Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakupongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri unayoendelea kuifanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kuhusu TBC Taifa na TBC FM. Hali ya usikivu wa redio hii katika Jimbo la Njombe Mjini ni adimu kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumbukumbu zangu sijawahi kusikia hata siku moja redio hii ya Taifa ikisikika ndani ya Njombe. Kwa mara ya mwisho niliwahi kusikia iliyokuwa Idhaa ya Biashara ya RTD miaka ya 1980, baada ya hapo sijawahi kusikia tena RTD wala TBC Taifa au TBC FM.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niombe Shirika la Utangazaji la Taifa liweze kufunga vifaa vinavyoweza kuifanya TBC isikike Njombe Mjini na viunga vyake ikiwemo kuweka angalau studio ndogo ili habari za Njombe ziweze kusikika, pia kuwafanya Wananjombe wanufaike na matunda ya maendeleo ya nchi yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutokusikika kwa TBC FM Njombe tunaifanya Njombe isipate habari za uhakika na kuwafanya Wananjombe watengwe na Watanzania wenzao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, redio hii inaendeshwa na kodi za Watanzania wote hivyo Njombe ni haki yetu kupata taarifa kutoka chombo hiki cha Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kukusihi tupate usikivu wa TBC FM Njombe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.