Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja ya Dharura (Changamoto ya Kupanda kwa bei za Mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa)

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hoja ya Dharura (Changamoto ya Kupanda kwa bei za Mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa)

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, binafsi nikupongeze sana wewe, nikupongeze kwa hekima kubwa uliyoonesha ya kuruhusu jambo hili ambalo linawagusa Watanzania liweze kuzungumzwa na Waheshimiwa Wabunge huku tukiamini kabisa Waheshimiwa Wabunge ndiyo wawakilishi wa Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini la pili niwapongeze Waheshimiwa Wabunge wote takribani 17 ambao wamesimama, wamechangia vizuri sana haitakuwa busara ya kurejea tena yale ambayo yamezungumzwa.

Sasa ukiangalia hoja za Waheshimiwa Wabunge hapa maeneo mawili ndiyo yaliyoguswa, wamegusia role ya Serikali kuweka ruzuku, lakini la pili wamezungumzia suala la tozo kwenye bei ya mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hatukupaswa kufika hapa tulipofika kwa sababu tunazo Kamati; unayo Kamati yako ya Bajeti, una Kamati ya Nishati ambayo wangeweza kukaa na Serikali haya mawazo ambayo wamezungumza Waheshimiwa Wabunge wangeweza kuzungumza katika Kamati hizo. Lakini nadhani hatujachelewa, naomba nirejee maelezo ya Mheshimiwa Simbachawene aliyosema kwamba jambo la dharura linatatuliwa kwa dharura. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naiomba sana Serikali jambo hili linawagusa Watanzania takribani milioni 60 maisha haya ya Watanzania yanazidi kwenda juu kwa sababu ya gharama ya mafuta na hatujui vita ya Ukraine na Urusi itaisha lini.

Mheshimiwa Spika, wamezungumza watu hapa kwamba ipo sheria ya kuwalinda consumers, lakini nataka niseme hatuna sheria moja ambayo inamlinda consumer. Sasa Mheshimiwa Waziri Makamba amesema hapa kwamba ataleta regulation, lakini mimi nadhani way forward ya jambo hili tuwe na policy ambayo itaenda kutengeneza sheria ya kuwa na mfuko ambao ni imara kabisa, inapotokea dharura kama hii Serikali iweze kuchukua fedha pale na kuweka ruzuku katika maeneo kama haya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo mimi nimefarijika sana nikiamini kabisa suala hili limezungumzwa kwa mapana na niiombe Serikali, naamini kabisa chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ninyi Mawaziri mliopo hapa mnaenda kuleta majibu ya haraka ili watanzania waone kwamba Serikali yao inawajali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.