Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa nafasi hii ya kuchangia bajeti ya Wizara ya Elimu. Kwanza kabisa napenda kuunga mkono hoja ya bajeti hii, lakini pia nitumie fursa hii kuipongeza sana Wizara ya Elimu. Wizara hii inafanya kazi kubwa na kwa wale wanaofuatilia kuna mabadiliko makubwa yanaendelea katika utendaji ndani ya Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka wa jana nimepata fursa ya kutembelea baadhi ya Ofisi za Wadhibiti Ubora katika jimbo langu pia na hapa Dodoma. Wanafanya kazi nzuri sana, rai yangu waongezewe vitendea kazi, magari pamoja na fedha za kutosha. Pia nimepata nafasi ya kutembelea mara kadhaa Ofisi ya Kamishna wa Elimu, wanafanya kazi nzuri sana sana, waongezewe kile kinachohitajika kwa maana ya fedha na vitendea kazi vingine wanaweza wakasaidia Taifa hili kufika mahali pazuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, nimpongeze sana Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa leadership commitment kubwa ambayo ameiweka katika elimu. Nimefanya assessment ndogo kwa haraka, toka Rais wetu ameingia nimeona ameweka sana vipaumbele vikubwa viwili; elimu pamoja na uchumi. Toka Rais ameingia katika hotuba yake alijibainisha wazi anataka kuona mitaala inafanyiwa mabadiliko na akawa ametoa rai mitaala hii i- shift kutoka kuwa knowledge based kuwa competence based. Kwa hiyo hili ni jambo kubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia wananchi wetu katika majimbo tunayotoka karibu kila mtu hapa amesema anahitaji Chuo cha VETA. Kule Serengeti ili wananchi waweze kupongeza juhudi za Rais hizi ambazo zimekuwepo katika ujenzi wa madarasa wanahitaji sasa kuona pia wanafunzi hao wengi wanaomaliza wanaingia na kusoma kozi za ufundi ili waweze kujiajiri.

Kwa hiyo, nimwombe Waziri wa Elimu waendelee kukamilisha mipango ile ambayo wamekuwa nayo ya kuona sasa kuwa Chuo cha VETA kinajengwa katika Jimbo la Serengeti na wananchi wale waweze kupata elimu ya kuweza kuwasaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika Mkoa wa Mara pale Butiama kuna Chuo cha Mwalimu Nyerere, Chuo cha Kilimo cha Mwalimu ambacho kitakuwa na branches moja ya branch itakuwa katika Jimbo la Serengeti. Eneo lile Mheshimiwa Waziri lipo na mpaka leo wananchi kila siku wanauliza mbona hakuna kinachoendelea? Kwa hiyo niwaombe sana ile mipango ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere, sasa uingizwe katika utekelezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kuishauri wizara hii katika eneo la mitaala. Tumeona sasa kila mmoja wetu anaona hakuna uwezekano wa nchi hii kuendelea kuahidi kwamba kila anayemaliza university ataajiriwa na Serikali, haiwezekani ukienda Amerika na ukienda sehemu yo yote ile haiwezekani. Profesa Golan Hiden alifanya kazi katika nchi ya Kenya na Tanzania, amefanya kazi University of Nairobi na University of Dar es Salaam.

Katika machapisho yake kadhaa, alibainisha tofauti kubwa aliyoiona kwa nini Kenya ilikuwa ikiendelea kwa kasi ukilinganisha na Tanzania, aliona tofauti kubwa ni elimu; lakini bado alibainisha vitu hapa ambavyo ningeiomba Wizara hii ijifunze.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tunazungumzia mitaala, tunaanza kutengeneza mitaala, lakini nikiangalia pale kuna shida kubwa ambayo bado hawajai-address, elimu yetu tumeendelea kukazania mtu tu apate division one, division two, it’s okay watu washinde katika mitihani. Hata hivyo, nina uhakika na tunaona, leo tuna watu wana division one wana first class, lakini hawajiamini, hawawezi kuthubutu, hawawezi kufikiri na kuja na ubunifu. Kwa hiyo, kuna shida kubwa hapa, ni lazima hii mitaala sasa ambayo tuna-focus kuwa nayo lazima tutafute masomo yatakayowajengea vijana wetu uwezo wa kuwa wabunifu, uwezo wa kujiamini, uwezo wa ku-take risk na uwezo wa kufikiri vizuri mahali walipo na mahali pa kazi. Ndio maana sasa umeona sisi hatuwezi kushindana sana, ni kwa sababu vitu hivi vinapungua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo naamini na baadhi ya Walimu wetu wanaotufundisha ujasiriamali ukiwafukuza kwenye kazi hizo hawawezi kufanya chochote. Sasa hii ni kwa sababu hawa ambao wanafundisha mambo haya hata hawaja-practice hawawezi ku-take risk, hawawezi kufikiri kitu kipya, kwa hiyo niombe sana hili lifanyiwe kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho nichangie katika mikopo. Mikopo inayotolewa katika elimu ya juu, sasa inaendelea kuleta manung’uniko makubwa miongoni mwa wananchi, imeanza kuona baadhi ya watu wanapendelewa, wengine wanapata mikopo na, wengine hawapati. Tumekuwa na vijana wengi mwaka jana hawakupata mikopo. Sasa leo tunaimba kwamba Taifa hili Watanzania waweze kuwa na patriotism. Patriotism haiwezi kuwepo kama mtu anaona Taifa halitendi kitu fulani ambacho anakitarajia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu kwa Mheshimiwa Waziri, tuangalie kila inavyowezekana, tuone wapi tunaweza tukapunguza, vijana wote wanaoomba mikopo waweze kupewa. Kule katika elimu ya msingi na sekondari tuangalie vitu vinavyowezekana tukavipunguza ili twende kuwapatia vijana hawa mikopo wote wanaoomba.

Mheshimiwa Naibu Spika, vigezo vinavyotolewa vingi havioneshi uhalisia na ukweli wa hali ya maisha ya wananchi wetu na sababu za kuweza kuwanyima mikopo. Kwa hiyo, tuombe tuchukue shule ya msingi, vijana wanaaomaliza elimu ya msingi, baadhi wanapobaki hawawezi kufanya kitu chochote. Investment kubwa ya fedha inayopelekwa kwenye elimu ya msingi na sekondari haimpi mtu ujuzi, lakini tunapeleka fedha nyingi sana huko na hawa vijana ambao wanashindwa kusoma, kama leo tumefikiri kwamba Watanzania hawawezi kujilipia elimu ya msingi, tunawezaje kufikiri kwamba Watanzania wanaweza wakajilipia elimu ya University, ambayo ni fedha nyingi sana. Kwa hiyo, niombe sana jambo hili kwa mwaka huu tuone vijana wetu karibu wote wanapewa mikopo ya elimu ya juu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. (Makofi)