Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hoja hii katika kuonesha ni jinsi gani sanaa na michezo inaweza kuwa na mchango mkubwa kwenye Pato la Taifa. Leo hii Taifa lingehakikisha tuna viwanja vya kutosha kuanzia ngazi ya Wilaya hadi Mikoa na vyote ni vya kisasa, si tungekuza soka na michezo mingine kama ridhaa, basketball, volleyball, netball na mingine mingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, enzi zetu wakati tunasoma, michezo ilikuwa na hamasa na shule zote za msingi na sekondari zilikuwa na viwanja vya kutosha. Michezo mbalimbali ilikuwa ikichezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ni wakati sasa viwanja ambavyo vinahodhiwa na CCM virudi kwa Serikali ili viendelezwe na kuweza kuleta tija. Ni muhimu kwa sababu hivi vilijengwa enzi ya chama kimoja ambapo ni fedha za Watanzania zilitumika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kuiomba Serikali angalau watusaidie kuboresha uwanja wa Wilaya Tarime ambao upo pale Tarime Mjini, kwani umetelekezwa na kubaki kutumika kwenye mikutano ya hadhara badala ya michezo husika. Uwanja una sifa zote za kuweza kuchezwa ligi za daraja la kwanza na ukiboreshwa utasaidia sana kukuza uchumi. Hivyo, natoa rai yangu kwamba Serikali ishirikiane na Halmashauri ya Mji wa Tarime ambayo tayari wameshatenga fedha kiasi kidogo kwa ajili ya uboreshaji wa uwanja wa Serengeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni dhamira ya Halmashauri ya Mji wa Tarime kujenga shule ya michezo kwa kushirikiana na Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini. Hivyo tumeomba Serikali ione umuhimu wa sports accessory ziweze kuwepo nchi nzima na kwa wale walio tayari kama Tarime Mjini wapewe vipaumbele. Bila shule za michezo huwezi kukuza vipaji kuanzia shule za msingi hadi sekondari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, tuwekeze kwenye sanaa na wasanii wa kuigiza na kuimba nyimbo ambazo zitakuwa na tija kwao. Mfano, wanamuziki wetu wana vipaji vizuri sana lakini uhalisia wa maisha yao hayaakisi kipato ambacho Watanzania wengine wanavyopata nje ya nchi ni nyingi tofauti na wanazopata hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri tuwekeze kwenye tamaduni zetu ambazo zinaweza kuwa pia kumbukumbu ya tamaduni zetu. Siku hizi tamaduni zinapotea kabisa; ngoma za jadi zinapotea na mambo mengine ambayo yangekuwa kivutio kwa Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kifupi naomba majibu, ni jinsi gani Serikali imejipanga katika hoja hii na nyingine?