Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kwanza kuanza kuchangia katika Wizara hii ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Kipekee kabisa kwanza nitoe pongezi nyingi kwa Mheshimiwa Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan, hasa pale alipoweza kupata mkopo wa Trilioni 1.3. Ni kwamba, fedha zaidi ya Bilioni Mia Nane na Hamsini na kitu ambayo ni sawa na asilimia kama 75 ya fedha hizo zimekwenda kwenye huduma za jamii, kwa maana kwamba, zimekwenda kujenga madarasa, kwa maana ya sekta ya elimu, lakini vilevile fedha zimekwenda kujenga miundombinu ya sekta ya afya. Kwa hiyo, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa uamuzi wake huo mzuri wa kupeleka huduma za jamii kwa wananchi wake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nitoe pongezi kubwa sana kwa Waziri wa Wizara hii, Mheshimiwa Profesa Adolf Mkenda na Naibu wake Mheshimiwa Omari Kipanga, vilevile nimpongeze sana Katibu Mkuu wa Wizara hii, Profesa Eliamani Sedoyeka, pamoja na Makamu wake wawili ambao ni Profesa James Mdoe pamoja na Profesa Caroline Nombo, watu hawa wamekuwa waungwana sana Pamoja na Watumishi wote wa Wizara hii kwa sababu wamekuwa ni watu wasikivu na wanapokuja kwenye Kamati yetu kwa kweli tunaongea kwa kuelewanana nia yetu ni moja na njema ya kutumia wanachi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, watu hawa wamekuwa waungwana sana pamja na watumishi wote wa Wizara hii kwa sababu wamekuwa ni watu wasikivu na wanapokuja kwenye Kamati yetu kwa kweli tunaongea kwa kuelewana na nia yetu ni moja na nia ni njema ya kutumikia wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kusema kwamba, Wizara hii ni muhimu sana na ni Wizara nyeti kwa kizazi chetu cha Tanzania. Kwa hiyo niendelee kusisitiza yale malengo endelevu ya milenia ambayo yanatuelekeza angalau 20% ya fedha za bajeti ziende kwenye sekta ya elimu, hilo tulizingatie. Tukifanya hivyo at least kwa 17% tutakuwa tumeweza kutatua changamoto nyingi ambazo zipo katika sekta hii au zinazoikabili sekta hii ya elimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, niungane na Kamati na wajumbe wenzangu wa Kamati ambao kwa kweli tumefanya kazi kubwa ya kuishauri Serikali. Katika yale maoni ya Kamati ninaendelea kusisitiza kwa mambo mawili matatu; la kwanza, ni kwenye mikopo ya elimu ya juu. Mikopo ya elimu ya juu tumekuwa na tatizo kubwa malalamiko yamekuwa ni mengi sana vijana, wazazi wanalalamikia hii Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kwa sababu tumekuwa tukipata fedha, lakini fedha hizo hazitoshi kwa Watanzania wanaohitaji mikopo kwa ajili ya kwenda kujiendeleza katika elimu za juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Kamati tumeliona hili na wakati mwingine tumekuwa tunachanganyikiwa kwa sababu hatuelewi lengo kubwa lilikuwa ni nini? Lengo zuri la Serikali tunalitambua kwamba ni kuwawezesha watoto wa elimu ya juu waweze kusoma kwa kupata mikopo, lakini uchaguzi wa watoto hawa au wale ambao wanapewa kipaumbele kupewa mikopo inakuwa inachanganya, wakati mwingine inaonekana kwamba watoto yatima ndiyo wapewe mikopo, ni kweli mtoto yatima anatakiwa apewe mkopo, lakini wakati mwingine watoto yatima hao hawapati hiyo mikopo.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati mwingine tunasema kwamba wale waliofaulu vizuri masomo ya sayansi ndiyo wapewe mikopo 100%, wakati mwingine hawapati 100%, wanakomea 40% na 50%. Wakati mwingine tunasema haya basi, wapewe wale watoto ambao wanaonekana wana ufaulu mzuri kwenye masomo labda ya art na masomo mengine, bado tunaona kwamba mkanganyiko na watu wengi wameshindwa kuelewa kwamba kipaumbele cha mfuko huu ni kitu gani.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tuliwauliza Bodi ya Mikopo, hivi kwa nini tusiwape mikopo watoto wote wa Kitanzania wanaohitaji mikopo ya elimu ya juu bila kujali ufaulu, bila kujali ni mtoto yatima, so long anahitaji mkopo huyu mtu anahitaji fedha kwa ajili ya kujiendeleza apewe mikopo. Wakasema kwamba mfuko huu ni mdogo, una bilioni 400 umeongezeka mpaka sasa bilioni 500. Je, ni shilingi ngapi inahitajika ili watoto wote wapewe mikopo hiyo? Wakasema tunahitaji bilioni 800. Hivi kweli kama mikopo hii inatolewa na baada ya muda fulani inarudishwa na hii kumbe ni biashara na wanalipa na interest kwa nini tusitafute bilioni 800, mtoto yoyote anayehitaji kukopa fedha apewe mkopo aende akasome.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kwa sababu mikopo hii inalipwa mtoto atakwenda kulipa tatizo ni nini? Tatizo hapa ni kwamba ni elimu, tuwaelimishe wazazi kwamba mzazi mwenye uwezo wa kumsomesha mtoto wake elimu ya juu amsomeshe, amuondolee ile burden ya kuja kulipa mikopo baadaye, lakini yule ambaye anahitaji kwa nini anyimwe mkopo? Hivi ni nani apate mkopo na nani akose mkopo, nani aende shule nani asiende shule.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tukasema kwamba ni vizuri Bodi hii ya Mikopo kwa sababu ilianzishwa kuwawezesha Watanzania, ifanye kazi kwa mfumo wa kibenki, wapewe fedha, watoe mikopo kwa riba nafuu baada ya pale wawafuatilie waliochukua mikopo walipe taratibu na watoto wengine waende wakasome. Kwa hiyo hili ni jambo ambalo tumesisitiza katika Kamati yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile mabenki binafsi yapewe na yenyewe fursa ya kuwakopesha wanafunzi kwa riba ndogo, itafutwe incentive kwenye mabenki haya waweze kuwapa mikopo wanafunzi wakasome.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii nimesoma taarifa ya Mheshimiwa Waziri nawapongeza sana NMB Mungu awabariki, wametoa bilioni 200 kwa ajili ya kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaotaka kusoma elimu ya kati. Waendelee na moyo huo waendelee kutoa mikopo kwa sababu tumekuwa tunasisitiza hata wale wanafunzi wa elimu ya kati wanaosoma Diploma ufundi mchundo, wanaosoma haya masomo ya VETA, wanaotaka kupewa ada shilingi 800,000, shilingi 700,000 au shilingi 600,000 kwa nini wasipewe mikopo? Tunatoa kwenye elimu ya juu tu na kwa elimu ya juu tu yenyewe tunatoa mikopo, tumefuatilia tumekuta 62% ya mikopo inayotolewa inapelekwa kwa wanafunzi wanaosoma masomo ya art, wakishamaliza kusoma masomo ya art wanapokwenda kwenye soko la ajira hawapati ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kama watoto hawapati ajira 62% wametoa kwa watoto wanaosoma art, watarudisha vipi hizi fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ni vizuri kuwapatia mikopo wanafunzi wanaosoma elimu ya kati na kwa kweli Benki ya NMB imefanya jambo jema na nawaomba na mabenki mengine wajitolee, wawape mikopo wanafunzi wanaosoma elimu ya kati kwa sababu ndiyo wanaoajirika kwa haraka na ndiyo wanaopata ajira haraka na ndiyo wanaoweza kurudisha mikopo hiyo kwa haraka. Tunaomba sana hilo lifanyike.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimalizie, suala la watumishi, sekta ya elimu inahitaji Walimu, Walimu hatuna. Sasa hivi tunajenga VETA kila wilaya na nawaomba nichukue fursa hii kuomba wilaya yangu ya Maswa wanijengee VETA. Wakishajenga VETA Walimu wa kuwafundisha watoto ufundi wako wapi? Tuwe na special program ya kufundisha Walimu watakaokwenda kufundisha ufundi kwenye VETA. Walimu wanaofundisha sasa hivi wana ile teknolojia ya zamani chuma wanaunganisha kwa zile sticker wakati siku hizi kuna teknolojia mpya wafundishwe teknolojia mpya, wapewe vifaa vya kisasa, watoto hawa wafundishwe elimu ya ufundi katika shule hizi, lakini wafundishwe na Walimu walio-qualify. Tumejenga madarasa vizuri tunashukuru, tunajenga VETA tunashukuru, lakini program ya Walimu ianzishwe ili kusudi ikawafundishe vijana hawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, Vyuo Vikuu vyetu ukienda kuangalia Vyuo Vikuu tumekwenda Chuo Kikuu cha Mkwawa, kuna Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, wanafunzi wamejaa wanaosoma undergraduate simply kwa sababu wanapata mikopo ya elimu ya juu. Tumeenda Mkwawa tumekuta wanafunzi zaidi ya 8,600 wanasoma undergraduate, tukauliza wanafunzi wanaosoma Masters wako wangapi? Tukaambiwa wako 57 tu kwa nini? Hakuna wanaojiunga, kwa nini hawajiungi? They are comfortable kwa sababu wanafunzi wanakuja wana mikopo ya elimu ya juu. Wanaosoma Masters na PhD hawana mikopo sasa hawawezi kuja hawa watu kama hakuna sensitization.

Tunaomba Vyuo Vikuu viwape fursa watu wanaofanya marketing waka-market kwa watu wanaotaka kusoma Masters wajiunge katika kozi hizi ili vyuo vikuu hivi viweze kuwadahili wanafunzi wa masters na PhD.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, ahsante kwa kunipa fursa. (Makofi)