Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, napenda kuwashukuru na kuwapongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Waziri, Naibu Waziri na viongozi wote kwa uongozi wao na utendaji uliotukuka wa Wizara ya Mambo ya Ndani.

Mheshimiwa Spika, napenda pia kutumia fursa hii kukupongeza wewe binafsi, Naibu Spika na uongozi wote wa Bunge kwa uongozi wenu mahiri na wenye ubunifu wa hali ya juu katika kuongoza mhimili wa Bunge.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi kinachoishia mwezi Aprili, 2022 Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani imesimamia kwa uadilifu na ufanisi mkubwa masuala yote ya usalama wa raia hasa kurudisha uwabikaji kazini iliopelekea kupungua kwa uhalifu. Pia kwa kusimamia vizuri, rushwa na upendeleo umepungua kwa kiasi kikubwa kupelekea wananchi kushiriki kikamilifu shughuli za ujenzi wa Taifa.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio hayo makubwa ya ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Mbalizi kwa kushirikisha wananchi, askari bado wanaendelea kufanya kazi katika mazingira magumu kutokana na kutokuwepo kwa nyumba za askari hasa katika eneo jirani na Kituo cha Polisi. Ni vigumu sana kwa Wilaya yenye askari zaidi ya 150 na inatoa huduma kwa wakazi karibu 500,000. Kunapotokea dharura, viongozi na hata askari inakuwa vigumu kujikusanya kwa muda muafaka. Pia wananchi wameonesha nia ya kushiriki kujenga vituo vingine katika miji midogo ya Ilembo, Isuto na Igoma. Kuna uhitaji mkubwa wa kuwepo vituo vya polisi katika maeneo haya kutokana na shughuli za kichumi na pia umbali toka makao makuu ya Wilaya.

Mheshimiwa Spika, napendekeza Serikali ianze mchakato na itenge bajeti ya angalau shilingi milioni 300 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vipya vya Ilembo, Isuto na Igoma. Kwa vile wananchi wameonesha nia ya kushiriki ujenzi wa vituo vitatu vipya vya polisi, bajeti hii inayoombwa ya shilingi milioni 300 itachochea kumaliza ujenzi wa maeneo muhimu ya vituo hivi na kuwezesha motisha na ufanisi kwa askari. Pia napendekeza kuongeza magari kwa ajili ya usafiri hasa ukizingatia jiografia ya Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.