Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Spika, naipongeza Wizara kwa jitihada kubwa inazofanya kunyanyua sekta ya elimu Tanzania, madarasa ya kutosha na hii imepunguza changamoto za madarasa kwa mkoa wetu wa Shinyanga, imepunguza umbali wa wototo wetu kufata elimu. Wizara inapaswa pia kuweka mkazo katika suala la vyumba maalum vya watoto wa kike maana mtoto wa kike anakosa masomo kipindi anachokuwa katika siku zake kuanzia siku tano hadi saba na hii kumfanya akose masomo kwa siku 50 kwa mwaka na hii inafanya kupunguza ufaulu kwa mtoto wa kike. Serikali inapsawa kutoa pads bure kwa ajili kujisitiri na hii itaongeza ufaulu sana kwa watoto wa kike, vyumba hivi maalumu kwa ajili ya kujibadilishia ni muhimu sana kwa mabinti wa kike.