Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, nami pia kwa niaba ya wananchi wangu wa Vunjo nianze kwa kutoa shukrani kwa Mheshimiwa Rais kwa madarasa aliyotupa pamoja na shule ya sekondari ambayo ametuwezesha kujenga pale Himo eneo la Njia Panda.

Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Elimu pamoja na timu yake; Naibu Waziri, Katibu Mkuu pamoja na viongozi wote wa Wizara kwa kazi nzuri wanayoifanya, na zaidi kwa kuisoma vizuri dira ya Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuhusiana na mwelekeo wa elimu unaohitajika katika kipindi kijacho; na kuanzia sasa kwamba elimu ilenge zaidi kuwapa wanafunzi maarifa ya kiufundi, ujuzi wa kutenda na stadi mbalimbali. Ninaamini kwamba wameisoma vizuri dira hiyo na ndiyo sababu wamekuja na hili ambalo sasa tunalizungumza la kubadilisha mitaala ya elimu yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme hivi, tatizo kubwa litakaolojitokeza ni walimu wa ufundi na walimu wa stadi mbalimbali. Stadi zimebadilika sana. Stadi zinazohitajika sasa hivi siyo zile za zamani zinazoendeshwa na VETA za magari ya zamani. Sasa magari yaliyoingia ni ya kidijitali, yako computerized. Ndiyo sababu unaona magari mengi yanatengenezwa kwenye garage za Wachina na wanatengeneza kwa fedha nyingi. Huwezi kuona vijana wetu wakipata stadi hizo za kuanzisha garage za kisasa ambazo ni za stadi ambazo zinahitajika sasa hivi kwa sababu magari ya sasa hivi ni tofauti.

Mheshimiwa Naibu Spika, mara nyingi tunafikiria kwamba ufundi na maarifa ni kwenye mambo ya kujenga, kushona, useremala na kadhalika, lakini mimi nataka niseme kwamba sasa hivi tulenge zaidi sekta ya huduma; kutoa mafunzo ya maarifa kwenye sekta ya huduma kwa sababu ndiko dunia inapokwenda na ndiko kwenye tija na ndiko ajira inazidi kuongezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama sijaonyesha kwa nini nimesema hivyo, nataka niseme hivi, katika kipindi cha nyuma wakati tukisoma, tofauti iliyokuwepo ni kwamba unapofika Darasa la Kumi na Mbili (Form Four) kunakuwa na Careers Masters na Walimu wanakaa wanamwangalia kila mwanafunzi, wanamshauri kwamba wewe sasa tunaona uko vizuri sana kwenye hesabu, au uko vizuri kwenye biology, au uko katikati au uko chini sana. Kwa hiyo, inapofika wakati wa mwisho, unaletewa fomu ya kuchagua na mwalimu anakuwa ameshakushauri kwamba wewe unaweza kwenda mbele au huendi. Ukienda mbele hutafika mbali kwa sababu anajua wewe ni mtu una talent ya namna hii na hii. Kwa hiyo, unapoletewa unaambiwa chagua, kuna vyuo vilivyokuwepo Technical School, kulikuwa na vyuo vya maarifa kulikuwa na vyuo mbalimbali ambavyo vinaorodheshwa, pia pamoja na University.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mtu anapewa fomu ambayo anachagua kwamba baada ya kupata ushauri na mwalimu wake, kwamba wewe lini unataka kwenda kusoma mambo ya magari? Unataka kusoma mambo ya Fitter and Turner nataka kusoma hiki na kile. Kwa hiyo, kunakuwa na michepuo kuanzia hapo hapo kwenye kidato hicho ambacho kwetu sisi ni Form Four itakuwa hata na Form Six, pia mnapewa uchaguzi ule. Hiyo michepuo ndiyo inakuwa mikondo mbalimbali ya kutunza talent. Kuna watu wengine wanapenda kwenda kusoma music, kungekuwa na Chuo cha Music, kungekuwa na hiki na kile.

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati mbaya baada ya kuvunja hiyo taratibu tukasema tunaingiza sijui kitu gani au mfumo gani? Hatukuendeleza hivi vyuo vya ufundi na maarifa, tukabakia tu tunakimbizana na university na colleges zikabadilishwa zikawa ni vyuo. Kwa hiyo, ikawa sasa mtu hapewi namna ya kuchagua kwamba sasa nimefikia mahali ambapo ni lazima nichague niende huku na michepuo ile inakupeleka kwenye kujifunza stadi, kujifunza ufundi na ujuzi mbalimbali ambao baadaye unakuja kusaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa hii mitaala tunayounda, nami nakubalina na mwenzangu mmoja natumaini ni Mheshimiwa Kingu, alisema jana kwamba Waziri awe na Baraza la Ushauri liwe linamwezesha kujua kwamba atabadilisha namna gani hiyo mitaala badala ya kuleta mambo ya siasa kwenye mitaala. Mitaala siyo siasa. Hii ipo, inajulikana duniani, kuna system ya UK, kuna British System, kuna American System na kadhalika, lakini mitaala hiyo siyo kitu cha kuweza kuibua, ni kwamba ni kuchagua twende na kipi na tukizingatie, lakini kuwe na watalamu ambao ni baraza. Hilo alikuwa analisema Mheshimiwa Kingu jana kwamba liwe linamshauri Waziri na Waziri analeta hapa kitu ambacho kimekaa sawasawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi hiyo ninaiunga mkono, lakini niseme hivi tuangalie tunaenda wapi, tunapoenda ni tofauti kabisa. Hebu tuone kwa mfano uchumi wa France na US mwaka 1,800 kilimo ilikuwa inaajiri watu asilimia 64, 1,900 kilimo kiliajiri watu asilimia 43 tu, 1,950 kilimo kiliajiri watu asilimia 32 na mwaka huu inaajiri asilimia tatu ya watu walioajiriwa. Ukienda kwenye manufacturing France ilikuwa 1,800 manufacturing iliajiri watu asilimia 22, 1900, 29 imeongezeka, 1950 manufacturing ilikuwa asilimia 33, lakini sasa hivi asilimia 20 tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Huduma (Services) 1,800 ilikuwa imeajiri asilimia 14, 1,900 asilimia 28, 1,950 asilimia 35 sasa hivi 76. Asilimia ya watu walioajiriwa kwenye nchii hizi ni kwenye Services. Ukiangalia kwenye matangazo ni hivyo hivyo ilishuka, services ilikuwa 13 percent 1800, sasa hivi ni asilimia 80; watu wote wapo kwenye services. Na services utakuta kwamba kwenye health and education 20 percent, kwenye hotels and restaurants na leisure na culture na haya mambo ya muziki 20 percent. Consulting, Accounting, Design, na kadhalika pamoja na financial services inachukua another 20 percent na kwenye Government Administration na Security pamoja na Armed Forces ni 20 percent.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ina-add 80 percent, na utakuta kwamba mapato ya Serikali asilimia 75 yanaenda kwenye maeneo haya ya huduma hasa hizi za afya na elimu na administration.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo utakuta kwamba mahali sasa pa kulenga elimu yetu, namna gani kuwawezesha watu kuingia kwenye kutoa huduma mbalimbali, isiwe kwenye hoteli tu; kupika vizuri, design and so forth; music na kadhalika. Huko ndiko tunakotaka tulenge.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tujenge vyuo ambavyo vitatoa maarifa hayo kwa vijana wetu; watapata ajira kwa sababu ajira ndiyo inakuwa huko, huku kwingine kote productivity inaongezeka haraka sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kilimo Mheshimiwa Bashe mambo anayoyafanya pale kwenye kilimo productivity itaongezeka siku za karibuni, na tutaona kwamba ajira zinafunguka sana kutoka kule au watu wataweza kutafuta kazi mahali pengine. Na huko kwenye viwanda pia productivity itaongeza sana kwa sababu wana-digitizer wanafanya automation, kwa hiyo lazima wata-realize watu. Watu hao watakwenda wapi… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)