Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Rais na Makamu wake kwa kuchaguliwa kwao na kazi nzuri wanazozifanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ninampongeza Naibu Spika, kwa ujasiri wake wa kuongoza vikao vyetu ndani ya Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa hotuba yake nzuri yenye mipango yake ya utekelezaji kwa kipindi hiki cha mwaka 2016/2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee chombo chetu cha habari TBC. Hatuna namna yoyote ya kutosaidia kukihudumia chombo hiki kama Serikali, ni chombo cha Serikali kinachotoa habari za ukweli na uhakika. Isingekuwa vizuri kuona chombo hiki kinashindwa kufanya kazi zake kama ilivyokusudia kwa kukosa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, chombo hiki kinasaidia sana kuitangaza nchi yetu kisiasa, kiutamaduni, kimichezo na mambo mbalimbali ya nchi yetu. Ninaomba Serikali kukisaidia kwa kukipa fedha tena kwa wakati ili katika mambo yanayoendelea katika nchi yetu wananchi wetu wapate kujua taarifa za ukweli na uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona ubadhirifu na uvunjwaji wa amani unatokea kwa sababu wananchi wamepata taarifa zisizo sahihi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja asilimia mia moja.