Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kushukuru. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa zawadi ya uhai lakini pia niwapongeze Wizara na Mawaziri kwa presentation nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze hotuba yangu kwa kujielekeza hasa hasa kwenye uandaaji wa wanafunzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, elimu ni dhana pana sana na ni ndoto ya kila mtoto anapozaliwa na ni hitaji lakini pia elimu ni huduma. Tunapozungumzia suala la elimu linaanzia hasa hasa kumuandaa mwanafunzi akiwa ngazi ya awali. Lakini mfumo wetu wa elimu wa Tanzania hauanzi kumuandaa huyu kijana akiwa kwenye ngazi ya awali. Tunajua mtoto yoyote anapozaliwa huwa ana carrier yake, na hizi carrier zinatakiwa ziwe developed, lakini sisi hatufanyi hayo. Na kwa sababu dunia ya sasa hivi na Tanzania tupo kwenye mchakato wa kubadili mitaala; ninaomba sana na nisisitize, tuanze kuandaa hii Mitaala yetu kwa kuangalia hizi carriers za hawa watoto wetu ili kuwaendeleza kulingana na kile ambacho wanatamani wao kukifanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii mtoto anatamani asome hivi lakini Mtaala wa Elimu una-force asome hivi. Matokeo yake tunamrundikia masomo mengi, vitu vingi ambavyo hatimaye siku haviendi kuwa msaada kwa huyu mtoto. Leo mtoto anasoma yale yale aliyosoma Mheshimiwa Gulamali, anasoma historia, kwamba nyani alikuwa anabadilika na kuwa binaadamu. Sasa hayo mabadiliko ya kuwa binaadamu kwa nini mpaka leo yasiwepo. Kumbe kuna vitu ambavyo vimepitwa na wakati kwa sasa hatutakiwi tuviendeleze.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo niwaombe sana, ili elimu iwe bora ni lazima huyu mtoto aandaliwe kwa kuangalia carrier yake iko vipi. Nchi za wenzetu zinaendelea kielimu ni kwa sababu tu watoto wao wanawaandaa kwa kuangalia carrier zao.

Leo mimi Rehema ni Mwalimu nilikuwa nina element za ualimu tangu nikiwa mdogo, hatimaye nikawa naendelezwa. Lakini leo hii elimu yetu inayotolewa inamlazimisha tu huyu mtoto asome kile kitu ambacho Serikali na Wizara inataka, kwa hiyo niombe nifanye huo mpango. Lakini tuhakikishe tunaandaa walimu wakuweza ku-impart hizi studies.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo jingine ni kwenye utunzi wa mitihani ya mwisho na usahishaji. Nchi yetu ya Tanzania tumeona a big success kwa elimu yetu ni kufanya mtihani au kumpima huyu mtu eti kwa kufanya mtihani ndipo tunapima achievement yake. Lakini hii achievement au hii mitihani ni lazima nayo sasa tuifanyie reformation tuone namna gani mitihani inatungwa lakini namna gani hii Mitihani inasahishwa. Tumeona sasa hivi mitihani the way inavyotungwa haitamsaidia huyu mwanafunzi kuweza kuyatumia yale maarifa aliyoyapata.

Mheshimiwa Naibu Spika, niliongea Bunge lililopita, leo mtihani wa shule ya msingi wa darasa la saba, mtoto unamtungia wa multiple choices, swali la kwanza mpaka la 50 multiple choices; hauoni kama unamsaidia huyu mtoto ku-guess majibu? Na unakuta kuna watoto wengine wana bahati sana anafanya ana ana ana doo; pale anapogusa tu jibu na kweli inakuwa jibu sahihi. Matokeo yake tunakuja kupata wanafunzi waliofaulu ambao hawajui kitu na wanakwenda sekondari. Tunawapa shida sana walimu wa sekondari. Mwanafunzi hajui kusoma wala kuandika vizuri. Halafu bado hata mitihani yenyewe anafanya tu shading.

Mheshimiwa Naibu Spika, kufanya shading ni jambo la kawaida, lakini kwa sababu tunataka tuwapunguzie Wizara suala la usahishaji tunalenga kuwapima hawa watoto maarifa waliyoyapata na siyo kuwapunguzia mzigo wasahishaji au Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa nimeona kwenye taarifa ya Waziri, inasema wanakwenda kusahihisha mitihani kidijitali, ina maana huyu mtu awe amejibu majibu kulingana na ninyi mlivyotunga mtihani. Sasa hapo nataka nifahamu; na hata huu mtihani nao utakuwa multiple choice mwanzo mwisho, kwa sababu kama atakuwa na maelezo yake binafsi yakienda tofauti na ninyi hamuoni kama mtaenda kutuletea shida kwenye matokeo?

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe sana, huu utungaji wa mitihani na usahihishaji tuuangalie upya, uende kupima zile study zote ambazo tunatarajia tuzipate au mwanafunzi azipate na si tu kufaulu mtihani.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni uendeshaji wa shule binafsi. Shule binafsi ni wadau wazuri sana wa elimu, wanatoa elimu sana wanaisaidia Serikali katika kutoa elimu kwa watoto wetu. Tunajua kwamba wanachukua wanafunzi wakiwa cream, wazuri sana, lakini hatimaye kuna baadhi ya manyanyaso wanayapata sana wazazi na wanafunzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwanafunzi leo wanamchukua akiwa mzuri lakini anapokaribia kwenye mwaka wa mtihani, kwa sababu alikuwa na matokeo mabaya wanamwambia ahame. Sasa, tangu mwanzo huyu mtoto mlimpokea akiwa mzuri lakini kwa sababu hamtaki kuharibu soko la biashara zenu mnaamua mumtoe; na bado tena huyo mtoto akitaka kurudi Serikalini anawekewa mizengwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe sana huko kwenye shule za private, kwamba pamoja na udau wao mzuri wa elimu nao waangaliwe upya, na wasilete manyanyaso. Lakini bado Serikalini mtoto anapokwama labda mzazi kakwamba mtoto arudi akasome kwenye shule hiyo hiyo ya kwetu ya Kayumba kwa nini tena anakataliwa? Ile ni haki yake ya kupata elimu bila kuangalia uwezo wa mzazi au nini.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala lingine ni kwenye maslahi ya walimu. Hatuwezi kuwa tunaboresha elimu bila kumboresha na huyu mwalimu ambaye anaitoa hiyo elimu. Walimu wana mahitaji makubwa sana na wanafanya kazi katika mazingira magumu. Mwalimu leo anafundisha na anakuwa na madaftari anayosahihsha mpaka yanamzidi; ilhali mazingira yake ya kufundishia ni magumu mno. Niiombe sasa Serikali kumpunguzia… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)