Simiyu ni wakulima wazuri, maji yale yakifika tutalima kilimo cha umwagiliaji kwa mazao ya mbogamboga, mazao ya biashara na mazao ya chakula. Sasa, tukipata mazao ya chakula tuta-supply hata mikoa ya Jirani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Sera ya Serikali ni kuwa na uwanja wa ndege kila mkoa kwa maana hiyo na Mkoa wa Simiyu tutapata uwanja wa ndege na eneo tumeshatenga. Kwa hiyo tutalima mbogomboga, cabage biringanya pilipili hoho nyanya tutasafirisha na kuuza nchi za nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Simiyu ni miongoni mwa mikoa tisa iliyo hatarini kukumbwa na janga. Kama tutapata Maji ya Ziwa Victoria yatatusaidia sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Simiyu ni mkoa wa wafugaji, tuna ng’ombe milioni mbili tuna mbuzi zaidi ya milioni nne tuna Kondoo zaidi ya milioni tatu, tuna bata na kuku pia. Wanyama wote hao wanahitaji maji; na maji ni uhai. Wanyama hawa wakipata maji watazaliana lakini vilevile na wafugaji watapata utajiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeza Serikali kwa Wilaya ya Meatu Kata ya Mwanuzi ambayo ilikuwa na shida sana ya maji, ilikuwa inakunywa maji ya tope, maji meusi ambayo yalikuwa yamechanganyika na tope lakini. Sasa hivi Serikali imejitahidi toka mradi ule ukamilike sasa hivi maji ya Meatu ni mazuri na ni meupe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la maji Meatu kukatikatika linasababishwa na kukatikatika kwa umeme. Ombi kubwa kwa Mkoa wa Simiyu kitu tunachokiomba Serikali itusaidie ni kutujengea kituo kile cha kupoza umeme ambacho kitasaidia sana. Vilevile miradi yote iliyoko sasa hivi Wilaya ya Meatu inayoendelea ikikamilika Wilaya ya Meatu itapunguza shida za maji kwa sababu itafikia asilimia 84.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali kwa mradi wa maji unaotoka Lamadi kwenda Mkula mradi huu umesaidia sana umegharibu bilioni mbili. Niiombe Serikali yangu sikivu, kuna vijiji viwili vimebaki kupitiwa na huo mradi ambavyo ni; Kijiji cha Chabutwa na Kijiji cha Mwanale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu, kuna Kata ya Nyaluande vijiji vyote vitatu havijapata maji. Vijiji hivyo ni Nyaluande yenyewe Mwagindi na Mwamkale. Pia Kata ya Igalukiro ina changamoto kubwa ya maji Kijiji cha Runala na Mwamagigisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea kuiomba Serikali yangu Sikivu, Wilaya ya Bariadi Kata za Sima, Gudui na Isanga kuna shida sana ya maji. Naomba Serikali ibaini mitaa yenye shida sana ya maji ili iweze kutupatia maji. Lakini vilevile naendelea kuipongeza Serikali kwa ajili ya Wilaya ya Itilima ambako tuna miradi mingi inayoendelea iliyokamilika. Hata hivyo, kuna Kata ya Kinamweri ina tatizo sana la maji. Naiomba Serikali itusaidie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie hapa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante, muda wako umekwisha Mheshimiwa.

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.