Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kukushukuru wewe kwa kunipa hii nafasi, lakini kipekee nichukue nafasi hii nimshukuru Profesa Mkenda, Waziri wetu wa Elimu pamoja na Naibu Waziri wa Elimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo nina hoja kubwa mbili ambazo nataka nimshauri Profesa pamoja na timu yake. Hoja yangu ya kwanza itajikita kwenye entry qualification za foreign students, naomba niongee Kiingereza; Vigezo vya kuwapata vijana wanaotoka nchi za nje kuja kusoma Tanzania. La pili nitaongelea ile foundation programme ambayo inatolewa na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze na suala la kwanza. Kwa upande wa admission ya foreign students vijana wanaotoka nje Kenya, Uganda, Zimbabwe na Malawi wanataka kuja kusoma Tanzania, bado tuna tatizo kubwa sana. Hili tatizo niseme limesababishwa na huu Mwongozo wa TCU, huu mwongozo wa TCU ambao ni third addition unasomeka end for standard and guidelines for university education Tanzania una kasoro nyingi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nizieleze. Kasoro ya kwanza, wenzetu wa Kenya mfumo wao wa elimu ni 8, 4, 3 kwa Tanzania mfumo wetu wa elimu ni 7, 4, 2, 3, miaka saba shule ya msingi, miaka minne kidato cha nne, miaka miwili kidato cha sita, miaka mitatu na kuendelea Chuo Kikuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wakenya wenyewe ni miaka nane shule ya msingi, miaka minne sekondari na kidato cha kwanza mpaka cha nne, miaka mitatu Chuo Kikuu hawana kidato cha tano, tatizo ni nini? Kijana ambaye amemaliza form four Kenya anaweza ku-accelerate kwenda kusoma Chuo Kikuu lakini ukimleta Tanzania haruhusiwi kusoma Chuo Kikuu, tuna tatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kijana ambaye ametoka kwa mfano Uganda amesoma diploma, akija huku Tanzania hawezi kwenda kusoma mpaka watu wa TCU na NACTE wamfanyie equivalence, ili aweze kusoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu ni nini hapa? Kwanza, ili vyuo vyetu viwe na international standard, hawa TCU wame-set a minimum standard of five percent enrolment ya foreign student kwenye vyuo vyetu, bila kuwa na a minimum five percent ya kuwa na idadi ya wanafunzi wanaotoka nchi za nje ndio hapo unajikuta chuo chetu labda cha Tanzania kipo 300 na ngapi, 2,000 na ngapi kidunia, hilo ni tatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maana nyingine ni kwamba, kumbe kuwa na idadi kubwa ya vijana wanaotoka nchi za nje kusoma Tanzania kunaongeza ubora wa elimu yetu na utambuzi wa elimu yetu kimataifa. Kwa maana hiyo ni kwamba tunapokuwa na vijana wengi wanatoka nchi za nje Kenya, Uganda Somalia Sudan Uingereza, wanakuja ku- improve diversity, vijana wetu watajifunza mambo mengi kutoka kwao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi kwa Tanzania idadi ya wanafunzi wa kutoka nchi za nje ni chini ya asilimia moja. hili ni tatizo kubwa sana. Kuna kitu kinaitwa education tourism, hawa vijana wakitoka Kenya, Uganda na Marekani, wakija Tanzania kusoma hawataishia kukaa UDOM tu, UDSM, SUA, au Mzumbe, watataka kutembelea mbuga zetu za Wanyama, tuna tatizo kubwa sana Profesa.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu ya pili ni kuhusu hii foundation program. Kwa NACTE na TCU wame-set standards kwamba ili uweze kusoma Chuo Kikuu, kama ulikuwa umemaliza diploma lazima uwe na a minimum at least 3.0 GPA, kwamba kama una GPA chini ya 3.0, huwezi kwenda kusoma Chuo Kikuu kwa mtu mwenye diploma . Sasa kuna double standard, wakaruhusu Open University ndio wana-offer foundation program kwa wale ambao wameshindwa kukidhi GPA ya 3.0 hili waweze ku-accelerate kusoma degree na hiyo foundation program inatolewa mwaka mmoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, vyuo vingine havijapewa ruhusu ya kutoa foundation program, ni tatizo. Natoa mfano, Chuo cha Mipango, mwanafunzi amesoma pale mambo ya mipango ya maendeleo vijijini amepata GPA ya 2.5, anatamani aendelee kusoma degree ya mambo ya maendeleo vijijini, Open University hawana degree ya mambo ya rural development planning, unamlazimisha mtoto a-change kutoka professional yake kutoka rural development planning akasome professional nyingine, hilo ni tatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tuna tatizo ambapo tuna chuo kimoja tu Tanzania ambacho kinatoa foundation program kwa wale ambao hawana vigezo vya kusoma degree ili waweze kusoma degree. Ushauri wangu ni nini? Naomba niishauri Serikali na Wizara mambo matatu. La kwanza…

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Taarifa.

T A A R I F A

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumpa taarifa mchangiaji kwamba, mwaka jana kuna vijana wetu walikuwa wanatoka Chuo Kikuu cha Kampala wakapata ajali na hawa vijana waliopata ajali ni hawa vijana ambao hawana sifa ya kujiunga kutokana na haya masharti ya TCU, lakini wanakubalika nchini Uganda. Kwa hiyo tumepoteza maisha na vijana wengine vilema kwa sababu kubwa TCU wamewakwamisha kuweza kudahiliwa katika Vyuo Vikuu vya Tanzania na matokeo yake wakaenda Uganda na kwa vile safari ni ndefu ndio wakapata usumbufu. Ahsante sana.

NAIBU SPIKA: Dkt. Chaya.

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakubali mchango na taarifa ya ndugu yangu Soud na naiunga mkono.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishauri Serikali, kabla sijaishauri Serikali mimi ni mdau wa elimu, kwa hiyo naifahamu vizuri Wizara ya Elimu. La kwanza kuhusu foundation program, naomba itolewe kwa vyuo vyote na nina sababu za msingi. Sababu ya kwanza ni kwamba kwa Open University tayari wameelemewa ku-offer foundation program kwa vijana wote ambao wana GPA ya less than 3.0, naomba Wizara iruhusu SUA watoe foundation program, Mzumbe watoe foundation program, UDOM watoe foundation program, ili tuweze kuwapa nafasi vijana wengi wenye GPA ya chini ya tatu, waweze kusoma mwaka mmoja ili wa-move kwenye degree level. Hilo la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kuhusu hizi standards tofauti tofauti za elimu, sisi ni washiriki wa East African Community, lakini ni member wa SADC, niishauri Serikali, tunahitaji ku-harmonize education framework zetu za hizi nchi. Nimesema hapa Kenya wana mfumo wao tofauti wa elimu, Uganda wana mfumo tofauti wa elimu, Sudani wana mfumo tofauti wa elimu, Rwanda vilevile, tunahitaji sisi kama East African Community Block, tuwe na mfumo mmoja ili tuhakikishe kwamba tunatumia hii fursa vizuri ya kuchukua hawa vijana kutoka katika maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, ni suala la kutambua hizi entry qualifications. Kama alivyotangulia kusema ndugu yangu Mheshimiwa Soud kama kijana aliyemaliza form four Kenya, Wakenya wanamruhusu kusoma degree ni kigezo gani tumekitumia sisi Watanzania kumkataa yule aliyemaliza form four Kenya kusoma degree Tanzania. Hivi tukilinganisha Vyuo Vya Kenya na Vyuo Vya Tanzania kwenye international standard, vyuo vipi vitakuwa kwenye hadhi ya juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba nimshauri Mheshimiwa Waziri lakini na Profesa wa TCU, wafanye utafiti wa kina ili waangalie kwa sababu hawa wanakuja kusoma Tanzania, at the end of the day wanarudi kufanya kazi kwao Kenya. Kwa hiyo sioni sababu ya kuwakataa hawa watu.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja. Ahsante. (Makofi)