Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Spika, kabla sichangia sana nataka nitende haki kwa Wizara hii na wasimamizi wake kwa kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayofanya. Mheshimiwa Waziri Masauni kazi yako ni nzuri, umekuwa msikivu, umekuwa muungwana, Naibu Waziri Sagini wewe ni Ndugu yetu sisi watu wa Sumve, tumekuwa tukileta shida zetu mnatusikiliza na mnazitatua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba sasa nichangie kidogo katika Wizara hii hasa katika vitu viwili. Katika Jeshi letu la Polisi ambalo linafanya kazi nzuri sana chini ya usimamizi wa IGP, wanafanya kazi nzuri sana ya kutulinda, lakini sijaelewa kuna shida gani kwa muda mrefu nimekuwa shahidi wa kuona mazingira magumu sana ya Askari wetu ya kufanya kazi, hasa vituo vyao vya Polisi na nyumba zao za kuishi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Askari wetu asilimia kubwa hawana makazi yanayofanana na kazi wanayoifanya, nadhani umefika wakati sasa Serikali kupitia Wizara hii tuende na jambo la dharura la msingi la kuhakikisha Askari wetu wanapata makazi ambayo yatawafanya wafanye kazi zao vizuri. Hao Askari tunaowazungumzia ndiyo watu ambao tukisikia kuna panya road tunawafuata wao, kukiwa kuna wezi tunawauliza wao! Lakini hawa Askari ambao ndiyo wanatulinda suala la kuwatafutia makazi limekuwa likiimbwa kila siku Bungeni lakini hatua hazichukuliwi! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hao Askari tunaowazungumzia ndiyo watu ambao tukisikia kuna panya road tunawafuata wao, kukiwa kuna wezi tunawauliza wao, lakini hawa askari ambao ndiyo wanatulinda suala la kuwatafutia makazi limekuwa likiimbwa kila siku Bungeni humu, lakini hatua hazichukuliwi. Sasa nafikiri umefika wakati Serikali hatuwezi kuwa tuna jenga nyumba 20 za askari tunazungumza hapa, wakati tumejaza askari huko kwenye vituo wanatulinda. Suala la nyumba za askari liwe ni jambo la kipaumbele, watu wanatulinda, tunataka watulinde, unajua inawezekana tunachukulia poa kwa sababu askari hawana tabia ya kulalamika, wao wakikutana na sisi wanapiga saluti, basi, lakini jamani tuangalie watu kama ndugu zetu. Mazingira wanayoishi ni magumu, kwa hiyo kuna haja kabisa ya kulichukulia suala la nyumba za askari kama jambo la msingi.

Mheshimiwa Spika, magari wanayotumia, kwenye Wilaya ya Kwimba, hapa ninavyozungumza kuna gari moja tu la askari lakini nalo ni bovu; na juzi kama wiki moja imepita kulitokea ajali pale Sengerema gari la Mwanza ya Askari steering road zilichomoka tu, yaani gari ambazo hazina service, sasa hata namna tu ya kutafuta vyombo vizuri vya kufanyia kazi hawa askari wetu kweli ndugu yangu tumeshindwa. Lazima tufika wakati tuamue kuliboresha Jeshi la Polisi, tusing’ang’anie tu kuwa tunalalamika barabarani askari wanafanya nini wanafanya nini, lakini na sisi tuangalie namna ya kuboresha Jeshi la Polisi. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa kengele imeshagonga.

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)