Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu ni kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kusaidia Wizara kuwa na vyuo vikuu vya uhakika ili kukuza sanaa na michezo nchini. Naomba Wizara ijikite katika kuibua vipaji kwa kuendeleza michezo shuleni ikiwa ni pamoja na kutoa motisha kwa walimu wa michezo, pia kwa wanafunzi wanaoshinda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kuwepo uhuru wa vyombo vya habari ikiwa ni pamoja na Televisheni ya Taifa kubaki ya Taifa na siyo kwa ajili ku-report taarifa za chama chochote bali itumike kama chombo huru kwa ajili ya Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kuunga mkono vyombo vya binafsi kwa mchango mkubwa vinaotoa kwa Taifa. Naishauri TBC kuongezwa mtaji ili iweze kuwafikia watu wengi katika jamii.