Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa chombo cha habari ni muhimu sana katika kuhabarisha jamii masuala ya kiuchumi, kisiasa, kisayansi na kijamii naiomba Serikali kusimamia haki za wanahabari, hasa katika kuangaliwa upya maslahi ya wafanyakazi. Serikali iangalie kutoa msaada wa kuwasomesha waandishi wa habari ili kupata wanahabari ambao ni wataalamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa utamaduni ni sehemu ya maisha ya binadamu naiomba Serikali izidi kuboresha utamaduni wetu wa Afrika.
Tunakoelekea utamaduni wetu unaelekea kupotea kwa sababu tumeanza kuiga utamaduni wa Ulaya, kwa mfano mavazi, muziki na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sanaa. Tanzania ni nchi ambayo inatambulika dunia kwa sababu ya kudumisha sanaa katika nchi yetu. Ukienda Ulaya utakuta sanaa ambazo zimetoka Tanzania, kwa mfano vinyago, vikapu, mikeka, shanga zilizotengenezwa na kabila la Kimasai. Naiomba Serikali kuangalia jinsi ya kudumisha na kuboresha sanaa ya nchi yetu hasa kuwaongezea mitaji watu wanaoshughulika na masuala ya sanaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, michezo ni sehemu ya kudumisha afya zetu, pia michezo inaongeza Pato la Taifa. Michezo inaleta ajira kwa vijana wetu. Naomba kujua Serikali ina mpango gani wa kudumisha michezo katika ngazi za Vijiji, Kata, Wilaya, Mikoa hadi Taifa, hasa mchezo wa mpira wa miguu na wa pete.
Mheshimiwa Mwenyekiti, waimbaji wetu wanaibiwa sana nyimbo zao, je, sasa Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha kuwa hawa wasanii wetu hawaibiwi CD, DVD zao? Naunga mkono hoja