Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na pongezi kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Prof. Adolf Mkenda Waziri wa Elimu, Mheshimiwa Architect Omari Juma Kipanga Naibu Waziri; Katibu Mkuu Ndugu yangu Profesa Eliamani Sedoyeka, Naibu Katibu Mkuu wa Sayansi Ndugu yangu James Mdoe, Naibu Katibu Mkuu anayeshughulika masuala ya elimu mwanamama Profesa Carolyne Nombo na wataalam wote wa Wizara ya Elimu kwa kazi nzuri wanayoifanya. Hawa nawapongeza si kwa sababu tu nawapongeza, kwa sababu baada ya Mheshimiwa Rais kutoa tamko kwamba sasa tupitie sera, mitaala kwa sasa wanachakalika wanapambana usiku na mchana kuhakikisha kwamba wanapitia sera yetu ya elimu. Wanapitia mitaala yetu ya elimu ili kuisogeza karibu na wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamekuwa na malalamiko ya muda mrefu ya elimu yetu kutokugusa maisha ya wananchi wa kawaida. Profesa Mashimba wameisema hii kwa kipindi kirefu sana. Kwa hiyo, mtoto akitolewa nyumba akipelekwa kwenye mfumo elimu anarudi ile asilia yake imeondoka lakini wameanza kuifanyia kazi kwa kasi kubwa, nawapongeza sana kwenye eneo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nitoe angalizo kwenye hatua hii ya mapitio ya sera na mitaala ambayo tunaifanya kwa sasa. Nimemsikia mara kadhaa Profesa Mkenda akisema mapito ya sera, mitaala ya elimu ni kazi ambayo imeanza kufanywa na dunia nzima, sisi tulianza mapema. Tunaomba sana tusiburuzwe na dunia sisi tulioanza mapema ile nia yetu ya awali ibaki pale pale ili tufikie elimu yetu iguse mazingira ya kwetu. Tupate elimu inayotatua changamoto tulizonazo kwenye mazingira yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yote ambayo yanafanyika dunia sasa ni Kijiji hatuyakatai lakini sisi tusimezwe na changamoto zile ambazo zipo duniani. Tuhakikishe tunatatua changamoto zetu kwanza, tunaboresha elimu yetu, tunahakikisha kwamba tunasogeza elimu tunayoitoa kwa wananchi wetu ili ukimfundisha mtu darasani akienda kwenye mazingira ya kawaida ya kuishi aweze kuitumia elimu ambayo ameipata ili iweze kumsaidia kwenye mazingira anayotoka.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa na utaratibu wa kutathmini ufaulu wetu kwa kuangalia yeyote aliyefaulu lakini ukiangalia wanaopata Daraja la Nne, wengi mno kwa nchi hii hasa kwa sasa ambao tunatoka vijijini. Vijana wale wamesoma Kidato cha Kwanza mpaka cha Nne ukilinganisha na wale ambao hata darasa la kwanza hawajaingia shughuli wanazozifanya zinafanana. Tuangalie elimu tunayotoa, itoe tofauti ya yule aliyekwenda shule na ambaye hajaenda shule ili wale waliokwenda shule wakatoe shule kwa wale ambao hawajaenda shule! Wao wawe kielelezo cha wale ambao hawajapata elimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaoishi na hao vijana, wanaofuga vijana ambao wamemaliza kidato cha nne na wale ambao hawajaingia hata darasa la kwanza mazingira ni hayo hayo, wanaolima vivyo hivyo, elimu yetu lazima itoe tofauti kati ya watu ambao wamekwenda shule na wawaelimishe wale ambao hawajapata bahati hiyo kwa sababu nafasi siyo nyingi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto nyingine tuliyonayo, waliomaliza Kidato cha Nne wamepata Daraja la Nne kwenda Sifuri, zaidi ya asilimia 65 mpaka asilimia 70, kwa sisi vijijini inaweza kuwa 75 mpaka 80! Hao tunawaacha tunawasahau historia yao inafutika baada ya kuwa wamefeli elimu ya sekondari. Kwenye imani zetu zote binadamu akiishi, ikifika siku ya kufa tunaamini kwamba baada ya muda fulani kuna jambo fulani zuri linafuata kwa Mwenyezi Mungu, ambaye hajafanya vizuri either anakwenda Jehanamu. Sisi tukimaliza tu Kidato cha Nne tumefunga hapo, tutengeneze uratatibu wa kusaidia hao vijana ili waje wasaidie Taifa lao. Tutengeneze Vyuo vya Ufundi ambavyo vitawapa ujuzi hao vijana waweze kutoa mchango stahiki kwa Taifa lao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesikiliza hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara Ndugu yangu Sedoyeka wakati Mheshimiwa Rais akiwa Mgeni Rasmi pale Arusha. Kwamba tutatanua Vyuo vya Ufundi mpaka kwenye ngazi angalau ya Tarafa. Mimi hivi ninavyoongea Jimbo la Hanang’ halina hata Chuo cha Ufundi – VETA. Tuweke nguvu kubwa kwenye eneo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nimefanya kazi mbalimbali wachina ukiuliza tu taarifa zao mtu mwenye cheti tu ana ujuzi wa kufanya mambo mbalimbali, nchi yetu tuwekeze huko kwenye elimu ya kati! tuweka nguvu kubwa huko. Lakini tuunganishe elimu yetu na mazingira yetu ya kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu yangu Mheshimiwa Waziri ulikuja mwaka 2020 Disemba pale Hanang’, wakati tukitaka kuboresha kilimo cha ngano, tukakuomba sana wakati huo ukiwa Waziri wa Kilimo, sasa Waziri wa Elimu. Kwamba ule uzalishaji wa Ngano Kituo cha Umahiri kiwe Hanang. Tuunganishe sekta zetu za uzalishaji, kilimo, ufugaji, uvuvi na elimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kile Kituo cha Umahiri tukipata Chuo Kikuu kitaendesha Kituo cha Umahiri Hanang’, tukafufua kilimo cha Ngano, tunachangamoto kubwa ya mbegu ya ngano na mbegu za mazao mbalimbali, itatusaidia sana. Tuunganishe elimu yetu na kazi tunazofanya za kilimo, ufugaji na uvuvi na mambo mengine mbalimbali ambayo tunafanya biashara ili elimu itusaidie kututoa sisi kwenye changamoto tulizonazo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kidogo suala la angalau hamasa kwa wale wanaotoa elimu. Upande wa elimu ya msingi imesemwa sana na Profesa Kitila Mkumbo. Elimu ya Sekondari ameisema lakini tukija kwenye upande wa Vyuo Vikuu ninachoomba kila mtu anayefanya vizuri tutambue mchango wake sawa sawa! Kama mtu ameleta jawabu la changamoto either ya kudhibiti upotevu wa maji tuutambue huo mchango. Maprofesa wetu wale Wahadhiri wetu wanaofundisha vyuoni tuwatengenezee utaratibu wa kutambua mchango wanaoutoa kwenye jamii yetu kwa kutatua changamoto zilizopo.

Mheshimiwa Naibu Spika, siyo sawa hata kidogo kama nimeitwa Profesa basi, haki ninazopata na Profesa yoyote ni sawa, kama mimi nimechangia zaidi utambuzi huo ufanyike. Kama mtu ameleta jawabu la suluhu ya kisiasa, kiuchumi na mambo ya kisaikolojia. (Makofi)