Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi, happy new year Waheshimiwa Wabunge wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nitumie fursa hii kuwashukuru Wanambeya kwa kunirudisha tena mjengoni kwa kipindi cha pili na kunifanya niwe Mbunge niliyechaguliwa kwa kura nyingi kuliko wote humu ndani, the most voted MP kwenye election ya 2015. Kama Waziri Mkuu anatokana na Wabunge waliochaguliwa wangeangalia kura nyingi may be mimi ndiye ningekuwa Waziri Mkuu humu ndani . (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme kitu kimoja, tunapanga Mpango wa Maendeleo humu ndani au tunajadili Mipango ya Maendeleo lakini wale wanayoipokea hii Mipango ya Maendeleo sidhani hata kama tayari wako cemented katika mazingira yao. Sina uhakika hata kama tayari mmeshapewa instrument ya kazi na Rais. Rais anapochagua Baraza la Mawaziri anawapa instrument ambayo ndiyo kama job description. Sasa nina wasiwasi kama hawa walishapewa na matokeo yake ndiyo maana wanaenda hovyoovyo tu kwa kufuata mizuka ya Rais. Rais akitumbua majibu huku wao wanatafuta kule kwenda kutumbua, kinachotakiwa siyo kutumbua majipu twende tutumbue mpaka viini. (Kicheko/Makofi)
KUHUSU UTARATIBU
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utaratibu.
MWENYEKITI: Samahani Mheshimiwa Mbilinyi, Waziri wa Nchi.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utaratibu, Kanuni ya 68 pamoja na Kanuni ya 64, mambo yasiyoruhusiwa Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa msemaji aliyekuwa anaongea kwanza ametumia maneno ya kuudhi lakini ametumia maneno ya dhihaka kwa kutaja jina la Rais kwa dhihaka. Kanuni ya 64(d) inasema hatatumia jina la Rais kwa dhihaka katika mjadala kwa madhumuni ya kutaka kulishawishi Bunge kuamua jambo lolote kwa namna fulani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi haya ni maneno kweli yanayostahili heshima ya Rais kusema kwamba anaongozwa kwa mzuka? Mzuka ni kitu gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nafikiri utusaidie kutupa mwongozo wako kama maneno hayo na Kanuni ile ya 64(d) yanaweza kweli kubeba maudhui ya kulitumia jina la Mheshimiwa Rais katika mazingira tuliyonayo hapa. Kwa nini asiyaondoe maneno haya halafu achangie tu hotuba yake kwa staha na watu wote waweze kumwelewa? (Makofi)
MWENYEKITI: Mheshimiwa Joseph, kwa heshima kabisa mdogo wangu naomba ufute maneno hayo.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa tunapambana na changamoto ya generation gap, ndiyo inayomkuta Mheshimiwa Waziri. Mizuka ni neno la Kiswahili lina maana ya hamasa yaani ile amshaamsha kwamba Rais anaamshaamsha na wao kwa sababu hawajapewa job description wanaiga, huyu yuko buchani anaangalia nyama, huyu anafunga mageti, huyu naye sijui anafanya nini, hiki ndiyo kitu wanachokifanya. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnaozomeazomea niwaonye, wengi wenu waliokuwa wanazomea hawajarudi hapa. Waliorudi ni wajanja kama Dkt. Mwinyi wako kimya tu. Wanaozomeazomea wengi hawajarudi, hamtaonja term ya pili, siyo mchezo, hiyo nawaambia wazi kabisa. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, turudi kwenye mchango…
MWENYEKITI: Samahani Mheshimiwa Mbilinyi, Waziri wa Nchi.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, bado niko pale pale kwenye Kanuni ile ile na naendelea kusisitiza, Mheshimiwa Rais wetu haongozi kwa mzuka, kwa hamasa, anaongoza kwa taratibu, Katiba na sheria, haongozi kwa mzuka au eti kwa hamasa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais ana Ilani, Katiba, sheria, na taratibu anazozitumia kuongoza. Kwa hiyo, huu uongozi wa kufuata generation eti Rais anaongoza kwa mzuka, kwa hamasa, haiwezi kukubalika. Haya ni maneno ambayo yanaudhi na yanataka kudhalilisha jina la Mheshimiwa Rais ndani ya Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kauli hiyo ifutwe. (Makofi)
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbunge Mbilinyi!
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tabia imeanza kujitokeza kutaka kufanya kama Rais sijui au huyu Rais wa Awamu ya Tano untouchable, haguswi kwa kauli wala nini, lazima tutasema. Sijasema Rais anaongoza kwa mizuka, nimesema hawa ambao hawajapewa job description ndiyo wanafuata mizuka ya Rais, wanafuata vigelegele, ninyi mnafuata vigelegele. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba unipe nafasi niendelee kuchangia.
MBUNGE FULANI: Mwongozo.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Utapokea Miongozo baadaye, naomba unipe nafasi ya kuchangia. President Magufuli siyo unatouchable ni mhimili mwingine na hili Bunge litajadili bila kumkashifu na bila kumtukana pale atakapokosea, kwamba anapotumbua majipu aende mpaka kwenye viini, anafukuza watu kazi, watu hawapewi nafasi ya kujitetea, halafu tunaongea humu mnataka kusema vitu gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kupata maendeleo bila demokrasia…
MWENYEKITI: Samahani Mheshimiwa Joseph Mbilinyi, naomba unyamaze kimya kwanza. Hii hoja imetolewa na Waziri wa Nchi. Sasa naomba Mheshimiwa Waziri wa Nchi, uendelee.
MBUNGE FULANI: Aendelee nini?
WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, unaongozwa na Kanuni, kama Mheshimiwa Mbilinyi hataki kufuta usemi wake na Kanuni zinaeleza wazi kama Mbunge anaamrishwa hataki kufuta usemi wake, kwa nini usitumie mamlaka yako kwa Kanuni ya 5 ili uweze kufanya maamuzi sahihi? (Makofi)
(Hapa baadhi ya Wabunge walikuwa wakiongea bila mpangilio)
MBUNGE FULANI: Unakifundisha kiti, eeeh!
MBUNGE FULANI: Kwani mzuka maana yake nini?
MWENYEKITI: Samahani, samahani, naomba tusikilizane.
MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi, naomba ufute kauli yako.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, unapoomba unatarajia kupata au kukosa. Katika hili nimekataa kufuta kauli kwa sababu anachokisema nimesema sicho nilichosema. Nenda kwenye Hansard utaona maneno niliyoyaongea kwa ufasaha wake kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo umeamua nyuma, usubiri uende kwenye Hansard utaangalia, kama yakiwa maneno aliyosema Mheshimiwa Mama Waziri…
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi naomba utulie.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Ambaye yupo kwenye tatizo la generation gap basi ningefuta.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi naomba utulie.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Naomba na muda wangu ulindwe lakini.
MWENYEKITI: Sasa kwa sababu umekataa kufuta kauli, nasema tutakwenda kwenye Hansard kuangalia kimezungumzwa nini ili hatua ziweze kuchukuliwa. Tunaendelea, malizia dakika zako chache.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo dakika chache, ni dakika nyingi tu kwa sababu mmenikata wakati nikiwa kwenye dakika moja au moja na nusu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kujadili maendeleo bila demokrasia, bila ya utulivu wa kisiasa kwenye nchi. Rais anasema yeye ni Rais wa vyama vyote, alisema kwenye kampeni mpaka juzi yuko Arusha, naona anaongea na watu, anasema yeye ni Rais wa vyama vyote, lakini Waziri Mkuu wake yule pale anatukataza Wapinzani tusifanye mikutano ya vyama vyetu vya siasa. Demokrasia iko wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kujadili maendeleo bila demokrasia, bila uhuru wa vyombo vya habari, wanafungia magazeti kiholela tu, wanakuja wanazuia wananchi wasiangalie Bunge kwenye TBC ambayo ni Televisheni ya Taifa halafu anakuja Nape anataka kufananisha sisi na Sri Lanka. Hivi toka lini sisi tumewahi kufanya mambo yanayoshabihiana na Sri Lanka? Kwa nini usiige Marekani ambako kuna TV inayoonesha Senate saa ishirini na nne inayoitwa C-Span, iko maalum kwa ajili hiyo, halafu unakwenda kuchagua Weakest link, unaenda Sri Lanka, unaenda Australia, ambako hatushabihiani wala hatushirikiani katika mambo yoyote. Ukifananisha na tunavyoshirikiana na Marekani na tunaweza kuwaiga vitu vizuri kama hivyo wana channel inayoitwa C-Span ambayo inaonesha Bunge la Marekani masaa yote ndugu zangu.
Ndugu zangu katika suala la drugs hatuwezi kujadili maendeleo wakati nguvu kazi inazidi kuharibika. Sasa mimi najiuliza nguvu kazi inazidi kuharibika kwa dawa za kulevya, mmekomaa na ganja (bangi) kama alivyosema yule Mheshimiwa aliyepita, lakini mimi naomba….
MWENYEKITI: Samahani Mheshimiwa Mbilinyi.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Again? I can’t even speak eeh?
TAARIFA
MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.
MWENYEKITI: Mwanasheria Mkuu!
MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Kanuni ya 68(8), si kweli kwamba Mheshimiwa Waziri Mkuu amepiga marufuku vyama vya siasa visifanye shughuli zao za siasa na Mheshimiwa Waziri Mkuu aliifafanua vizuri hiyo hoja siku ya Alhamisi alipoulizwa swali na Kiongozi wa Upinzani hapa Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kutoa taarifa hiyo.
MWENYEKITI: Umeipokea taarifa Mheshimiwa?
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naikataa, Waziri Mkuu anatakiwa afute kauli yake kabisa na aseme vyama viko huru siyo kupindapinda, kwamba niliongea kama Mbunge, sijui niliongea kama nini, aseme kwamba ni ruksa kwa watu kufanya shughuli zao za kisiasa kama kawaida. Hicho ndicho anachotakiwa asema. Ingekuwa ni uongo angekanusha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunajaribu kusema, mnazungumzia dawa za kulevya, Rais Kikwete alimkabidhi Rais Magufuli ripoti ya kazi yake ya miaka kumi yenye kurasa 54. Miaka ya nyuma huko Kikwete alisema anayo majina, je, yale majina kwenye hii ripoti ya kurasa 54 hayakuwepo? Kama hayakuwepo kwenye hii ripoti ya kurasa 54 kulikuwa na nini basi labda wananchi tungeambiwa kwa faida ili tujue nchi inakwendaje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuje kwenye mipango ya maendeleo Kimataifa, safari za nje siyo tatizo. Kuna gharama nzuri na gharama mbaya. Gharama mbaya ni pale kama vile Kikwete alikuwa anaenda sijui anapokelewa sijui na Mkuu wa Shule, Mkuu wa Chuo, sijui anapokelewa na Meya, sijui anapokelewa na Mkuu wa Taasisi gani, lakini ni lazima ili tuende sambamba na dunia, sisi siyo kisiwa, lazima Rais Magufuli aende UN , lazima aende AU kwenye vikao vya Kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kuna Mkutano Davos wa Kimataifa, dunia yote iko kule inazungumzia uchumi, wewe umekaa huku, unasemaje Mipango ya Maendeleo. Kwa hiyo, kuna gharama mbaya na gharama nzuri. Gharama nzuri unakwenda Davos, unakutana kule na dunia, kina Putin na akina nani, mnajadili dunia inavyokwenda masuala ya uchumi, unatangaza na visima vyetu vya gesi kule kwa deal nzuri na vitu vingine kama hivyo ndugu zangu.
Kwa hiyo, gharama nzuri ni pamoja na kwenda Davos, kwenda UN, lakini pia kuangalia delegation iwe ndogo siyo kwenda na delegation ya watu 60, watu 70. Kwa hiyo, President Magufuli he has to go abroad akajifunze. Take a jet brother, he have to take a jet akajifunze dunia inafanya vipi, Marais wanafanya vipi, watu wapo Davos huko akina Putin, akina nani, yeye amekaa hapa. Apunguze delegation tu, aende na watu kama kumi na tano, 10 inatosha, aache kwenda na watu 60, 40.
Mheshimiwa Mwenyekiti, rasilimali watu mnasema mnaboresha wakati wafanyakazi bado wananyanyaswa, wanafukuzwa hovyo. Hapa leo niko Bungeni, tayari huko Mbeya Cement kwangu, kuna wafanyakazi wanapunguzwa. Mtu kafanya kazi miaka nane, anakuja kupewa 180,000/= ndiyo kiinua mgongo huko. Mnaboresha vipi masuala ya wafanyakazi. Umeme, naona hata kazi kuchangia hivi vitu in details kwa sababu miaka mitano nimechangia na mpaka leo bado tuko vilevile, ndiyo maana unaamua kutupia tu kama hivi. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la umeme, Profesa Muhongo, nimeangalia ukurasa wa 41 kwenye mpango wa umeme, nishati. Sijaona mpango wa umeme kutumia chanzo cha joto ardhi (geothermal), ambao dunia nzima inajua ndiyo umeme rahisi, kule Italy kuna kituo cha geothermal toka mwaka 1911 mpaka leo kinafanya kazi, wanabadilisha tu nyembe zile kwa sababau chanzo ni cha uhakika na cha maana zaidi. Katika hili, Serikali hii imeanzisha Kampuni, kuna meneja, kuna management wako kule Mbeya wamekaa hela hamuwapi wanahitaji dola milioni 25 kutuletea umeme huu nafuu, lakini ninyi mnakaa mme-mention hapa kila kitu mambo ya geothermal (joto ardhi) hamna, maana yake nini? Mtakwenda kesho mtawatembelea ofisini, mtasema hawafanyi kazi, mtawafukuza kazi, mnasema mmetumbua majipu wakati hela ya kufanyia kazi hamjawapa ndugu zangu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, nitoe angalizo kwa Mheshimiwa Waziri wa Fedha, nakufahamu siyo sana kwa kukufuatilia weledi wako, wewe ni technocrat, siyo mwanasiasa, usifuate hawa wanasiasa wanazomeazomea, tunaamini kwamba ukitulia, ukatumia nafasi yako kama technocrat ukacha cheap politics, populism, unaweza ukaisaidia nchi pengine na sisi tutaku-support ili twende vizuri. Ahsante sana. (Makofi)