Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, napenda kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri na jitihada nzuri inayoendelea kufanyika kwa ajili ya kuiboresha elimu yetu chini ya usimamizi mzuri wa Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu, mfano mzuri ni madarasa tuliyoyanayo kwa sasa na hakuna tena second selections.

Mheshimiwa Spika, elimu ni ujuzi na kujua kusoma ni muhimu, hivyo mimi niiombe Serikali ijikite kwenye kufudisha ujuzi kwa mtoto kwa vitendo zaidi kuliko masomo ya darasani mfano mtoto aangaliwe kwenye miaka minne ya mwanzo pale anapoanza shule kwa walimu wetu wenye utaalaam watawajua vijana hawa wanataka kufanya nini hapo baadae basi miaka mitatu ya kufikia darasa la saba waweze kupelekwa kwenye shule ambazo Serikali itakuwa imezitengeneza kwa ajili ya elimu ya ujuzi husika kwa mtoto kwani tutamjenga kijana kuweza kujiajiri au kuajiriwa.

Mheshimiwa Spika, niishauri Serikali kuanzia sasa tuangalie ni jinsi gani tunaweza kuzitenganisha hizi shule za sekondari kulingana na vipaji vya wanafunzi badala ya kusoma masomo yote kwa miaka minne basi wasome ujuzi wanaotegemea kujiajiri au kuajiriwa na hii itapunguza sana upungufu wa ajira kwenye Serikali yetu kwani wengi watajiajiri.

VETA ni muhimu sana lakini vijana wanajiunga baada ya kujiona hawakufanya vizuri miaka minne ya sekondari. Niiombe Serikali yangu sikivu iliangalie hili jambo kwa umakini zaidi.